Huyu bibi amebobea kwa rushwa kumbe Sumeye alimtuhumu ukweli kua kagawa mahela kupata ujumbe wa nec ya ccm
Mary Nagu nusura
achomwe moto akigawa rushwa ya uchaguzi! Ilikuwa hivi, makamanda wa
CHADEMA wakiongozwa na Mbunge wa Karatu, Israel Natse na Mbunge wa Viti
Maalum, Pauline Gekul, walitonywa na askari wa miguu wa Kata ya
Bashanet, kuwa CCM wako mahali wameita watu na kuwafungia ndani ya
nyumba wakiwapatia rushwa ili wamchague mgombea wao.
Makamanda wa Ki-iraq wakapiga yowe kuita wenzao. Nyumba ikazingirwa,
watu wakitaka kuichoma moto, ndani yake akiwemo Nagu na Jitu Soni. CCM
wana hali mbaya sana katika kata hiyo ambapo CHADEMA na mgombea wake,
Lawrence Tara, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, wanakubalika
sana. Polisi kutoka Babati mjini na vijijini ndiyo wamefanikiwa
kumwokoa Nagu alfajiri ya leo, baada ya kuzingirwa usiku kucha.
Muda huu ndiyo Kamanda wa Anga, Mbowe anaelekea kata hiyo ya Bashnet
kwenda kufunga kazi, kisha atakwenda Dongobesh, Makuyuni, kisha Arusha
mjini, Uwanja wa Soweto Kaloleni.
Updates combination Tumaini Makene (Man of the
letters) na Mohamedi Mtoi.
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.
Last edited by a moderator: