Uongozi CHADEMA umeshindwa kusimamia chama

Uongozi CHADEMA umeshindwa kusimamia chama

Lipo tatizo na halitaondoka kwa watu kufukia vichwa kwenye mchanga.
Mwaka 2006 nikiwa kwenye mkutano Mkuu wa CHADEMA pale PTA nilitaka wajumbe wajadili kifungu kwa kifungu cha Katiba iliyokuwa inapendekezwa, lakini wajumbe wengine walishakuwa wamechoka kujadiliana.

Tatizo la CHADEMA liko kwenye utofauti kati ya dhana ya chama na jinsi chama kinavyoendeshwa. Wakati CHADEMA inaamini katika dhana ya "Decentralization" na "Devolution" Katiba yake ime-Centralize mamlaka yote ya chama kwenye Kamati Kuu.

Kwa ivo Wilaya na Majimbo hawana mamlaka ya moja kwa moja juu ya wale wanaochaguliwa katika maeneo yao. Mfumo wa kusimamia na kuratibu shughuli za wachaguliwa wa Ngazi ya Kata, Majimbo na Wilaya inasimamiwa na Kamati Kuu kupitia Ofisi za Kanda.

MTAZAMO
 
We jamaa shida yako ni moja tu: Mahaba yaliyopitiliza kwa Wilbrod Slaa. Tangu Slaa aondoke CDM umekuwa mchungu sana. Huna jema hata moja kwa chadema. I cannot take you seriously; the same way I do to MM. Punguzeni mahaba, yanapofusha.

Hoja ni nini hapa?

alichosema ni sahihi au sio sahihi??

wewe ndio una mahaba sasa!!
 
Hapo hoja yako ni mfu kaka.Unamhukumuje Nassari bila kusikiliza utetezi wake,subiri hadi kesho tutaona yale atakayozungumza maana baada ya press najua utakuja na uzi mwingine tofauti na huu na imekuwa kawaida yako kujikanyagakanyaga mwenyewe kwa hoja za kutafutiza.

suala la Nassari ni la kisheria,wewe huna a wala b kuhusu sheria.Ushatoa hukumu kwa kuangalia upande 1.hata waliojiuza kina mtolea tulisikiliza utetezi wao kwanza.

kimya ni busara,ngoja kesho tusubiri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Brother hujawahi kukata tamaa kukishauri chama hiki ukipendacho kwa dhati ya moyo wako! Sema wanazi huwa hawakuelewi.

Una point ya msingi sana! Chadema kila mtu anasauti! Mashinji is just there as a toothless dog.

Sent using Jamii Forums mobile app
una ushahidi gani kwamba chadema kila mtu ana sauti,ushawahi kupitia tweeter za akina Nape,Bashe,Makamba,kigwangwala,polepole,bashiru,uvccm na zinginezo.Kaangalie teet zao afu uone kama zinaendana na utadhani ni watu wa kutoka vyama tofauti.

chadema wabunge wake wanatimiza majukumu ya kitaifa.ndio maana wanashinda mitandaoni na wana hoja za kitaifa.Lakin ccm wao ni mapambio tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna tatizo lingine la msingi ambalo wanachama, wapenzi na wafuasi wa CHADEMA wanaona aibu kulisema hadharani, ni ATTITUDE mbovu ya viongozi na wabunge wengi wa chama hicho. Chukulia mfano wa mbunge Joseph Haule a.k.a profesa Jay, unadhani mtu kama yule ni lini atazongwa zongwa na makesi kama ya Lijuakali? Sio kwamba haongei, sio kwamba hafanyi mikutano na wananchi wake na wala sio kwamba hakosoi serikali na watawala lakini kinachomtofautisha na wenzake ni attitude yake tu. Kama kuna siku Profesa Jay atakamatwa na kupata kesi kama za hao wengine basi nitaamini kweli wapinzani wanaonewa. Tofauti na hapo CHADEMA rekebisheni mienendo yenu mibovu.

Tatizo kubwa la Chadema wamezoe siasa za hisia ,wanaamini kwenye kutukana au kufarakana na kubishana Zaidi kama njia ya kuwapatia umaarufu, sikatai lakini siasa hubadilika kulingana na mazingira na wakati, mfano;
1. Kuna haja gani ya Lijuakali kila siku yuko mahakamani? utagundua kama ulivyosema altitude.
2. Kuna haja gani ukiwa kwenye media lazima utukane? freedom of speech sio kutukana tu, chadema wengi ni wapenzi wa siasa za Kenya, je wanaweza hata wakatupatia video moja ya Raila /kalonzo /Mudavadi/akimtukana uhuru? , kuna tofauti kubwa kati ya kukosoa na kutukana, kukosoa ni kuielekeza serikali au Rais kuwa kwa hili ur wrong fanya hivi maana yake unatoa na solution.
3. Hadithi za kununuliwa, asilimia kubwa ya wabunge wao pia hawakubaliani na misimamo ya chadema, watu wanataka maendeleo wew unasema usishirikiane na serikali iliyopo a the end wananchi utawaambia nini maendeleo yakichelewa, ndio maana utaona wabunge wengi wa upinzani wanakimbia, chadema kwa kulijua hilo wanakuja na ngojera wamenunuliwa, tupe evidence hakuna.
4. Msimamo wa chadema sio maendeleo,kama mmegundua toka Magufuli aingie madarakani tumejua picha halisi ya upinzani wa Tanzania, hawako kwa ajiri ya maendeleo na kushika dola kwa miaka ijayo, wao maslahi yao ni Maisha yao. Mimi nilifikiria katika wakati huu washikamane na serikali kuleta maendeleo kama walivyo kuwa wanahubiri enzi zile ,leo wamekuwa ni watu wanapigania bunge live, wanapigania waongee kwenye tv waonekane, hivi kweli bunge live linaweza kukwamisha jitihada zako za kuwaletea wananchi maendeleo?
5. Mimi nilitoa ushauri kuwa wajitathimini kwanza wao wenyewe, wapate maoni direct ya kutoka kwa wananchi ,wawaulize kuwa hivi tukitukana, tukipigana na serikali nyie huku mnatungumzia vipi? VS tukishiriakiana na serikali katika maendeleo, tukafuata utaratibu wa kawaida wa mikutano, je wananchi watasema nin, wakipata maoni yote, watajua nini cha kufanya, lasivyo watu watakuwa wana tafuta visa kama nasari anazuga hahudhurii bunge au chochote ili wafukuzwe, maana anaona hakuna dira.
 
Wakuu,

Pamoja na lawama kwa huyo Nassari au hata Ndugai ambaye ametumia vyema sheria iliyowazi kabisa kwanini tusijiulize nafasi ya viongozi wa chama kwenye hili sakata?

Hivi kweli imefikia hatua Chadema hawafuatiliani tena mwenendo wa wabunge wao bungeni ikiwemo mahudhurio? Mbunge anakosa kuhudhuria vipindi vitatu vya bunge hadi anachukuliwa hatua na spika kabla nyie wenyewe hamjachukua hatua? What a shame!

Tukisema tatizo la Chadema ni zaidi ya CCM na dola kama kilivyo kilio cha kila siku hatueleweki! Kama kuna taasisi inayotimiza majukumu yake ya kawaida huu ujinga usingetokea.

Tumesema mara nyingi, Chadema ya sasa hakuna nidhamu, kila mtu anasharubu, kila mtu anaweza kuita press au kuandika chochote mtandaoni bila kujua kwanza party position.

Tatizo la nidhamu linakolezwa na dharau kwa katibu mkuu Mashinji. Katibu mkuu pamoja na uwezo wake mkubwa kimbinu lakini ameshindwa kusimamia chama hasa baada ya mpasuko wa 2015.

Katibu mkuu Mashinji si kiongozi mbovu bali anaongoza watu ambao wanapitia kipindi cha mpito ambacho kinaweza kuamua mustakali wa chama kama karata zisipochangwa vizuri na chama kilihitaji mtu anaweza kukemea yeyote na ikibidi hata kuchukua hatua kama ilivyowezekana ku manage crisis ya Zitto na kundi lake.

Wanachama na wapenda mabadiliko tuache kutetea ovyo uongozi uliopo kwa namna mambo yanavyoenda. Chadema ina vijana wengi walioiva ni vizuri kupewa vijiti tuanze upya. Bila mabadiliko hali hii haishushi tu morali ya wanachama bali inazidi kupenya hadi kwa viongozi waandamizi.

Tuache kauli za kutiana moyo ambazo sasa zimegeuka faraja hewa kuwa chama kitabaki hata kama viongozi wake waandamizi wakiondoka. Chama kinapoteza watu muhimu kwa namna inayohitaji tafakari na fikra huru kubaini tatizo.

Napenda kurudia rai yangu, wanaoikumbuka vizuri sana NCCR watakuwa wanaogopa hata unyasi kwa yanayoendelea Chadema. Chama kinaelekea ilipo NCCR kama mzaha! Chukueni hatua badala ya kupeana moyo hewa.

Walau Chadema zama hizi kuna mitandao kuipa uhai kidogo tofauti na enzi za Mkapa na jinsi NCCR ilivyopotezwa na kubakia jina la Mbatia kwa sasa.
Mkuu MTAZAMO nakubaliana na wewe ni kwa asilimia zote
 
Hapo hoja yako ni mfu kaka.Unamhukumuje Nassari bila kusikiliza utetezi wake,subiri hadi kesho tutaona yale atakayozungumza maana baada ya press najua utakuja na uzi mwingine tofauti na huu na imekuwa kawaida yako kujikanyagakanyaga mwenyewe kwa hoja za kutafutiza.

suala la Nassari ni la kisheria,wewe huna a wala b kuhusu sheria.Ushatoa hukumu kwa kuangalia upande 1.hata waliojiuza kina mtolea tulisikiliza utetezi wao kwanza.

kimya ni busara,ngoja kesho tusubiri.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimesikiliza maelezo ya Mbowe na maoni aliyotoa Lissu kuhusu sakata la Nassari na wote wanaonekana hawana takwimu au hawajui kama kweli mbunge wao hajahudhuria vikao vyote vitatu hadi walipopata maelezo ya Mbunge mwenyewe.

Shortly chama kipo out of touch na mwenendo wa wabunge hili tukubali na hatua za kujirekebisha zichukuliwe. Hata kuchanganyikiwa kwa wanachama wengi jana ni sababu utetezi wa Nassari ulikuwa hafifu na chama hakikuwa na records ili kutoa taarifa rasmi.

Sasa nimesikia mwenyekiti akitoa maagizo Nassari alijieleze mwenyewe. Kwa ufupi chama kinategemea taarifa ya mbunge kwa 100% lakini wao hawana records zozote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kipindi katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru anafuatilia wabunge wa CCM watoro bungeni tulichukulia juhudi hizi kishabiki na hata walioitwa kuhojiwa tukageuza kisiasa zaidi.

Tunahitaji kubadilika sana kimtizamo ili kuweza kujenga vyama vya upinzani imara.

Sent using Jamii Forums mobile app

Bila kupinga maoni yako ya post namba moja na 2, hilo bunge kibogoyo ni mtu asiye na shughuli nyingine tu anaweza kwenda kupoteza muda huko. Ni jambo gani la maana huko bungeni wanasimamia mpaka mbunge asipofika iwe tatizo? Mfano toka Profesa Muhongo kapoteza uwaziri umewahi kumuona akichangia chochote? Sio yeye tu, fuatilia wabunge wengi, karibu 50% huwa hawana mchango wowote zaidi ya kufuata posho. Kazi yao kubwa ni kwenda kujaza vyoo na kuwinda posho.
,
Siungi mkono Nasari kutokuhudhuria vikao vyoye vya bunge lakini ni kipi kimekwama jimboni kwake kwakuwa haendi bungeni? Hilo bunge zaidi ya kumsifia na kupitisha atakacho Magufuli kuna kipi cha maana ambacho kinamngoja Nasari?
 
Mkuu hata kufatilia mwenendo wa wabunge ikiwemo mahudhurio tunaleta excuse kama hizi? Kesho ukisikia kuna ubadhirifu Chadema si bado tutakuja na ngonjera hizi? Tunahitaji kubadilika, lipo tatizo zito!

Sent using Jamii Forums mobile app

Unamfuatilia mtu anayetishiwa uhai wake? Ni lini ulikemea udhalimu wa dola dhidi ya cdm mpaka ushangae leo hali ilipofikia? Hali hii iliyopo inakufurahisha kwani chama kimefikia ulipotaka. Fanya sherehe kwani matamanio yako yametimia
 
Kuna tatizo lingine la msingi ambalo wanachama, wapenzi na wafuasi wa CHADEMA wanaona aibu kulisema hadharani, ni ATTITUDE mbovu ya viongozi na wabunge wengi wa chama hicho. Chukulia mfano wa mbunge Joseph Haule a.k.a profesa Jay, unadhani mtu kama yule ni lini atazongwa zongwa na makesi kama ya Lijuakali? Sio kwamba haongei, sio kwamba hafanyi mikutano na wananchi wake na wala sio kwamba hakosoi serikali na watawala lakini kinachomtofautisha na wenzake ni attitude yake tu. Kama kuna siku Profesa Jay atakamatwa na kupata kesi kama za hao wengine basi nitaamini kweli wapinzani wanaonewa. Tofauti na hapo CHADEMA rekebisheni mienendo yenu mibovu.

Mkuu unadhani hatuoni mwenendo uliopo? Unataka kuniambia ukikamatwa hiyo inamaanisha haifuati sheria?
 
Nimesikiliza maelezo ya Mbowe na maoni aliyotoa Lissu kuhusu sakata la Nassari na wote wanaonekana hawana takwimu au hawajui kama kweli mbunge wao hajahudhuria vikao vyote vitatu hadi walipopata maelezo ya Mbunge mwenyewe.

Shortly chama kipo out of touch na mwenendo wa wabunge hili tukubali na hatua za kujirekebisha zichukuliwe. Hata kuchanganyikiwa kwa wanachama wengi jana ni sababu utetezi wa Nassari ulikuwa hafifu na chama hakikuwa na records ili kutoa taarifa rasmi.

Sasa nimesikia mwenyekiti akitoa maagizo Nassari alijieleze mwenyewe. Kwa ufupi chama kinategemea taarifa ya mbunge kwa 100% lakini wao hawana records zozote.

Sent using Jamii Forums mobile app
uko sahihi kwamba kuna udhaifu hilo halipingiki lakin tusimhukumu nassari mpaka pale ambapo kesho atatoa maelezo yenye kina.Muda utaamua kaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kipindi katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru anafuatilia wabunge wa CCM watoro bungeni tulichukulia juhudi hizi kishabiki na hata walioitwa kuhojiwa tukageuza kisiasa zaidi.

Tunahitaji kubadilika sana kimtizamo ili kuweza kujenga vyama vya upinzani imara.

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha dogo atumie pesa ya kodi. Angeacha kwa kusema anamuunga mkono mzee baba mngeng'amua kitu, lakini kwa staili hii hakuna atakaegundua kitu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu si ndio raha kwa ccm? Kwani hata walipokuwa wanafanyiwa ukatili na kuporwa kura ulitoa maoni yoyote kukemea uhuni ule?

Ni jukumu lao kusearch na kuona niliisema nini..mambo mengine siyo uhuni... upinzani kweli kabisa unaamini unafanyiwa "uhuni" na bado wanaitwa wapinzania?
 
Ni jukumu lao kusearch na kuona niliisema nini..mambo mengine siyo uhuni... upinzani kweli kabisa unaamini unafanyiwa "uhuni" na bado wanaitwa wapinzania?

Kama kuna chochote ulihoji kuhusu huo uhuni ni kabla ya Magufuli kuingia madarakani. Baada ya hapo uhuni wowote waliofanyiwa wapinzani uliona ni stahiki kisa walimpokea Lowassa.
 
Ni kweli kabisa ndio maana tunazuia mikutano ya ndani pamoja ya wazi, halafu viongozi wa upinzani tunawambakia kesi na kuwanyima dhamana ili wasipate muda kuongoza vyama vyao, ma tunasubiri uchaguzi uje tuibe kura tena na kupora ushindi maana viongozi wa upinzani wameshindwa kuongoza, uko sahihi kada mwenzagu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna uhusiano gani wa ulichoandika na uzembe wa kuvuliwa ubunge kwa nassari?
 
Kabla ya kuilamu CHADEMA na uongozi wake tujikumbushe wanayopitia viongozi na wabunge wake katika zama hizi za utawala wa awamu ya tano ya CCM.

Mnadhimu mkuu wa CHADEMA kamanda Tundu Lissu yupo ktk matibabu baada ya kushambuliwa na watu wanaosemekana hawajulikani.

Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe alikuwa rumande kwa miezi kadhaa. Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Mashinji, Wabunge wengi wa CHADEMA na madiwani wao wamefunguliwa kesi nyingi mahakamani na kutakiwa kuripoti Polisi mara kwa mara.

Edward Lowassa aliyekuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha CHADEMA pia alikuwa ameandamwa kwa kesi nyingi kabla ya kukimbilia CCM.

Halafu wanatokea watanzania wasaulifu kushindwa kubaini, kutambua na kuona njama zote hizo hapo juu kuififisha CHADEMA kisiasa, kwa Chama cha CCM kutumia njia haramu.


Itakuwa ni aibu kina ' MTAZAMO ' kuja na hoja dhaifu kuielekezea kidole CHADEMA kuwa ni taasisi dhaifu wakati ilitakiwa wao kina MTAZAMO kukemea kwa kupaza sauti tabia ya CCM kutumia kila njia haramu kuvidhoofisha vyama vya CHADEMA na CUF.
Lugora apiga marufuku mikutano ya ndani:

Hali hii ya CCM na serikali yake kuvisakama vyama vingine vya siasa Tanzania siyo nzuri kwa taifa letu lenye katiba ya kidemokrasia na hamu ya kuwa na nchi ya amani na utulivu.

Je hii ndio sababu Nassari hajawa bungeni vikao vitatu?
Yaani mnasikitisha mpaka mnashindwa kutengeneza stori ya kusapoti huu ujinga.
 
Back
Top Bottom