Makanyaga
JF-Expert Member
- Sep 28, 2007
- 10,329
- 6,851
View attachment 656121
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Geita, Upendo Furaha Peneza (Chadema), ametaja sifa za mwanaume wa aina gani anayemhitaji maishani mwake amuoe,
Upendo ambaye kwa muonekano ni mrembo alisema kwa sasa hana mpenzi, mchumba wala mwanaume yeyote.
Alisema katika maisha yake anapenda sana mwanaume mpambanaji na mwenye kujituma katika kusaka mafanikio maishani bila kujali rangi, kabila wala dini.
Mbunge huyo kijana ambaye mwishoni mwa wiki iliyopita alitawala vyombo mbalimbali vya habari, ikiwemo mitandao ya kijamii kufuatia mkutano wake na waandishi wa habari akiponda vibaya kitendo cha wanasiasa kuhama vyama, hakutaka kuingia kwa undani sana katika maisha yake ya kimapenzi ingawa alikiri kuwahi kupitia maisha ya uhusiano kama binadamu mtimilifu na kwamba kwa sasa anamuomba sana Mungu ampe mwanaume wa haja yake ili kutimiza furaha maishani mwake.
“Sina chochote kwa maana ya mpenzi, mchumba au mwanaume wa aina yeyote na mara nyingi sana huwa sipendi kuzungumzia maisha yangu binafsi, lakini kikubwa napenda sana mwanaume mwenye kujituma kutafuta mafanikio na kwa kweli namuomba sana Mungu atimize haja ya moyo wangu ili niweze kufurahia maisha, unajua ukiwa na mwanaume mchakarikaji na wewe unahamasika kupambana zaidi na maisha,” alisema Peneza.
My Take
Ninazo sifa za kukuoa mama,mkisikia huyu kaolewa mjue ndio mimi maana kila nikitazama picha yako na yenyewe inanitazama
Naomba nikiri kuwa Mh. Mbunge mbali na kuwa smart kichwani, Mungu amemjalia hata katika maswala mengine, ni mzuri sana kwa sura pia!