Unya unaofanywa na wafugaji dhidi ya wakulima mkoani Morogoro

kunguni wa ulaya

JF-Expert Member
Mar 16, 2014
4,132
6,100
TAARIFA YA KUSIKITISHA KUTOKA KATA YA MASANZE JIMBO LA MIKUMI.

OFISI YA MBUNGE Jimbo La Mikumi inalaani sana kitendo cha kinyama kilichofanywa na Ndugu zetu wa jamii ya wafugaji kwa kujichukulia sheria mkononi na kumjeruhi vibaya Ndugu Augustino Mtitu mkulima wa kitongoji cha Upangwani, Kijiji cha Dodoma Isanga, Kata Ya Masanze Jimbo la Mikumi ambapo leo tarehe 25 desemba majira ya Mchana amechomwa mkuki mdomoni na kutokezea nyuma ya shingo yake, ambapo alipelekwa hospitali ya wilayani Kilosa na baadae amekimbizwa hospitali ya mkoa MOROGORO ili kufanyiwa operesheni ya kuondoa mkuki huo na kwa matibabu zaidi.
AUGUSTINO MTITU alishambuliwa na wafugaji wa kimasai alipokuwa akimsaidia jirani yake kufukuza Ng'ombe wasiharibu mazao shambani kwake,
Kipande cha mti kinachoonekana hapo mdomoni ndiyo mkuki uliokatwa ili kupunguza urefu wa mkuki huo wakati wakimkimbiza hospitali, Inasemekana MwenyeKiti wa kijiji na MwenyeKiti wa kitongoji hicho nao wamejeruhiwa.

WITO KWA SERIKALI.
Ofisi Ya Mbunge Mikumi inatoa wito kwa Serikali kuwabaini wale wote waliofanya kitendo hiki cha kinyama kuhakikisha wanachukuliwa hatua kali za kisheria ili kuweza kukomesha vitendo hivi vya kujichukulia sheria mkononi inayopelekea kuongezeka kwa uvunjifu mkubwa wa Amani na migogoro isiyokwisha kati ya wakulima na wafugaji wilayani KILOSA.

Imetolewa na:-
Robert A. Galamona
Katibu Ofisi Ya Mbunge
Mikumi.

Chanzo-Face book akaunti ya Profesa J.

Picha zipo hapo chini.
 
TAARIFA YA KUSIKITISHA KUTOKA KATA YA MASANZE JIMBO LA MIKUMI.

OFISI YA MBUNGE Jimbo La Mikumi inalaani sana kitendo cha kinyama kilichofanywa na Ndugu zetu wa jamii ya wafugaji kwa kujichukulia sheria mkononi na kumjeruhi vibaya Ndugu Augustino Mtitu mkulima wa kitongoji cha Upangwani, Kijiji cha Dodoma Isanga, Kata Ya Masanze Jimbo la Mikumi ambapo leo tarehe 25 desemba majira ya Mchana amechomwa mkuki mdomoni na kutokezea nyuma ya shingo yake, ambapo alipelekwa hospitali ya wilayani Kilosa na baadae amekimbizwa hospitali ya mkoa MOROGORO ili kufanyiwa operesheni ya kuondoa mkuki huo na kwa matibabu zaidi.
AUGUSTINO MTITU alishambuliwa na wafugaji wa kimasai alipokuwa akimsaidia jirani yake kufukuza Ng'ombe wasiharibu mazao shambani kwake,
Kipande cha mti kinachoonekana hapo mdomoni ndiyo mkuki uliokatwa ili kupunguza urefu wa mkuki huo wakati wakimkimbiza hospitali, Inasemekana MwenyeKiti wa kijiji na MwenyeKiti wa kitongoji hicho nao wamejeruhiwa.

WITO KWA SERIKALI.
Ofisi Ya Mbunge Mikumi inatoa wito kwa Serikali kuwabaini wale wote waliofanya kitendo hiki cha kinyama kuhakikisha wanachukuliwa hatua kali za kisheria ili kuweza kukomesha vitendo hivi vya kujichukulia sheria mkononi inayopelekea kuongezeka kwa uvunjifu mkubwa wa Amani na migogoro isiyokwisha kati ya wakulima na wafugaji wilayani KILOSA.

Imetolewa na:-
Robert A. Galamona
Katibu Ofisi Ya Mbunge
Mikumi.

Chanzo-Facebook akaunti ya Profesa J.
1482691569375.jpg
1482691576424.jpg
 
TAARIFA YA KUSIKITISHA KUTOKA KATA YA MASANZE JIMBO LA MIKUMI.

OFISI YA MBUNGE Jimbo La Mikumi inalaani sana kitendo cha kinyama kilichofanywa na Ndugu zetu wa jamii ya wafugaji kwa kujichukulia sheria mkononi na kumjeruhi vibaya Ndugu Augustino Mtitu mkulima wa kitongoji cha Upangwani, Kijiji cha Dodoma Isanga, Kata Ya Masanze Jimbo la Mikumi ambapo leo tarehe 25 desemba majira ya Mchana amechomwa mkuki mdomoni na kutokezea nyuma ya shingo yake, ambapo alipelekwa hospitali ya wilayani Kilosa na baadae amekimbizwa hospitali ya mkoa MOROGORO ili kufanyiwa operesheni ya kuondoa mkuki huo na kwa matibabu zaidi.
AUGUSTINO MTITU alishambuliwa na wafugaji wa kimasai alipokuwa akimsaidia jirani yake kufukuza Ng'ombe wasiharibu mazao shambani kwake,
Kipande cha mti kinachoonekana hapo mdomoni ndiyo mkuki uliokatwa ili kupunguza urefu wa mkuki huo wakati wakimkimbiza hospitali, Inasemekana MwenyeKiti wa kijiji na MwenyeKiti wa kitongoji hicho nao wamejeruhiwa.

WITO KWA SERIKALI.
Ofisi Ya Mbunge Mikumi inatoa wito kwa Serikali kuwabaini wale wote waliofanya kitendo hiki cha kinyama kuhakikisha wanachukuliwa hatua kali za kisheria ili kuweza kukomesha vitendo hivi vya kujichukulia sheria mkononi inayopelekea kuongezeka kwa uvunjifu mkubwa wa Amani na migogoro isiyokwisha kati ya wakulima na wafugaji wilayani KILOSA.

Imetolewa na:-
Robert A. Galamona
Katibu Ofisi Ya Mbunge
Mikumi.

Chanzo-Fesibuku akaunti ya Profesa J.
Hayo ni matendo yanayojirudia katika eneo hilo hadi wananchi wanakosa imani Na serikali yao mh. Mbunge ashauri serikali itafute suluhisho la kudumu
 
Poleni sana MUNGU amponye,,ila jitahid kuandika vizuri hakuna kitu kinachoitwa fesibuku isitoshe wewe ni katibu wa mbunge
 
Duu unyama huu haupaswi kufumbiwa macho, waliohusika wote sheria ichukue mkondo wake
 
Tuweke kumbukumbu ya picha hizi za kusikitisha, nina imani iko siku atakuja mburula ataziweka na kichwa cha habari....... MKE WA MTU SUMU.
 
Watu wengi wamefunga shughuli za kilimo morogoro hasa kilosa kwa sababu ya wagugaji korofi.
Kilosa kuna Mito,Mabwawa,Maji ardhini,Mbuga za wanyama, Madini,Ardhi bikra,Miti ya mbao, Vyuo na taasisi za kilimo. Kama kilosa ingekuwa ni nchi ingekuwa zaidi ya uswizi.

Serikali ifanye kitu hili liishe yaani baraka ya mifugo isijekuwa laana kwa kilimo.
 
Wafugaji wanazidi kutawala aisee hapa Tanzania. Hakuna hata mtu mmoja anayeweza kushindana nao. Mkienda polisi hupati msaada mahakamani nako hovyo,ukisema upambane nao madhara yake nayo yanakua makubwa..aisee tunaelekea kubaya kabisa kuhusu amani ya nchi.
 
Elimu inaitajika sana kwa wamasai bila ivyo hukombeleni naona tatizo litazidi serikali iwape Elimu kuhusiana na kufuga mifugo michache wanayoweza kuipatia malisho inasikitisha sana kwakweli
 
aisee hali inazid kuwa mbaya sana. hiii migogoro ya wakulima na wafugaji haijapewa attention ya kutosha na kwa namna hii wengi wataumia sana.
 
Back
Top Bottom