Upinzani nchini

Upinzani nchini

Pamoja na kwamba wamezuiliwa bado mi naamini kulikua na njia mbadala wa kudeal na hayo makatazo kwa njia ya amani na watawala wakawaelewa kuliko njia walizotumia za kutukana na kukejeli.

Ivi kweli Leo hii wewe mbunge wa chadema au mwanachama kamati kuu ya act wazalendo ukamkejeli mbowe au zito kabwe tuone kama atakuacha salama Basi vivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa watawala.

Kwa hiyo njia ya halali haikua ya kukejeli na kutukana.Hiyo ni sawa na enzi zile tulivyokua mashuleni tukidai kubadilshiwa vyakula hauwezi kufikisha ujumbe huo kwa kumtukana mkuu wa shule kwenye school baraza hata Kama hoja yako inamashiko lahasha kwa sababu hawezi kukusikiliza Zaid zaidi atakutimua shule kwa utovu wa nidhamu.
 
Wapinzani wa Tanzania wanafanya makosa obvious sana yanayowapunguzia credit hivyo kutoaminika Mbele ya jamii

1. wanahubiri democrasia halaf kwenye vyama vyao hawana hiyo democrasia

2. wanahubiri utawala wa sheria na kuheshim katiba wakati wao hawafati sheria na katiba za vyama vyao

3. wanahubiri sera za kupinga ufisadi na matumizi mabaya ya pesa wakat wao wanawakumbatia mafisadi na waliwapa hadi kugombea urais na kila mwaka wanapata hati chafu za CAG

4. wanapinga ukomo wa kugombea urais ila wao wameruhusu mwenyekiti wao asiwe na ukomo kugombea uenyekiti

5. hawana misimamo na kila siku wanaunga mkono juhudi sasa nani atawaamini
Hivi na wewe ujiona umetoa maoni!
 
Upinzani pamoja na figisu zote wanazofanyiwa unatakiwa kubadilika na kubadilika,mitazamo na aina ya siasa wanazozifanya kutoka kwenye siasa za kiharakati kua siasa za ukombozi zenye hoja mubadala kwa mustakabali wa nchi na zifike kwa wananchi.

Kuendelea kung'ang'ania kudai vitu ambavyo pengine wananchi walio wengi hawajui maana yake na faida zake ni kupoteza muda.

Hapa upinzani unatakiwa uje na hoja mbadala namna watayabadilisha maisha ya watanzania ikiwa ni pamoja na kueleza Sera zenye nguvu na mashiko kwa wananchi:

- Waeleze namna wataboresha huduma ya elimu ili ilete tija kwa watanzania wote tofauti na saizi ambapo mtu unasoma huna mbele Wala nyuma pengine hata fani unayosomea haujui faida zake na matumizi yake. Mbona watu waliosoma ulaya ni simple kutoboa kimaisha tofauti na huju kwetu tatizo liko wapi hapa wake na majibu na hoja za kueleweka.

- Waeleze namna gani wataongeza au kuboreaha mazingira ya ajira nchini ili kila mtanzania hata yule ambae hana degree 4 aweze kuajilika kutokana na elimu yake hatimae ajikwamue kimaisha.

- Waeleze namna gani wataboresha huduma za afya na upatikanaji wa vifaa tiba, dawa nk. ili ikiwezekana kila Mtanzania atibiwe kama sio bure basi kwa gharama ya chini sana ambayo ni affordable

- Waeleze namna gani wataboresha shule za kata zilizojengwa na serikali ya CCM ikiwa ni pamoja na kuzipatia vifaa vya maabara vya kutosha au kuzifanya zifanane na shule kongwe nchini ambazo kipindi cha nyuma ziliaminika ni shule za vipaji maalumu.

- Waeleze namna gani wataboresha sector ya michezo ili iwe mkombozi kwa watu wenye vipaji michezo lakini pia namna gani watavutia wawekezaji hata kama ni wazawa waweze kuwekeza katika michezo hatimaye kuanzisha accademy za michezo nchini. Ambapo michezo kwa wenzetu imetumika kama njia mbadala wa ajira.

- Waeleze namna gani watawasaidia vijana ambao wako katika harakati za kujenga nyumba namna gani serikal watakayokua wameiunda itawasaidia mabati, au sehemu yote ya upauaji.

Na mengine mengi hata kama yatakuwa sio ya kutekelezeka kwa muda mfupi bali hapa lengo ni kufikisha sera kwa wananchi ili imani iliyopotea irejee sasa kwa sababu siasa ni kuuza sera pamoja na purukushani kutoka chama tawala lakini ukiwa mjanja unafanya siasa katika mazingira hayo hayo.

Lakini pia pamoja na kuuza sera huko wasisahau kudai demokrasia na tume huru kwa pamoja mana kufanya hivyo bila demokrasia ni sawa na kulia chakula kwenye mzinga wa nyuki.
Hawajapewa muda wa kufanya hayo what next.................
 
Kwani mkuu CCM wanatumwa na mabwana zao wepi hao?
Akili yako inakomea kwenye vyama. Wenye upeo wanafikiri zaidi ya hapo, kwakuwa wanaotumika kutimiliza azma za mabwana nilio wataja, hawako kwenye vyama pekee, hata nje ya vyama; na kwa maana hiyo, sisi tunawapima kwa matendo yao. Wanaweza kuwa ndani ya vyama vyote vya siasa, taasisi za kidini, vyama vya kiharakati, vyama vya kitaaluma, taasisi za serikali n.k

Ni mara chache taasisi kusajiliwa ikijipambanua kuwa ni kuwadi au kibaraka wa mabwana hao, bali nia hiyo hujificha kwenye malengo mazuri yaliyo andikwa. Ili uwabaini, lazima uchunguze kauli zao, matendo yao, mienendo na tabia zao, n.k

Hivyo kwa kiwango kikubwa, viongozi katika vyama (upinzani) japo si wote, ila walio wengi na viongozi wakubwa, wameonesha pasi na shaka, kukengeuka katika utamaduni, imani, falsafa na desturi asili ya vyama hivyo na kuanza kuenenda, na kutamka yale ambayo kwayo, yanatufanya kujiridhisha kuwa sasa wako kwenye project ya mabwana wale; na ndiyo maana wameacha sasa kuhubiri na kusimamia yale ambayo mtoa mada ya msingi ameelezea na kuanza kubeba agenda zisizo wahusu watanzania bali mabwana wale.

Soma; Intarnational relations(by Emmanuel Wallestain).
 
Akili yako inakomea kwenye vyama. Wenye upeo wanafikiri zaidi ya hapo, kwakuwa wanaotumika kutimiliza azma za mabwana nilio wataja, hawako kwenye vyama pekee, hata nje ya vyama; na kwa maana hiyo, sisi tunawapima kwa matendo yao. Wanaweza kuwa ndani ya vyama vyote vya siasa, taasisi za kidini, vyama vya kiharakati, vyama vya kitaaluma, taasisi za serikali n.k
Kumbuka mwanzisha uzi anaongelea kuhusu wapinzani na ndani yake ametaja yale ya CCM. Tayari anaongelea vyama hata kama wengine wanahusika walengwa wakuu ni vyama vya upinzani. Mfano huu hapa chini.
- Waeleze namna gani wataboresha shule za kata zilizojengwa na serikali ya CCM ikiwa ni pamoja na kuzipatia vifaa vya maabara vya kutosha au kuzifanya zifanane na shule kongwe nchini ambazo kipindi cha nyuma ziliaminika ni shule za vipaji maalumu.
Kama uzi ni kuhusu wapinzani na wapinzani wakuu au wanaofahamika ni vyama sioni wewe unakikmbilia wapi. Ili hao unao waita mabwana zao wafanye yao na kieleweke vyama lazima vihusike (kwa siasa za Tanzania). Hivyo usijifanye wewe una upeo kuliko wengine kwenye hili kwani mada ya msingi ni kuhusu wapinzani, ili waje na sera mbadala kama mleta uzi anavyo shauri ni lazima vyama vihusike. Kumbuka hata wagombea huru hatuna Tanzania.
Swali langu-kwa vile wewe umeona wapinzani hawana agenda bali ajenda za bwana zao, yaani kwa ufupi unasema watanzania hawawezi kufikiri-sasa tuambie CCM wao wanafikiriwa na nani? Mabwana zao ni nani?
 
Wewe unaandika upupu gani?Upinzani bila hata ya kuwa na hoja zenye mashiko tayari wananchi wameshaichoka CCM.Wametawala karibu miaka 60 kwa ahadi zilezile zisizo na utekelezaji.Wananchi wanachohitaji ni nchi kuwa na demokrasia ya kweli.Wajichagulie viongozi bila kulazimishwa.Upinzani hata uje na Sera nzuri kiasi gani ,CCM bado hawatakubali kuachia madaraka.Kama Sera za upinzani zilizopo ni mbovu na CCM wanauhakika wanazo Sera nzuri waweke Mazingira sawa ya kufanya siasa na uchaguzi huru,tuone nini kitatokea!
Sawa wameichoka lakini pamoja na hayo wananchi hawaoni mbadala wa kuwapeleka nchi ya ahadi Mana wote wanaonekana ni wachumia tumbo tu.Yaani afadhali ya walioko madarakani kuliko hao
 
Sawa wameichoka lakini pamoja na hayo wananchi hawaoni mbadala wa kuwapeleka nchi ya ahadi Mana wote wanaonekana ni wachumia tumbo tu.Yaani afadhali ya walioko madarakani kuliko hao
Kama wananchi hawaoni mbadala CCM ingeacha tu sanduku la kura liamue kiuhalali tuone mambo yatakavyo kwenda.Acha kukaririshwa na fix za kina slowslow!
 
Una uelewa wa mambo na maarifa pia hoja lakini umekosea taget ulipoilekeza hoja yako
 
Wapinzani wakiendelea na sera zao za kujimwambafai watapuuzwa
Mzee wa kujimwambafai anajulikana kapiga kombati bila cheo chochote? Hivi alipitia hata jeshi la mgambo.
IMG_20191120_190036.jpg
 
Kumbuka mwanzisha uzi anaongelea kuhusu wapinzani na ndani yake ametaja yale ya CCM. Tayari anaongelea vyama hata kama wengine wanahusika walengwa wakuu ni vyama vya upinzani. Mfano huu hapa chini.

Kama uzi ni kuhusu wapinzani na wapinzani wakuu au wanaofahamika ni vyama sioni wewe unakikmbilia wapi. Ili hao unao waita mabwana zao wafanye yao na kieleweke vyama lazima vihusike (kwa siasa za Tanzania). Hivyo usijifanye wewe una upeo kuliko wengine kwenye hili kwani mada ya msingi ni kuhusu wapinzani, ili waje na sera mbadala kama mleta uzi anavyo shauri ni lazima vyama vihusike. Kumbuka hata wagombea huru hatuna Tanzania.
Swali langu-kwa vile wewe umeona wapinzani hawana agenda bali ajenda za bwana zao, yaani kwa ufupi unasema watanzania hawawezi kufikiri-sasa tuambie CCM wao wanafikiriwa na nani? Mabwana zao ni nani?
Nadhani kabla hujauliza usome aya yangu ya mwisho nilivyo hitimisha; ila inategemea upeo na utayari wa akili kuelewa.
 
Nadhani kabla hujauliza usome aya yangu ya mwisho nilivyo hitimisha; ila inategemea upeo na utayari wa akili kuelewa.
Bado inaongelea vyama na hili ndio msingi wa bandiko lako. Hoja ya upeo na utayari wa akili kuelewa hiyo ni ya kwako usihamishe magoli.
 
Bado inaongelea vyama na hili ndio msingi wa bandiko lako. Hoja ya upeo na utayari wa akili kuelewa hiyo ni ya kwako usihamishe magoli.
Sasa mbona ulisema kuwa swala hili nataka kulielekeza kwingine na sio vyama wakati hitimisho langu limetanabahisha kwa vyama vya upinzani? Ndiyo maana nikakuelekeza usome aya ya mwisho. Akili ikikosa utayari wa kuelewa madhara yake ni hayo.
 
Sasa mbona ulisema kuwa swala hili nataka kulielekeza kwingine na sio vyama wakati hitimisho langu limetanabahisha kwa vyama vya upinzani? Ndiyo maana nikakuelekeza usome aya ya mwisho. Akili ikikosa utayari wa kuelewa madhara yake ni hayo.
Uliandika: "Akili yako inakomea kwenye vyama. Wenye upeo wanafikiri zaidi ya hapo, kwakuwa wanaotumika kutimiliza azma za mabwana nilio wataja, hawako kwenye vyama pekee, hata nje ya vyama; na kwa maana hiyo, sisi tunawapima kwa matendo yao". Sioni hapa tunabishania nini. Ahsante na kwa heri.
 
Uliandika: "Akili yako inakomea kwenye vyama. Wenye upeo wanafikiri zaidi ya hapo, kwakuwa wanaotumika kutimiliza azma za mabwana nilio wataja, hawako kwenye vyama pekee, hata nje ya vyama; na kwa maana hiyo, sisi tunawapima kwa matendo yao". Sioni hapa tunabishania nini. Ahsante na kwa heri.
Lazima uage maana huna uwezo wa kujadili kwa akili bali kelele; sasa kona niliyokupeleka ni kwa wenye akili. Hata hivyo machache niliyokueleza yamekusaidia kuwa mstaarabu hata kwa kuaga kwa uungwana, nakushukuru sana.
 
Back
Top Bottom