Unga wa sembe kg 1 sasa ni tsh 1500/1600

Unga wa sembe kg 1 sasa ni tsh 1500/1600

Wacha ipande wakulima na wafanya biashara wa mahindi wanufaike.
 
we bado unakula sembe!!! wenzako tumesharudi dona na bei tumekuta pungufu maradufu. Tatizo lako umeng'ang'ania ulimwengu wa malaika, rudi kwenu mkuu.
 
"Mimi nahisi kuna Wakulima wanaficha mahindi kwa makusudi ili kumkomoa Rais wetu"
Makada watakuja na kauli hizo.
 
Wachumi wanaweza kutusaidia hapa, hivi inakuaje hapa? Nchi yetu inasifika sana kwa uzalishaji wa nafaka ya mahindi ukanda huu wa Afrika mashariki kuliko hata mchele, lakini bei ya kilo moja tu ya unga wa mahindi inakimbizana na bei ya kilo ya mchele.


Kinachonishangaza ni kitu kimoja, mzunguko wa pesa sio mzuri lakini pamoja na upatikanaji wa pesa kua mgumu lakini bado thamani ya shilingi haijapanda zaidi inashuka. Sasa kuna uhusiano gani kati ya kupanda kwa thamani ya shilingi na kuadimika kwa shilingi? Kuadimika kwa shilingi kunaweza kua suluhisho la kushuku kwa thamani yake?
 
Kwakweli hili limenishangaza kwa miaka mingi sikuwahi kusikia ubwabwa na ugali kulingana bei ila sasa naona ngoma droo, sasa sijui ni wakulima wa mahindi wamepunguza uzalishaji au mchele ndo umeshuka bei.
 
Mimi nauza 1600 , lazima tuelewane mwaka huuu
 
Mimi niko tegeta nauza 1kg shilingi 1500 being ya Unga Kule Mashine imekuwa juu sana na haiko stable inabadilika kila baada ya Siku mbili au tatu
 
nipo kweenye dieti nakula matunda tu na mboga mboga kwa kweli sijui mchele wala unga
 
mh bk jero ni hatali unga wa muhogo,mtama na wa ulezi unahitajika kwa sasa...
 
Mkuu nina miezi kibao nanunua mahindi ya kusaga dona kilo 1 Tsh 1500 kama ni 1400 basi imepungua.
 
Alafu kale kawimbo maarufu kale..lazima kashike nafasi ya kwanza mwaka huu 2016.
[emoji445] [emoji444] [emoji443] [emoji448] [emoji449] [emoji447] [emoji441]
 
Back
Top Bottom