Update: Lema kufikishwa Mahakamani Jumatatu

Update: Lema kufikishwa Mahakamani Jumatatu

Kama ni Arusha hii lazima tuitafute haki ya mbuge wetu lema kwa njia yeyote ile na hawa ccm wanazidi kujichimbia kaburi hapa A. City kiukweli na si propaganda.
 
Freedom is coming, hizo ni dalili za mwisho watanzania kuwen tayari kuipokea tanzania mpya 2015!
 
MAMBO yamezidi kumwendea kombo Mbunge wa Arusha Mjini, (Chadema) Godbless Lema baada ya Jeshi la Polisi kutangaza rasmi kwamba itamfikisha Mahakamani, siku ya Juma tatu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Liberatus Sabas amema kwamba Mbunge huyo hawezi kuachilia huru kwa sababu mashtaka dhidi yake yameshakamilika na atafikishwa Mahakamani siku ya Juma tatau.

"Hatuwezi kumwachia kwa sababu anatarajia kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili"alisema Sabas.

Wakati Kamanda huyo akitoa msimamo huo, taarifa za ndani ya Jeshi hilo zinaeleza kwamba Mbunge huyo amehojiwa kwa zaidi ya saa nane sasa na bado yuko katika chumba maalum kwa mahojiano zaidi na maofsa wa Polisi huku akitakiwa kuonyesha ujumbe mfupi wa vitisho aliyodaiwa kuwa ametumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo.

Katika hatua nyingine Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Arusha, kimekuwa na kikao kirefu kinachoongozwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo na kwamba ajenda kubwa inayojadiliwa ni tukio zima la vurugu zilizotokea katika Chuo cha Uhasibu mkoani humo.

Lema alikamatwa usiku wa kuamkia leo baada ya Askari wa Jeshi la Polisi kumfuata nyumbani kwake na kuzingira nyumba yake kabla ya zoezi la kumchomoa ndani ya nyumba hiyo kufanyika.

Mbune huyo anatuhumiwa kwa makosa mbalimbali ikiwemo kosa la kuchochea vurugu katika chuo hicho baada ya kutokea mauaji ya Mwanafunzi Henry Koga aliye uawa kwa kuchomwa kisu juzi akirejea chuoni hapo kutoka kwenye matembezi yake, hata hivyo haijajulikana mara moja sababu za kuawa kwa mwanafunzi huyo wala watuhumiwa hawajakamatwa.

My Out Look:
Nazidi kuyasadiki Maneno ya Rafiki yangu SSP Chuwa kuwa Tatizo sio Mulongo.

Yeye ana execute to Matakwa ya Mkulu Dhidi ya Lema.

Ile Issue ya Lema kumpa Live Mkulu kuwa analea Udini imemchoma sana Mkulu.

Rafiki Yangu SSP Chuwa Akaongeza, "CCM ni Wepesi Mno na Weupe Suala linapofika Mahakani"

Wao wana Mamlaka na Fedha, Lema ana Mungu

===================
Kinachojiri Mahabusu
===================



sawa mkuu tunasubir mrejesho jf kama kawaida m4c itasima tu wapende wasipende
 
Tunasubiri hizo charge sheet wakimfungulia mauaji..wakae wajue nao wataondoka arusha mmoja mmoja!ni aibu sana sana hata wakimfunga Lema CCM hawana chao Arusha na hivi wanajipa wakati mgumu zaidi Arusha na nchi nzima!udini upo ndani ya JK kama aseme Lema ama mwingine yeyote!
 
Kipanya Anaongea kwa Lugha ya Picha hali si shwari
kp27042013.jpg
 
mamakamani wanaenda watu na ni kwa ajili ya watu tusubiri hayo mashitaka kesi nyingi kwa wanasiasa wa upinzani zimeenda mahamani lakini zinaisha kimya kimya, na hawazitangazi zimeisha ni kama vichekesho lakini hatufikiri kama garama inatumika pasipokuwa na tija
 
Kwa sababu kuna watu walioko CCM na serikalini wanapitia huku,nadhani ni muda muafaka wa kumweleza Rais wetu wa Jamhuri ya Tanzania kuwa kinachoendelea chini ya himaya yake kinamatokea hasi,basi awawajibishe watu wake watende haki ,vinginevyo kwanye shimo la panya hata nyoka huwa wanaingia,wasitegemee vurugu itakapoaanza ni watu maskini na wanyonge tu ndio wataadhirika hata wenye pesa zao pia.
 
Siku zote haki huwa hishindwi kwa dhuluma...huwa inachelewa tu lakini itafika na katika kutafuta haki hiyo wengine watapata shida na mateso na manyanyaso mbalimbali hadi kupoteza maisha yao ila ni kwa sababu wanatetea wengine....nampa hongera sana kiongozi G.lema na makamanda wote kwa yote yanatokea kamwe tusirudi nyuma...Mungu mwema awabariki sana makamanda.......
 
Huyu anaemtuma Mulongo na haya mambo nadhani hajitambui,na haujuhi Watanzania wa mtaani wamechoka kiasi gani,muda si mrefu yatakuja timia yale maneno ya Mwl Nyerere yatatimia!wanajaribu kucheza na akili za Watanzania waone reaction yao!ila sasa inaelekea mwisho na uoga umeanza kuwatoka watu!hawalielewi ilo,ila hata wao hawatakua salama mambo yakìaribika
 
Hujui kuwa kama system ikiwa nzuri hata hauitaji kutoa jasho ili kufanikiwa? . Jiunge na wenzako uboreshe maisha yako na ya kizazi chako.Hii ni kama uko sincere na wewe siyo imposter!

yani usubirie tu uboreshewe maisha
funguka bado upo gizani acha ujinga wewe siku zote even bilble say utakula kwa jasho lako
 
Kwa sababu kuna watu walioko CCM na serikalini wanapitia huku,nadhani ni muda muafaka wa kumweleza Rais wetu wa Jamhuri ya Tanzania kuwa kinachoendelea chini ya himaya yake kinamatokea hasi,basi awawajibishe watu wake watende haki ,vinginevyo kwanye shimo la panya hata nyoka huwa wanaingia,wasitegemee vurugu itakapoaanza ni watu maskini na wanyonge tu ndio wataadhirika hata wenye pesa zao pia.

Sidhani kama ilo wazo lako kuna mtu ambae atalizingatia japo watu wa taasisi ya raisi wanapita humu,bado hawaamini na hawajielewi kabisa,nadhani haya ndio yanaelekea kutimia: “Siku inakuja ambapo watu watachagua kifo kuliko fedheha na ole wao wale watakoiona siku hiyo! Na ole wao wale watakaoifanya siku hiyo isiepukike. Natumaini na kusali kuwa siku hiyo kamwe haitofika” –MwalimuNyerere (Januari, 1966)
 
Mkuu wahenga walisema kipenda roho hula nyama mbichi,kwako wewe Lema ni malaika.
Kama waona Lema ana ubavu wa kupimana na Mkuu wa Mkoa basi sisi tutabaki kuwa watazamaji.

Picha inaendelea, Lema yuko lupango na Mkuu anapeta.
Haihitaji akili nyingi kuelewa nani anaumia.
Kwani lupango ni watu wa namna gani wanaokaa humo siyo watanzania? je hakuna wapiga kura wake humo? je huoni kama wanahitaji kupata mawazo yake?...Mhe Lema alishaenda magereza mwenyewe baada ya kukataa mdhamana hivyo kwa Lema kumtishia Lokapu ni upumbavu mtupu..ngoja zamu yenu ikifika...
 
Kwani lupango ni watu wa namna gani wanaokaa humo siyo watanzania? je hakuna wapiga kura wake humo? je huoni kama wanahitaji kupata mawazo yake?...Mhe Lema alishaenda magereza mwenyewe baada ya kukataa mdhamana hivyo kwa Lema kumtishia Lokapu ni upumbavu mtupu..ngoja zamu yenu ikifika...
Mkuu naamini wewe ni mtu mwenye akili timamu.
Nikuulize jambo na pengine orientation yako kiakili inaweza kuwa jolted.

Hivi kuna wakati huko mbele ya safari mbunge wenu anaweza kufanya kitu kwa akili kidogo bila kuchezea lockup na ujembe wake bado ukafika kiufasaha?
Hapo ndo umuhimu wa shule!
 
Hapa wakimpa kesi ya mauaji Mji hautakalika.
Hawawezi kumpa kesi ya mauaji. Sana watasema alichochea wanachuo kumfanyia vurugu mulongo. Prosecutors wamweke mulongo kama mmoja wa mashahidi akatoe ushahidi.
 
katika vitabu vyote vya dini zote hakuna mahali ambapo shetani na wafasi wake waliwahi mshida MUNGU na wafasi wake. Mlogo hakuna mahali ambapo alifanya vizuri katika utumishi wake. JK siku akiachia ngazi na Mlongo ataishia hapo hatakuwa kiongozitena katika nchi hii. JK ni gaidi na matendo yake ni ya kishetani na ndiyo maana nchi imejaa malalamiko kila kona. Kazi ya shetani ni kujinja na kuua ndicho anachokifanya agent wake JK na Mlongo.
 
Hivi kwanini watanzania tusifuate mfano wa wananchi wa Misri,Tunisia na Libya?

Kuna haja gani ya kuendelea kuwavumilia hawa watawala wanaofanana na madikteta?

Tuandamaje kuwatetea wachochezi wa vurugu na udini?
 
jamani naomba msaada kujuwa hatima ya lema ya kusumbua jeshi la taifa na kuchochea vurugu atapona kweli pamoja na vijana wa arusha kutaka kumtetea......chama ambacho kinaangaliwa sasa hivi kuwa kiinaweza leta mabadiliko baadae member wake wanafanya mambo ya namna hiyo
 
jamani naomba msaada kujuwa hatima ya lema ya kusumbua jeshi la taifa na kuchochea vurugu atapona kweli pamoja na vijana wa arusha kutaka kumtetea......chama ambacho kinaangaliwa sasa hivi kuwa kiinaweza leta mabadiliko baadae member wake wanafanya mambo ya namna hiyo

Umeshakunywa chai?
 
Back
Top Bottom