Updates za yanayojiri kwenye Maandamano ya CHADEMA

Updates za yanayojiri kwenye Maandamano ya CHADEMA

Hela zinaibiwa na wezi wapo lkn hakuna wa kuwahoji. Komba kasema serikali 3 ataingia msituni hana wa kumhoji. Polis wameacha kazi wooote wamerundikana kwa mbowe. Kwani walikuwa na silaha gani? Jamani tunaenda wapi?
 
mimi namshauri mh. mbowe arudi jimboni kwake akajue shida za wananchi wake waliom
chagua. huu si mda wa maandamano
 
Huwa nacheka sana ninapoona Chadema wanavyoichezesha na kuichezea serikali ya CCM. Nacheka zaidi ninapoona jinsi serikali hiyo inavyokiogopa na kukichukulia Chadema kwa makini zaidi. Sasa hivi Serikali haithubutu kukipuuza chama hicho cha upinzani. Kwa mfano wakitamka tu kuandamana, Serikali inaacha shughuli zote na kuelekeza nguvu zake kwenye maandamano hayo. Sasa Chadema ikikohoa tu Serikali inasikiliza kwa makini sana. Hii maana yake ni nini? Inamaanisha kuwa Chadema si chama cha kufanyia mzaha. Kikitamka kitatumia Red Brigade kujilinda, Serikali inatumia vyombo vyake vyote kupiga kelele za kulaani. Kama Chadema inatamka tu kelele za Serikali zinakuwa hivyo, basi siku ikiacha kutamka na kuanza kutekeleza maazimio yake kwa vitendo basi Serikali yote itasimama.

Kama kweli Chadema si chochote wala si lolote, basi wapuuzeni. Mbona CCM na Serikali yake wanababaika kiasi hicho kufuatilia nyendo za Chadema. Kama Chadema ni wapuuzi, basi wapuuzeni. Msiseme kwa midomo tu kuwa ni wapuuzi, wapuuzeni kwa vitendo pia. Sasa nimeanza kuona tishio kubwa la Chadema kwa CCM—Tisho la wazi kabisa. Siipendi Chadema wala siipendi CCM, lakini nafurahia mchezo wa kisiasa ambao serikali ya CCM inachezewa na Chadema. Yaani Chadema wanaandaa mtego wa kisiasa na Serikali inanasa katika mtego huo.
 
Ni wakati mzuri kwa majambazi kuvamia mabenki na taasisi nyingine wajiibie wanavyotaka kwa sababu polisi wanatumikia siasa ya chama chao ccm na kuacha kufanya kazi inayotumia kodi za kila mtanzania ambayo waliajiliwa kufanya!
 
Mkuu kwa hilo tuko pamoja, Amani ya Nchi isihatarishwe na mhuni yeyote!

Mtaji wa kina Mbowe ni ujinga wa Watanzania. Tangu lini tajiri aliyejenga mijumba ya kifahari huko Dubai awapiganie maskini wasio na hata pakulala?.
 
Mimi nasema WAPIGWE TUUU...kwenye maandamano haya wakindaman Waislamu na wakipigwa Virungu MICHADEMA yoote humu inashngilia. Sasa zamu yao. PIGA HAOOOO mpaka watakapokuwa na adabu.

Mpuuzu wewe umezoea kuvuruzwa.
 
mimi namshauri mh. mbowe arudi jimboni kwake akajue shida za wananchi wake waliom
chagua
. huu si mda wa maandamano

Shida hizo ni Katiba ya Wananchi na kuepusha ufujaji wa fedha zao zinazotafunwa na Bunge Maalumu la Katiba. Au unazungumzia shida gani nyingine?
 
Waliokuwa wanasema jana kuwa kesho tutakuwa mstari wa mbele ndo wanaomba updates wapo na vi-keyboards,ukamanda ni shida

Kwa hiyo ukiandama hata simu unaacha nyumbani? Kwa kuwa wewe unapost ukiwa internet cafe basi una kila mtu ni kama wewe. Uboya mwingine bwana ni shida kweli.
Ova
 
Mtaji wa kina Mbowe ni ujinga wa Watanzania. Tangu lini tajiri aliyejenga mijumba ya kifahari huko Dubai awapiganie maskini wasio na hata pakulala?.

Halafu wenyewe wakiitwa makamanda wanajiona wanajeshi kweli
 
badala tuandamane bei ya unga imepanda eti tunamsindikiza mbowe watz bhana

Ngoja nikusidie kufikiri, maana wewe sijui unakitumia kichwa chako kwa kazi gani?
Ni hivi, nchi inahitaji ukombozi wa pili ndicho kinachofanywa na Chadema ikiongozwa na Mbowe, ndio maana tumemuunga mkono leo kwa maandamano. Ukipata ukombozi wa pili utashusha bei ya kila kitu sio bei ya unga tu.
Ova.
 
Back
Top Bottom