Satoh Hirosh
JF-Expert Member
- Mar 30, 2021
- 5,950
- 23,264
Ni Jambo la huzuni sana.
Jana tupo kazini mida ya saa nane mchana mara jamaa akapokea simu kutoka nyumbani,taarifa haikuwa nzuri Mara ghafla akaanza kulia. Tulipomuuliza nini tatizo akasema amepata taarifa mwanae ameng'atwa na nyoka porini kwa hiyo amekutwa amefariki. Ni binti wa kike anasoma darasa la tatu huko mkoani Mtwara.
Baada ya kupata taarifa hiyo mbaya tukafanya maandalizi,akasinidikizwa nyumbani ili akajiandae kwenda mkoani Mtwara kumzika mwanae.
Usiku saa 5 akanipigia simu kwamba walipopeleka mwili wa marehemu hospitali ya mkoa,ripoti ya daktari ilisema binti hakung'atwa na nyoka Kama walivyodhani,bali alibakwa Kisha akavyunjwa shingo na kutelekezwa porini.
Watu waliopeleka mwili hospitali walisema shingo ilikuwa imelegea sana kuliko kawaida. Na nadhani ripoti ya mchana ya kung'atwa na nyoka ilisambaa kwa sababu mwili uliokotwa porini, wakaamua kujiongeza kwa kudhani ni nyoka ndiye alimsababishia mauti binti mdogo.
Inasikitisha sana binti mdogo ambaye hawezi hata kujitetea kwa lolote unamfanyia ukatili na kumwondolea uhai,tena kwa kumvunja shingo..dah!
Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
Jana tupo kazini mida ya saa nane mchana mara jamaa akapokea simu kutoka nyumbani,taarifa haikuwa nzuri Mara ghafla akaanza kulia. Tulipomuuliza nini tatizo akasema amepata taarifa mwanae ameng'atwa na nyoka porini kwa hiyo amekutwa amefariki. Ni binti wa kike anasoma darasa la tatu huko mkoani Mtwara.
Baada ya kupata taarifa hiyo mbaya tukafanya maandalizi,akasinidikizwa nyumbani ili akajiandae kwenda mkoani Mtwara kumzika mwanae.
Usiku saa 5 akanipigia simu kwamba walipopeleka mwili wa marehemu hospitali ya mkoa,ripoti ya daktari ilisema binti hakung'atwa na nyoka Kama walivyodhani,bali alibakwa Kisha akavyunjwa shingo na kutelekezwa porini.
Watu waliopeleka mwili hospitali walisema shingo ilikuwa imelegea sana kuliko kawaida. Na nadhani ripoti ya mchana ya kung'atwa na nyoka ilisambaa kwa sababu mwili uliokotwa porini, wakaamua kujiongeza kwa kudhani ni nyoka ndiye alimsababishia mauti binti mdogo.
Inasikitisha sana binti mdogo ambaye hawezi hata kujitetea kwa lolote unamfanyia ukatili na kumwondolea uhai,tena kwa kumvunja shingo..dah!
Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app