Kabla hamjaanza kushutumu kuwa serikali ya awamu ya Tano inadhamira ya kuua na kuufuta upinzani nchini ni vema mkajiaangalia mienendo yenu na kisha mkajitathmini ni nani hasa ambae anataka kuutokomeza upinzani Nchini, ni serikali au Upinzani wenyewe?
Miaka ya 2005 ,2010 na 2015 upinzani ulijizolea umaarufu sana kwa wananchi kwa kuwa na sera bora ambazo zilijipambanua vyema kwa wananchi na wananchi walizielewa kwa urahisi kiasi cha kuwakubali na hivyo kujenga imani kwao.
Sera kama ya kupambana na mafisadi ambayo Dr. Slaa aliisimamia kwa nguvu zote au utawala wa kimajimbo ambayo Mbowe kamanda wa anga alikuwa akisimamia unaona kabisa zilikuwa zikivuta hisia kwa wananchi walio wengi. nakumbuka pia namna Dr. Slaa alivyokuwa anaweza kujenga hoja zenye ushahidi wa kutosha bungeni na nchi nzima Dr. Slaa na akina Zitto Kabwe walijipatia umaarufu kwa hoja kali Bungeni.
Hali imekuwa tofauti sasa upinzani leo hii ukiwaambia wawaeleze wananchi ajenda yao wanayo isimamia kama chama pinzani sina shaka kabisa kuwa hawana na kama wanayo basi hawana nguvu ya kuisimaimia mbele ya wananchi. mbaya zaidi hoja ambazo zilikuwa zinawapambanua na kuwatofautisha na chama tawala ndizo ambazo serikali au chama tawala ndio wanazitekeleza kwa nguvu zote na hivyo kuwafanya wakose hoja za kusimamia.
Ninachokiona kwa upinzani kwa sasa ni hoja za kudandia au bendela fuata upepo, leo ikija hoja ya korosho basi wapinzani wote watahamia katika mitandao ya kijamii na wataishupalia na kuonyesha umahili na ujuaji wao kuhusu suala husika, kesho lijitokeza suala la maduka ya kubadilishia fedha basi wanasahau korosho wanahamia maduka ya kubadilishia fedha.
Mwisho wa siku 2020 hii hapa. Magufuli atawaambia wananchi Mnaziona Barabara, Hospitali,Reli,Elimu bure, Upatikanaji wa umeme, madawa, maji nk.... sasa sijui nyie mtaonyesha nini?
Ninachokiona ni kuwa upinzani wamekosa watu wenye maono na uwezo mkubwa wa kuandaa sera na ajenda za kitaifa kama walivyokuwa enzi za kina Dr. Slaa na kundi lake hivyo kabla hawajaaza kumtafuta anaeua upinzani wajitafakali wenyewe na kuona wanaanguka wapi?
Magufuli Anachapa kazi na wananchi wanaona na vile vizuri anavyovifanya na nyie mnavipinga kwa kudai mnataka maendeleo ya watu badala ya vitu wananchi wanawashangaa pia.
Miaka ya 2005 ,2010 na 2015 upinzani ulijizolea umaarufu sana kwa wananchi kwa kuwa na sera bora ambazo zilijipambanua vyema kwa wananchi na wananchi walizielewa kwa urahisi kiasi cha kuwakubali na hivyo kujenga imani kwao.
Sera kama ya kupambana na mafisadi ambayo Dr. Slaa aliisimamia kwa nguvu zote au utawala wa kimajimbo ambayo Mbowe kamanda wa anga alikuwa akisimamia unaona kabisa zilikuwa zikivuta hisia kwa wananchi walio wengi. nakumbuka pia namna Dr. Slaa alivyokuwa anaweza kujenga hoja zenye ushahidi wa kutosha bungeni na nchi nzima Dr. Slaa na akina Zitto Kabwe walijipatia umaarufu kwa hoja kali Bungeni.
Hali imekuwa tofauti sasa upinzani leo hii ukiwaambia wawaeleze wananchi ajenda yao wanayo isimamia kama chama pinzani sina shaka kabisa kuwa hawana na kama wanayo basi hawana nguvu ya kuisimaimia mbele ya wananchi. mbaya zaidi hoja ambazo zilikuwa zinawapambanua na kuwatofautisha na chama tawala ndizo ambazo serikali au chama tawala ndio wanazitekeleza kwa nguvu zote na hivyo kuwafanya wakose hoja za kusimamia.
Ninachokiona kwa upinzani kwa sasa ni hoja za kudandia au bendela fuata upepo, leo ikija hoja ya korosho basi wapinzani wote watahamia katika mitandao ya kijamii na wataishupalia na kuonyesha umahili na ujuaji wao kuhusu suala husika, kesho lijitokeza suala la maduka ya kubadilishia fedha basi wanasahau korosho wanahamia maduka ya kubadilishia fedha.
Mwisho wa siku 2020 hii hapa. Magufuli atawaambia wananchi Mnaziona Barabara, Hospitali,Reli,Elimu bure, Upatikanaji wa umeme, madawa, maji nk.... sasa sijui nyie mtaonyesha nini?
Ninachokiona ni kuwa upinzani wamekosa watu wenye maono na uwezo mkubwa wa kuandaa sera na ajenda za kitaifa kama walivyokuwa enzi za kina Dr. Slaa na kundi lake hivyo kabla hawajaaza kumtafuta anaeua upinzani wajitafakali wenyewe na kuona wanaanguka wapi?
Magufuli Anachapa kazi na wananchi wanaona na vile vizuri anavyovifanya na nyie mnavipinga kwa kudai mnataka maendeleo ya watu badala ya vitu wananchi wanawashangaa pia.