Wakuu,
Pamoja na lawama kwa huyo Nassari au hata Ndugai ambaye ametumia vyema sheria iliyowazi kabisa kwanini tusijiulize nafasi ya viongozi wa chama kwenye hili sakata?
Hivi kweli imefikia hatua Chadema hawafuatiliani tena mwenendo wa wabunge wao bungeni ikiwemo mahudhurio? Mbunge anakosa kuhudhuria vipindi vitatu vya bunge hadi anachukuliwa hatua na spika kabla nyie wenyewe hamjachukua hatua? What a shame!
Tukisema tatizo la Chadema ni zaidi ya CCM na dola kama kilivyo kilio cha kila siku hatueleweki! Kama kuna taasisi inayotimiza majukumu yake ya kawaida huu ujinga usingetokea.
Tumesema mara nyingi, Chadema ya sasa hakuna nidhamu, kila mtu anasharubu, kila mtu anaweza kuita press au kuandika chochote mtandaoni bila kujua kwanza party position.
Tatizo la nidhamu linakolezwa na dharau kwa katibu mkuu Mashinji. Katibu mkuu pamoja na uwezo wake mkubwa kimbinu lakini ameshindwa kusimamia chama hasa baada ya mpasuko wa 2015.
Katibu mkuu Mashinji si kiongozi mbovu bali anaongoza watu ambao wanapitia kipindi cha mpito ambacho kinaweza kuamua mustakali wa chama kama karata zisipochangwa vizuri na chama kilihitaji mtu anaweza kukemea yeyote na ikibidi hata kuchukua hatua kama ilivyowezekana ku manage crisis ya Zitto na kundi lake.
Wanachama na wapenda mabadiliko tuache kutetea ovyo uongozi uliopo kwa namna mambo yanavyoenda. Chadema ina vijana wengi walioiva ni vizuri kupewa vijiti tuanze upya. Bila mabadiliko hali hii haishushi tu morali ya wanachama bali inazidi kupenya hadi kwa viongozi waandamizi.
Tuache kauli za kutiana moyo ambazo sasa zimegeuka faraja hewa kuwa chama kitabaki hata kama viongozi wake waandamizi wakiondoka. Chama kinapoteza watu muhimu kwa namna inayohitaji tafakari na fikra huru kubaini tatizo.
Napenda kurudia rai yangu, wanaoikumbuka vizuri sana NCCR watakuwa wanaogopa hata unyasi kwa yanayoendelea Chadema. Chama kinaelekea ilipo NCCR kama mzaha! Chukueni hatua badala ya kupeana moyo hewa.
Walau Chadema zama hizi kuna mitandao kuipa uhai kidogo tofauti na enzi za Mkapa na jinsi NCCR ilivyopotezwa na kubakia jina la Mbatia kwa sasa.