salosalo
JF-Expert Member
- Jun 7, 2012
- 596
- 278
TAFADHALI SANA NAOMBA MNAPO TOA TAARIFA HUMU NDANI ZIWE NI ZA UHAKIKA NA KAMA KUNA UWEZEKANO TOA CHANZO. MIMI NIPO UDOM, UTAWALA, MCHAKATO WA KUAJIRI UNANDELEA KAMA KAWAIDA, NA KILA IDARA IKO NA WATU WAKE, NA ZAIDI YA HAPO MAJINA YANAPITISHWA KWA WATU WA UTUMISHI, SASA KAMA WEWE UMEAMBIWA UTOE 500000 TSH, UNADANGANYWA, MAANA HII KAZI HAIFANYWI NA MTU MMOJA.
UKWELI NI KWAMBA APPLICANTS NI WENGI NA WENGI HAWANA VIGEZO, NI PAMOJA NA KUWA NA VYETI BATILI.
ANDIKENI UKWELI.:shock:
Usitetee kitu ambacho kiko uchi namna hiyo, mimi najua swala la rushwa kwa ajira za UDOM tangu nilipohudhuria usaili mwaka jana. palikuwa na watu zaidi ya 3000. Nafahamu jamaa yangu mmoja aliyeombwa rushwa na akatoa huku majina ya watu waliofaulu oral interview yakichakachuliwa na kuingizwa ya wale waliofaulu kupata connection ya kuhonga. Jamaa yangu mwingine alipambana sana ili apate kuhonga alishindwa maana hakuwa na connection, walimuogopa.
Kama yalifanyika mwaka jana kwa nini isiwezekane mwaka huu.
Tena nilisikia mkipokea pesa mnachomoa baadhi ya viambatanisho (nakala za vyeti) vya wenye sifa ili wapoteze sifa na watu wenu wapite. Kwendra huko