Updates: VodaCom Premier League 2009/2010

Updates: VodaCom Premier League 2009/2010

TIMU GANI ITAKUWA BINGWA WA LIGI KUU TANZANIA BARA(Vodacom Premier League)


  • Total voters
    72
  • Poll closed .
Ndo naangalia mechi za Fa pia,BOLTON 3 BIRMIHAN 2 MPIRA UMEISHA, BOLTON WANAFIKA NUSU FAINALI KWA MARA YA KWANZA
KATIKA KIPINDI CHA MIAKA 11,MAAJABU
 
mchezaji wa afc kaonyeshwa kadi nyekundu baada ya kumkanyaga kwa makusudi samatta
 
mpaka mwisho wa mchezo Yanga 0 na JKT 0
......AFC 0 na Simba 2...
 
Mechi kati ya simba na ilikubwa na utata hapa machana waleo kutokana kubadilishwa kwa kiingilio badala ya 3000 kwa 5000 na kuwa 5000 kwa 10000 hali iliyopelekea wapenzi hao kugomea mechi hiyo na kuzuia watu wengine kununua ticket mpka walipoingilia polisi na kuwa bembeleza ndipo walikubali kulipia 5000 huku wakionyesha kuimiss simba sana
IMG_2125.JPG
ticket ilivyochakachuliwa
IMG_2172.JPG
Mbunge wa Arusha mjini alitia timu na kupokelewa na wapenzi wake kwa fijo na ndelemo na mara baada ya mpira kuisha kulifanyika maandamano yasiyo na kibali sijui taarifa za kiinterejesia zinasema
IMG_2180.JPG
 
Leo ni Yanga na Azam FC kwenye uwanja wa Uhuru na hapa Arusha ni kati ya AFC iliyojihakikishia kushuka daraja zidi ya Mtibwa Sugar...
 
Kama Yanga atashinda mechi zote mbili zilizobaki na simba akashinda mechi yake moja iliyo baki basi ligi ya mwaka huu itaamuliwa kwa tofauti ya magoli, Simba ndiyo inaonekana kuwa kwenye nafasi nzuri zaidi kwani ina magoli 36 wakati Yanga ina magoli 26 kama inavyooneka hapo juu...
 
Picha ya ubingwa twaweza ipata baada ya dk 90 za mpambano wa leo...........................
 
Kama Yanga atashinda mechi zote mbili zilizobaki na simba akashinda mechi yake moja iliyo baki basi ligi ya mwaka huu itaamuliwa kwa tofauti ya magoli, Simba ndiyo inaonekana kuwa kwenye nafasi nzuri zaidi kwani ina magoli 36 wakati Yanga ina magoli 26 kama inavyooneka hapo juu...

Hapana mkuu Yanga ndo wana nafasi nzuri ya kuwa bingwa mkuu wangu mfumo unaotumika katika VPL kwa timu zinazofungana points ni kwa kuangalia Goal difference ambayo inapatikana kwa kuangalia tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa,kabla ya mechi ya leo Goal difference iko hivi: Simba wanefunga magoli 36 na wamefungwa 15(36-15=21) na Yanga wamefunga magoli 26 na wamefungwa 06(26-06=20) so kabla ya mechi ya leo goal difference ni Simba21-Yanga20=01(hii ni kabla ya mechi ya leo ya Yanga ambayo inaendelea na Yanga inaongoza kwa magoli 3-1)
 
Mpira umeisha Yanga 3 African Lyon 1

Kwa matokeo haya ni kwamba Simba wana ponti sawa na Yanga ila yanga anaongoza kwa goal difference ya 1(Simba kafunga magoli 36 na kafungwa magoli 15,goal difference ni 36-15=21,Yanga wamefunga magoli 29 na wamefungwa magoli 07,goal difference ni 29-07=22).Hivyo tofauti ya magoli ni 22-21=01

Bingwa ataamuliwa katika mechi za mwisho ambapo Simba itacheza na Majimaji na Yanga itacheza na Toto Africans
 
Hapana mkuu Yanga ndo wana nafasi nzuri ya kuwa bingwa mkuu wangu mfumo unaotumika katika VPL kwa timu zinazofungana points ni kwa kuangalia Goal difference ambayo inapatikana kwa kuangalia tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa,kabla ya mechi ya leo Goal difference iko hivi: Simba wanefunga magoli 36 na wamefungwa 15(36-15=21) na Yanga wamefunga magoli 26 na wamefungwa 06(26-06=20) so kabla ya mechi ya leo goal difference ni Simba21-Yanga20=01(hii ni kabla ya mechi ya leo ya Yanga ambayo inaendelea na Yanga inaongoza kwa magoli 3-1)

Mkuu
Ngoja nikusahihishe

Kabla ya mechi za jana na leo za Simba vs JKT na Yanga vs A.Lyon
Yanga wamefunga magoli 26 na kufungwa 6
Simba kafunga 35 kafungwa 15

Na kanuni zipo hivi
Kama timu zikifungana point basi kwanza kabisa itaangaliwa goal difference. Zikifanana basi itafuata ni sheria ya nani ana matokeo mazuri baina ya hizo timu mbili zilipocheza. Baada ya hapo then ndio wanaangalia nani ana magoli mengi ya kufunga
 
Back
Top Bottom