Mohamedi Mtoi
R I P
- Dec 11, 2010
- 3,321
- 6,328
Mary Nagu nusura achomwe moto akigawa rushwa ya uchaguzi! Ilikuwa hivi, makamanda wa CHADEMA wakiongozwa na Mbunge wa Karatu, Israel Natse na Mbunge wa Viti Maalum, Pauline Gekul, walitonywa na askari wa miguu wa Kata ya Bashanet, kuwa CCM wako mahali wameita watu na kuwafungia ndani ya nyumba wakiwapatia rushwa ili wamchague mgombea wao.
Makamanda wa Ki-iraq wakapiga yowe kuita wenzao. Nyumba ikazingirwa, watu wakitaka kuichoma moto, ndani yake akiwemo Nagu na Jitu Soni. CCM wana hali mbaya sana katika kata hiyo ambapo CHADEMA na mgombea wake, Lawrence Tara, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, wanakubalika sana. Polisi kutoka Babati mjini na vijijini ndiyo wamefanikiwa kumwokoa Nagu alfajiri ya leo, baada ya kuzingirwa usiku kucha.
Muda huu ndiyo Kamanda wa Anga, Mbowe anaelekea kata hiyo ya Bashnet kwenda kufunga kazi, kisha atakwenda Dongobesh, Makuyuni, kisha Arusha mjini, Uwanja wa Soweto Kaloleni.
» Kamanda Mbowe amemaliza mkutano wa Bashnet sasa ngoma Dongobesh, Mbulu. Kama ilivyokuwa jana Muheza ambako mikutano ya CCM na CUF ilikufa kwa watu kwenda kusikiliza mikutano ya CHADEMA, leo pia mkutano wa CCM hapa Bashnet umekufa, watu wamekimbilia kumsikiliza Mbowe.
Mwenyekiti ametoa kauli nzito hapa Bashnet akionya mchezo mchafu wanaofanya CCM Monduli wa kuanza kukodi vijana ili wakawafanyie fujo watu wa CHADEMA, amesema kama vijana wa CHADEMA nao watapewa amri ya kulipiza matendo ya CCM itakuwa ni songombingo ambayo itaharibu nchi.
CHADEMA hawako tayari kuona damu ya Mtanzania yeyote ili mtu mmoja awe diwani, lakini kwa mambo ya CCM kuanza kufanya vurugu huku vijana hao wakilindwa na polisi, itafika mahali haitakubalika! Amesema ''vijana wa CCM nchi nzima ni 10% wakati wale wa CHADEMA ni 90%, amewataka waache mara moja.
Nape amepita hapa nusu saa kabla Mkiti Mbowe hajatua, watu walimzomea. Walikuwa na wapambe na masare yao. Mbowe alipofika, wananchi wachache waliokuwepo kwenye mkutano wake wakaondoka kwenda CHADEMA.
» More update
Tunatoka Kata ya Makuyuni, sehemu inaitwa Mbuyuni. On the way to A-City kwa ajili ya kata nne za mjini. Finalization. We are so hopeful here. Lowassa is so desperate than ever before. Ametafuta yale magari makubwa ya kubeba ng'ombe kwenda Dar, ili kusomba watu hadi kutoka Meru. Bado 'imebuma'. Ajiandae kwa goli la nne. Goli la kwanza: alimleta Batilda Buriani Arusha mjini, akapigwa, akamleta mkwe wake Sioi, Arumeru Mash., akapigwa, akamleta mtu wake pale Daraja Mbili, udiwani, akapigwa, kesho akipigwa ni goli la nne.
Helkopta inarusha vipeperushi hapa mjini Makuyuni. Tunaitafuta Arusha. Dogo janja kakabidhiwa majukumu hapa. Anasema amekuwepo kwa wiki 2 sasa, makamanda wamefanya kampeni ya nyumba kwa nyumba, mtu kwa mtu. Mbowe amesema uchaguzi huu unakwenda kuwa kielelezo kingine cha Watanzania kukataa udhalimu wa watawala na kujiandaa kuwaondoa kabisa madarakani 2014-2015.
Updates combination Tumaini Makene (Man of the letters) na Mohamedi Mtoi.
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.
Makamanda wa Ki-iraq wakapiga yowe kuita wenzao. Nyumba ikazingirwa, watu wakitaka kuichoma moto, ndani yake akiwemo Nagu na Jitu Soni. CCM wana hali mbaya sana katika kata hiyo ambapo CHADEMA na mgombea wake, Lawrence Tara, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, wanakubalika sana. Polisi kutoka Babati mjini na vijijini ndiyo wamefanikiwa kumwokoa Nagu alfajiri ya leo, baada ya kuzingirwa usiku kucha.
Muda huu ndiyo Kamanda wa Anga, Mbowe anaelekea kata hiyo ya Bashnet kwenda kufunga kazi, kisha atakwenda Dongobesh, Makuyuni, kisha Arusha mjini, Uwanja wa Soweto Kaloleni.
» Kamanda Mbowe amemaliza mkutano wa Bashnet sasa ngoma Dongobesh, Mbulu. Kama ilivyokuwa jana Muheza ambako mikutano ya CCM na CUF ilikufa kwa watu kwenda kusikiliza mikutano ya CHADEMA, leo pia mkutano wa CCM hapa Bashnet umekufa, watu wamekimbilia kumsikiliza Mbowe.
Mwenyekiti ametoa kauli nzito hapa Bashnet akionya mchezo mchafu wanaofanya CCM Monduli wa kuanza kukodi vijana ili wakawafanyie fujo watu wa CHADEMA, amesema kama vijana wa CHADEMA nao watapewa amri ya kulipiza matendo ya CCM itakuwa ni songombingo ambayo itaharibu nchi.
CHADEMA hawako tayari kuona damu ya Mtanzania yeyote ili mtu mmoja awe diwani, lakini kwa mambo ya CCM kuanza kufanya vurugu huku vijana hao wakilindwa na polisi, itafika mahali haitakubalika! Amesema ''vijana wa CCM nchi nzima ni 10% wakati wale wa CHADEMA ni 90%, amewataka waache mara moja.
Nape amepita hapa nusu saa kabla Mkiti Mbowe hajatua, watu walimzomea. Walikuwa na wapambe na masare yao. Mbowe alipofika, wananchi wachache waliokuwepo kwenye mkutano wake wakaondoka kwenda CHADEMA.
» More update
Tunatoka Kata ya Makuyuni, sehemu inaitwa Mbuyuni. On the way to A-City kwa ajili ya kata nne za mjini. Finalization. We are so hopeful here. Lowassa is so desperate than ever before. Ametafuta yale magari makubwa ya kubeba ng'ombe kwenda Dar, ili kusomba watu hadi kutoka Meru. Bado 'imebuma'. Ajiandae kwa goli la nne. Goli la kwanza: alimleta Batilda Buriani Arusha mjini, akapigwa, akamleta mkwe wake Sioi, Arumeru Mash., akapigwa, akamleta mtu wake pale Daraja Mbili, udiwani, akapigwa, kesho akipigwa ni goli la nne.
Helkopta inarusha vipeperushi hapa mjini Makuyuni. Tunaitafuta Arusha. Dogo janja kakabidhiwa majukumu hapa. Anasema amekuwepo kwa wiki 2 sasa, makamanda wamefanya kampeni ya nyumba kwa nyumba, mtu kwa mtu. Mbowe amesema uchaguzi huu unakwenda kuwa kielelezo kingine cha Watanzania kukataa udhalimu wa watawala na kujiandaa kuwaondoa kabisa madarakani 2014-2015.
Updates combination Tumaini Makene (Man of the letters) na Mohamedi Mtoi.
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.
Last edited by a moderator: