Update ya siku ya upanda miti leo Oktoba mosi

Update ya siku ya upanda miti leo Oktoba mosi

Mwanapropaganda

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2014
Posts
4,235
Reaction score
2,512
Kama mheshimiwa makonda, mkuu wa mkoa wa Dar es salaam alivyotangaza kuanza upandaji miti maeneo mbalimbali ifikapo siku ya leo ya oktoba mosi.

Wale mlio kwenye shughuli hiyo muhimu kwa ustawi wa mazingira tupeane taarifa ya zoezi linavyokwenda, vile vile kuwajulisha wengine sehemu ambayo miche ya miti inatolewa kwa wanaopanda miti.

OKTOBA MOSI NDIO LEO.
 
Anataka watu wapande miti hadi kwenye lami..mwingine nyumba yake haina hata nafasi tokana na kiwanja kilivyo unamwambia apande miti
 
miche na maeneo yakupandia ni changamoto wengi wa wakazi wa dar ni wapangaji na wafanya biashara maeneo hawana pia gharama za kununua miti na upatikanaji wake ni changamoto watapanda wachache inatosha
 
Makonda kama naibu amiri jeshi mkuu vile,maana askari mara wanafagia barabara,mara kupima afya watu mara kupanda miti kwa 'maagizo' yake
 
Kuna yeyote aliepanda mti? Tupigie picha uiweke hapa.!

Vipi yale mazoezi ya Mtaani yanaendelea bado?
 
wewe utaopanda mti wakati maji ya kumwagilia huna? lazima haya mambo mawili yaende sambamba, Dar ni kame, jua la siku moja tu linakausha kila kitu. nasubiri hoja ya maji Dar
 
Back
Top Bottom