Ungekuwa rais ungefanya nini?

Mbona rahisi tu! ningetunga safari niende nje ya nchi maana najua huu ni upepo tu utapita!
 
Kha, mbona watu wanaenda mbali sana?!? Kufanyaje kote huko, mbona jambo liko straight Wala halina kona hili.. Inshu inayopigiwa kelele hapa Na kunyofoa roho Za watu ni Nini? Sio ngoma, SIO mpira, sio machinga, sio harusi Mradi Wa Bomba la Gesi, hayo mengine nani kakosea, nani kakwiba, nani kaonewa, nani afukuzwe ni ya baadae sana, tamko la haraka sana Kwa sasa ni Mwenye Nyumba ya Nchi Kutangaza Kusitisha Mradi huo haraka. Na IKIWEZEKANA KUUFUTA KABISA.. !! Hayo mengine yatafuata baadae sana.. Mie nashangaa mpaka sasa jamaa yuko muted tu.. Kiasi Gani Raisi wetu Hana huruma Na raia wake. Kweli baba gani Wa Nyumba unamwona mbwa anatafuna Watoto wewe badala ya kumtimua mbwa unakimbilia kumsaka mwenye mbwa hiyo hii ni ajabu. Mkuu wa Nchi akisema Mradi ameusitisha jazba otapoa Na Amani itarejea faster.. Mbona kitu ndogo sana hii..
 
Toa mchango wako wa nini ungefanya kuhusu nchi yetu ya TANZANIA ili mambo yawe murua.
 
Nitakua MZALENDO,kisha NITAUA hadharani wanaokula rushwa,ufisadi.WATU wote kufanya kazi za uzalishaji kuanzia ngazi ya familia
 
Toa mchango wako wa nini ungefanya kuhusu nchi yetu ya TANZANIA ili mambo yawe murua.
Kwanza kabisa ni vyema swali hilo ukajiuliza mwenyewe kabla ya kuwauliza wenzako. Je kwa sasa unaifanyia nini nchi yako?
 
Ningewa-confirm makaimu katibu wote wa wizara ili wafanye kazi bila woga na kuwaondoa wale ambao wameshindwa kazi katika kipindi chote cha kukaimu.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Ningekuwa Raisi
1.badala ya kujinadi majukwaani kukerwa na milipuko ningeunda tume ya kimahakama kuchunguza wahusika.
2.ningeunda tume ya usuruhishi haswa kuhusu watuhumiwa wa ufisadi,watumiaji madaraka vibaya ili kama ni kurudisha pesa walizo iba au kodi zilipwe maana hawa ndio wanao hujumu mipango yote yenye tija kwa Taifa na kutunga mikataba yenye maslahi binafsi.
3.kipindi hiki cha mchakato wa Katiba ningevunja serikali ya chama Tawala nikaunda serikali ya mpito(sio mseto wa vyama) ili kusimamia katiba bila kutafuta maslahi ya chama chochote kile ili baada ya ya kukamilika serikali ijayo ifuate katiba mpya kwa maslahi ya nchi na sio chama.
Toa mchango wako wa nini ungefanya kuhusu nchi yetu ya TANZANIA ili mambo yawe murua.
 
Mi kama ningekuwa rais
1. Ningetokomeza mbu, mende, sisimizi na nzi wooote Tanzania.
2. Ningeondoa foleni Dar kwa kujenga barabara za juu ili watu wapige kazi murua
3. Ningeifanya treni kuwa chombo cha Usafiri mkuu Tanzania.
4. Fisadi yeyote ningemchinja hadharani.
5. Ningefanya utu uonekane ni wa thamani kuliko pesa.
6. Ningefuta jeshi la polisi
7. Ningeifanya pesa yetu iwe na nguvu kuliko dola.
8. Ningehamishia wizara zote mikoani.
9. Kilimo ndo kingekuwa moyo wa Taifa.
10. Ningeondoa kodi zote na kuongeza kodi ktk sekta ya madini ili watanzania wooote wafaidike nayo.
Nawasilisha.
Ni mimi Rais asiye
F I S A D I - baba RiTzI 2.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom