Untold treasures: Mkoa wa Lindi na vivutio vya utalii.

Ahmet

JF-Expert Member
Oct 15, 2019
1,537
3,404
Habari za muda huu wapendwa, natumai Kila mtu ni mzima.

Acha leo niwaonyeshe uzuri wa mkoa wa Lindi, mkoa uliopo kusini mwa Tanzania. Watu wengi hasa kutoka kasikazini, magharibi au hata Kanda ya kati wanaweza wasiufahamu vizuri mkoa huu. Si ajabu mtu akakuambia hajui kama Lindi ni mkoa. Baadhi wanadhani ni miongoni mwa wilaya za mkoa wa Mtwara.

Mkoa wa Lindi ni watatu kwa ukubwa Tanzania kwani una kilomita za mraba 66040. Ukubwa wa mkoa huu ni asilimia 7.1 ya ukubwa wa Tanzania. Mkoa huu mkubwa umejawa rasilimali na vivutio vingi vyenye kustaajabisha na kupendeza machoni mwa wengi.

Basi bila kupoteza muda acha niwatembeze katika baadhi ya sehemu ambazo ni za kuvutia zipatikanazo mkoani Lindi.

1. Tendaguru formation, hapa ndipo yalipogunduliwa mabaki ya mjusi mkubwa ambayo yalichukuliwa na wajerumani (Dinosaurs). Picha ya chini ni mabaki ya mjusi huyo huko nchini Urejumani.

images (9).jpeg

images (11).jpeg

2. Magofu ya kilwa na Historia yake, dola ya Mrima, Kilwa ilikuwa na fedha yake. Magofu haya ni yenye kupendeza na huvutia watu mbalimbali kuja kuyatazma.
images (26).jpeg

images (35).jpeg

3. Selous game reserve, ni pori kubwa mno na wanyamwa wengi wapo hapa.
images (39).jpeg

images (55).jpeg

4. Fukwe za bahari ya Lindi, ni zenye kuvutia kwelikweli. Fukwe hizi zimepambwa na mchanga mweupe na miti mingi ya minazi pembezoni.
images (46).jpeg

images (45).jpeg

5. Cradle of Majimaji, mnara wa Nandete Kilwa ndio mahali ambapo Vita vikubwa kabisa vya Majimaji vilianza
images (48).jpeg

6. Mazao Kama korosho, ufuta, miogo, mtama na vyakula vya bahari kama pweza, ngisi, uduvi n.k. vinapatikana kwa wingi mkoani Lindi.
images (43).jpeg

images (59).jpeg

7. Visiwa vizuri vyenye maajabu na Historia nzuri. Mkoa wa Lindi una visiwa vingi vinavyopatikana katika bahari ya Hindi, Sanje ya Kati, Songo mnara, Songo songo, Fanjove private island, Kilwa kisiwani ni baadhi tu kati ya visiwa vilivyopo mkoani Lindi.
images (47).jpeg

images (52).jpeg

8. Uwepo wa gesi asilia chini ya bahari, gesi iliyogunduliwa karibu na pwani ya manispaa ya Lindi inatajwa kuwa ndio nyingi zaidi kuliko ile ya Mtwara. Gesi asilia pia inapatikana katika wilaya ya Kilwa ambayo inachangia megawatt nyingi katika grid ya taifa.
images (44).jpeg


Hakika Lindi ni pazuri, karibu Lindi.
 
Habari za muda huu wapendwa, natumai Kila mtu ni mzima.

Acha leo niwaonyeshe uzuri wa mkoa wa Lindi, mkoa uliopo kusini mwa Tanzania. Watu wengi hasa kutoka kasikazini, magharibi au hata Kanda ya kati wanaweza wasiufahamu vizuri mkoa huu. Si ajabu mtu akakuambia hajui kama Lindi ni mkoa. Baadhi wanadhani ni miongoni mwa wilaya za mkoa wa mtwara.

Mkoa wa Lindi ni watatu kwa ukubwa Tanzania kwani una kilomita za mraba 66040. Ukubwa wa mkoa huu ni asilimia 7.1 ya ukubwa wa Tanzania. Mkoa huu mkubwa umejawa rasilimali na vivutio vingi vyenye kustaajabisha na kupendeza machoni mwa wengi.

Basi bila kupoteza muda acha niwatembeze katika baadhi ya sehemu ambazo ni za kuvutia zipatikanazo mkoani Lindi.

1. Tendaguru formation, hapa ndipo yalipogunduliwa mabaki ya mjusi mkubwa ambayo yalichukuliwa na wajerumani (Dinosaurs). Picha ya chini ni mabaki ya mjusi huko nchini Urejumani.

View attachment 2200460
View attachment 2200468
2. Magofu ya kilwa na Historia yake, dola ya Mrima, kilwa ilikuwa na fedha yake. Magofu haya ni yenye kupendeza na huvutia watu mbalimbali kuja kuyatazma.
View attachment 2200471
View attachment 2200473
3. Selous game reserve, ni pori kubwa mno na wanyamwa wengi wapo hapa.
View attachment 2200483
View attachment 2200484
4. Fukwe za bahari ya Lindi, ni zenye kuvutia kwelikweli. Fukwe hizi zimepambwa na mchanga mweupe na miti mingi ya minazi pembezoni.
View attachment 2200485
View attachment 2200486
5. Cradle of Majimaji, mnara wa Nandete Kilwa ndio mahali ambapo Vita vikubwa kabisa vya Majimaji vilianza
View attachment 2200488
6. Mazao Kama korosho, ufuta, miogo, mtama na vyakula vya bahari kama pweza, ngisi, uduvi n.k. vinapatikana kwa wingi mkoani Lindi.
View attachment 2200491
View attachment 2200493
7. Visiwa vizuri vyenye maajabu na Historia nzuri. Mkoa wa Lindi una visiwa vingi vinavyopatikana katika bahari ya Hindi, Sanje ya Kati, Songo mnara, Songo songo, fanjove private island, kilwa kisiwani ni baadhi tu kati ya visiwa vilivyopo mkoani Lindi.
View attachment 2200494
View attachment 2200497
8. Uwepo wa gesi asilia chini ya bahari, gesi iliyogunduliwa karibu na pwani ya manispaa ya Lindi inatajwa kuwa ndio nyingi zaidi kuliko ile ya Mtwara. Gesi asilia pia inapatikana katika wilaya ya Kilwa ambayo inachangia megawatt nyingi katika grid ya taifa.
View attachment 2200499

Hakika Lindi ni pazuri, karibu Lindi.
Namiss samaki na pweza uwanja wa fisi, starehe zote zimewekwa eneo moja, Shanta Shanta za kumwaga, goli la nguo kali mtumba pale 77 container, kuna mgahawa karibu na shirton lodge wako vizuri, lami ya Lindi, Lindi shimoni Paris of Africa, kitovu cha starehe, Amazing Lindi,
 
Namiss samaki na pweza uwanja wa fisi, starehe zote zimewekwa eneo moja, Shanta Shanta za kumwaga, goli la nguo kali mtumba pale 77 container, kuna mgahawa karibu na shirton lodge wako vizuri, lami ya Lindi, Lindi shimoni Paris of Africa, kitovu cha starehe, Amazing Lindi,
Aisee sehemu zetu za kujidai hizo
 
Back
Top Bottom