Update: Lema kufikishwa Mahakamani Jumatatu

Update: Lema kufikishwa Mahakamani Jumatatu

Kwenye suala la mahakama CCM watupu maana kule ni hoja kwa hoja sio blah blah
Lema kuwa makini huu ni mkakati wa kukupotezea mda ili mwisho wa siku ukose mda wa kuwatumikia wananchi wako
Take care
 
Hivi kwanini watanzania tusifuate mfano wa wananchi wa Misri,Tunisia na Libya?

Kuna haja gani ya kuendelea kuwavumilia hawa watawala wanaofanana na madikteta?
4 sure kwani tunangoja nini?am tired with this stupid ccm;;;;;tired nalia kabisa kwanini wenzetu wanateseka kwa kupigania haki zetu?hivi hii nchi c yetu sote?am tired with ccm
 
wanazidi kumpa Lema umaarufu zaidi
kwa sisi wanasheria kutokumpa dhamana eti kwa vile mashtaka dhidi yake yamekamilika ni umbumbumbu
wa sheria
Dhamani huweza kutolewa muda wowote iwe na polisi au mahakama kama shtaka lake lina dhamana
tena mbunge mtu wa watu sijaona mantiki ya kumnyima dhamana.
Kesi hii itawaumbua zaidi CCM na inazidi kuwachonganisha na wananchi.
Matendo yao watayajutia 2015.
 
-Mhusika wa mauaji hafuatiliwi!
-Lema j3 anatakiwa awe bungen!
-Hamna tume iliyoundwa!
-Miaka yote hata mchawi akiua msibani lazma atalia/kutoa pole
-lkn huyu Mulongo kaenda kufanya kuperka siasa msibani ili
kukoreza hasira za watu ili wampate mtu waliompangia!!
hapa kuna kitu either nyuma ya pazia sio bure!
Nyway tme will tell!!

lk tutiane moyo kwa maandiko haya na pia huwa nafarijika nipitiapo haya maandiko kuwa
Mungu hawezi kuwaacha watz wenzangu
-_-Mhubiri 5:8 ujapokuwa unaona maskini kuonewa, na hukumu ya haki kuondolewa kwa jeuri ktk jambo, usilistaajabie jambo hilo; kwa 7bu, Aliye juu kuliko walio juu huangalia;
Tena wako walio juu kuliko wao.
 
Kwetu sisi wanasheria hii ni kesi rahisi sana kushinda,serikali inaenda kupigwa mweleka mkali sana asubuhi na mapema.
 
Mbona ni Godbless Lema tu kila mara? Chadema Ina wabunge 23 wa kuchaguliwa lakini hawakamatwi isipokuwa Lema! Picha ya kuwa mbunge lakini ni Raia . Ni lazima atii sheria na kuwa mfano kwa wananchi waliomchagua. Hauko juu ya sheria.


Kwani kosa lake ni lipi ?,mbona unamhukumu moja kwa moja?
 
Mkuu wahenga walisema kipenda roho hula nyama mbichi,kwako wewe Lema ni malaika.
Kama waona Lema ana ubavu wa kupimana na Mkuu wa Mkoa basi sisi tutabaki kuwa watazamaji.

Picha inaendelea, Lema yuko lupango na Mkuu anapeta.
Haihitaji akili nyingi kuelewa nani anaumia.
Anapetaje Ilhali kila Anapopita watu wanazomea, what kind of Life is that??????
 
Point ni ipi hiyo unayotaka kumchagulia kuchangia. Mkuu huwezi kuweka bandiko hapa JF na kuwa 'SELECTIVE' kwa yale unayopenda watu wayaongee na kuchangia. This is JF. Hakuna kutishana nyani au Nyani ngabu kama miafrika tulivyo.

You can ignore him but you can't shanty him.

Vijana wa Lumumba,
Mie sio Size yenu Jaman, Thread ninazo zifunguaga huwaga zinawawia Vigumu Kuzielewa Hence kuchelewesha Malipo Yenu Kutoka Lumumba.
Post za Great Thinkers wa JF ni za Kufikirisha sana Kichwa
Sasa kwa Vichwa Panzi/ Samaki kama nyie sana sana Vichwa vyenu vita Over Heat katika tu Kujaribu kuelewa Content Ya Thread.
Mnahitaji Kumwagiwa Maji Vichwani for Cooling.
Naona Mnataka Kusafiria Nyota za Great Thinker wa JF wanaoweka Post za Kufikirisha Vichwa Ku Jibu Utumbo ili Japo Siku Ipite.
Then Mpeleke Feedback Lumumba Kwa Kujinadi, Oooh,leo Nimemjibu shardicle , mie Nimemjibu yegella, oooh mie nimemtusi Crashwise,
Oooh mie nimetusi Arushaone, Oooh, mie Mzee Mwanakijiji Ka Quote ----- wangu ,Ona mie EMT Kajibu Post yangu na Mengine Meengi tu.
Dawa yenu ni kuwa Puuza tu.
 
Hofu yangu huyo Mkulu asije akaamrisha unga wa Mwakyembe kwa Lema manake yule baba ana roho mbaya unapeleka majeshi kwa mtu mmoja yeye na familia yake kama vile haini huyo mulugo hana akili pia wakati huu asingethubutu kufanya hayo
 
Hivi kwanini watanzania tusifuate mfano wa wananchi wa Misri,Tunisia na Libya?

Kuna haja gani ya kuendelea kuwavumilia hawa watawala wanaofanana na madikteta?
Anza ww kuiga ya misri, mmezoea kuiga hamtumii akili umbulula huo! Nyie mna akili za gong'onda.
 
MAMBO yamezidi kumwendea kombo Mbunge wa Arusha Mjini, (Chadema) Godbless Lema baada ya Jeshi la Polisi kutangaza rasmi kwamba itamfikisha Mahakamani, siku ya Juma tatu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Liberatus Sabas amema kwamba Mbunge huyo hawezi kuachilia huru kwa sababu mashtaka dhidi yake yameshakamilika na atafikishwa Mahakamani siku ya Juma tatau.

"Hatuwezi kumwachia kwa sababu anatarajia kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili"alisema Sabas.

Wakati Kamanda huyo akitoa msimamo huo, taarifa za ndani ya Jeshi hilo zinaeleza kwamba Mbunge huyo amehojiwa kwa zaidi ya saa nane sasa na bado yuko katika chumba maalum kwa mahojiano zaidi na maofsa wa Polisi huku akitakiwa kuonyesha ujumbe mfupi wa vitisho aliyodaiwa kuwa ametumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo.

Katika hatua nyingine Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Arusha, kimekuwa na kikao kirefu kinachoongozwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo na kwamba ajenda kubwa inayojadiliwa ni tukio zima la vurugu zilizotokea katika Chuo cha Uhasibu mkoani humo.

Lema alikamatwa usiku wa kuamkia leo baada ya Askari wa Jeshi la Polisi kumfuata nyumbani kwake na kuzingira nyumba yake kabla ya zoezi la kumchomoa ndani ya nyumba hiyo kufanyika.

Mbune huyo anatuhumiwa kwa makosa mbalimbali ikiwemo kosa la kuchochea vurugu katika chuo hicho baada ya kutokea mauaji ya Mwanafunzi Henry Koga aliye uawa kwa kuchomwa kisu juzi akirejea chuoni hapo kutoka kwenye matembezi yake, hata hivyo haijajulikana mara moja sababu za kuawa kwa mwanafunzi huyo wala watuhumiwa hawajakamatwa.

My Out Look:
Nazidi kuyasadiki Maneno ya Rafiki yangu SSP Chuwa kuwa Tatizo sio Mulongo.

Yeye ana execute to Matakwa ya Mkulu Dhidi ya Lema.

Ile Issue ya Lema kumpa Live Mkulu kuwa analea Udini imemchoma sana Mkulu.

Rafiki Yangu SSP Chuwa Akaongeza, "CCM ni Wepesi Mno na Weupe Suala linapofika Mahakani"

Wao wana Mamlaka na Fedha, Lema ana Mungu
Hapo kwenye rangi Nyekundu inaonyesha jinsi mkuru anavyotumia madaraka yake vibaya lakini hapo kwenye Njano inaonyesha jinsi Mungu anavyopigania watenda haki.

Hakika kitaeleweka hata kama watwafunga viongozi wa CHADEMA​ wote.
 
serekali ya ccm ina ondoa amani ya nch taratibu...pia wanajenga ukuta kati yao na wananch
 
Sina uoga wowote ila mimi sio bendera fuata upepo kama wewe .

Unapokua huna unachosimamia kama misingi ya utu huwa unadhani wengine walionacho wanafuata upepo!!

Watu wa aina hii huwa wanaamka maslahi yao yanapoguswa!
Sikulaumu,maana najua hata kule tulikoona umma umetaka mabadiliko wapo waliopinga pia!
 
Only one man Prophet Lema amesababisha Radio call nchi nzima zinafoka ! Kweli nimeamini Mbunge Mmoja tu wa Cdm ana thamani ya polisi 200 wa Tanzania ! Swali la kizushi ni kwamba kwa mwendo huu , tutaweza kulikomboa Ziwa Nyasa kutoka Malawi ?
 
Badala ya mimi kutafuta hela niisaidie familia yangu eti nikaandamane . Huu ni upuuzii uliotukuka . Wajinga ndio wafuate mawazo yako .

wewe ni mkuu wa mamburura wote kama hujui umuhimu wa siasa kwenye maisha yako
 
Umeteleza sana unaposema kuwa mambo yamemuendea kombo kamanda Lema.(nitake radhi tafathali)
Mimi kama mpiga kura wa arusha nimemchagua Lema apambane kwa ajili ya haki kwa kila raiya, kama kiongozi kabla hajapmabania haki za raiya ni lazima apambanie haki zake bila uoga na kutoa mfano kwa vitendo namna ya kukomesha vitendo vya kukandamiza haki na demokrasia na huu ndo uwajibikaji dhidi dhuluma za dola.
Lema tumemchagua aingie mpaka magerezani akaone na kushiriki kutatua changamoto za wapiga kura na baada ya hapo Mungu atajidhihirisha mbele ya dunia nzima pamoja na Mulongo Magessa a.k.a Faraoh.
May God blessGodBless Lema.

NB: Tukianza kufunguliana kesi za uongo zenye nia ya kukandamiza demekrasia tuhakikishe tunakuwa na pesa zakutosha maana always mahakamani CCM na ushetani wake wote huambulia patupu kwasababu mahakama sio chombo cha propaganda so imani ni kubwa kuwa tunakwenda kumuaibisha shetani kwa mara nyingine tena.
 
Back
Top Bottom