Unazungumzia CCM ipi?

Kalamu

JF-Expert Member
Nov 26, 2006
7,458
8,521
CCM kimekuwa chama chenye milengo mbalimbali (rangi nyingi), na kwa maoni yangu hii ni sababu mojawapo inayofanya vyama vya upinzani wapate taabu sana kukikabiri barabara chama hiki na kukiondoa kwenye madaraka.

Ni hoja yangu kwamba, ni ndani ya CCM hiyo hiyo kwa kuwa na makundi mbalimbali, yenye milengo mbalimbali kiasi kwamba hivi vyama vya upinzani vilivyoko nje ya chama hicho, mahitaji yao (wenzao wenye milengo kama wao) tayari wamo ndani ya CCM.

Kwa hiyo, kwa chama kama CHADEMA, walipata taabu sana toka kwa kundi lililo upande wa Magufuli, huku wenzao waliomo ndani ya chama hicho, kutokana na muundo wa chama, hawakuweza kuinua kidole na kuwatetea CHADEMA.
Baada ya Magufuli kuondoka, kama alivyoondoka, na kundi lililokuwa limenyamaza likiwa upande wa akina Samia, sasa ndio wanaotawala anga. Kundi hili ni kundi lenye misimamo inayokubaliana karibu kwa kila kitu na CHADEMA, kasoro kuwaachia washike serikali. CHADEMA imejikuta haina wigo wa kumkabiri Samia, ambaye naye hatumii njia zilezile za kuwakandamiza kama alizotumia Magufuli.

Kwa hali hii, ni ajenda gani wanayoweza kuishika na kumkabiri nayo Samia? Ukandamizaji hakuna, Katiba Mpya, inazungumzika, Tume Huru, hili tutalifanyia kazi. Sasa CHADEMA imebaki na kitu gani kuwapelekea wananchi wawaunge mkono!

Mbowe kautazama ukweli huu, na kuamua kama alivyo amua ni nini chama chake kifanye.

Wakati huo huo, huko ndani ya CCM vikelele vya kundi la Magufuli linatafutiwa dawa. Kamati Kuu na Kamati mhimu zinasukwa upya kuondoa takataka za Magufuli huko. Hawa wanaopiga kelele pembeni, wakati wakiwa ndani ya chama, wengi wanatupiwa minofu, na wale ambao ni sugu kama akina Polex2, akina Bashiru, akina Kalamaganda wote wamekwishawekwa pembeni.

Hiyo ndiyo CCM, ambayo, kwa rangi zake mabalimbali na uwezo wa kujigeuza kila mara, imeapa" kutawala nchi hii milele"! Kweli?

Kama vyama vyote vya upinzani tayari wanayo makundi yao ndani ya CCM, yako wapi tena matumaini ya waTanzania?

Kwa mwendo huu huu, kuna siku tutajikuta akina Thomas Sankara wakiibuka bila ya kutegemewa. Hilo ndilo litakaloiondoa CCM na makundi yake yote, ndani na nje ya chama.

Sikuhariri chochote, naomba usinilaumu kwa makosa ya uandishi.
 
CCM kimekuwa chama chenye milengo mbalimbali (rangi nyingi), na kwa maoni yangu hii ni sababu mojawapo inayofanya vyama vya upinzani wapate taabu sana kukikabiri barabara chama hiki na kukiondoa kwenye madaraka.

Ni hoja yangu kwamba, ni ndani ya CCM hiyo hiyo kwa kuwa na makundi mbalimbali, yenye milengo mbalimbali kiasi kwamba hivi vyama vya upinzani vilivyoko nje ya chama hicho, mahitaji yao (wenzao wenye milengo kama wao) tayari wamo ndani ya CCM.

Kwa hiyo, kwa chama kama CHADEMA, walipata taabu sana toka kwa kundi lililo upande wa Magufuli, huku wenzao waliomo ndani ya chama hicho, kutokana na muundo wa chama, hawakuweza kuinua kidole na kuwatetea CHADEMA.
Baada ya Magufuli kuondoka, kama alivyoondoka, na kundi lililokuwa limenyamaza likiwa upande wa akina Samia, sasa ndio wanaotawala anga. Kundi hili ni kundi lenye misimamo inayokubaliana karibu kwa kila kitu na CHADEMA, kasoro kuwaachia washike serikali. CHADEMA imejikuta haina wigo wa kumkabiri Samia, ambaye naye hatumii njia zilezile za kuwakandamiza kama alizotumia Magufuli.

Kwa hali hii, ni ajenda gani wanayoweza kuishika na kumkabiri nayo Samia? Ukandamizaji hakuna, Katiba Mpya, inazungumzika, Tume Huru, hili tutalifanyia kazi. Sasa CHADEMA imebaki na kitu gani kuwapelekea wananchi wawaunge mkono!

Mbowe kautazama ukweli huu, na kuamua kama alivyo amua ni nini chama chake kifanye.

Wakati huo huo, huko ndani ya CCM vikelele vya kundi la Magufuli linatafutiwa dawa. Kamati Kuu na Kamati mhimu zinasukwa upya kuondoa takataka za Magufuli huko. Hawa wanaopiga kelele pembeni, wakati wakiwa ndani ya chama, wengi wanatupiwa minofu, na wale ambao ni sugu kama akina Polex2, akina Bashiru, akina Kalamaganda wote wamekwishawekwa pembeni.

Hiyo ndiyo CCM, ambayo, kwa rangi zake mabalimbali na uwezo wa kujigeuza kila mara, imeapa" kutawala nchi hii milele"! Kweli?

Kama vyama vyote vya upinzani tayari wanayo makundi yao ndani ya CCM, yako wapi tena matumaini ya waTanzania?

Kwa mwendo huu huu, kuna siku tutajikuta akina Thomas Sankara wakiibuka bila ya kutegemewa. Hilo ndilo litakaloiondoa CCM na makundi yake yote, ndani na nje ya chama.

Sikuhariri chochote, naomba usinilaumu kwa makosa ya uandishi.
Hakuna kitu,pitia wimbo wa nyerere wa dr Remmy you tube utajua watanzania wameichoka ccm mda sana
 
Tanzania ni nchi yenye usiri mkubwa mno, na bahati mbaya sana wananchi wengi tuna kasumba ya kushindwa kusoma nyakati. Kuhusu kutokea wakina Sankara, tayari hilo lishafanyika mwaka 2021 sema kwasababu ya mihemko ya kisiasa wengi tulishindwa kulitazama katika mapana yake. Mwendazake alienda, wengine waliumia, wengine walifurahia.

Tatizo lipo sehemu moja tu, katika lugha za kiusalama nchini Tanzania, Raisi ni alama muhimu mno ya ustawi wa nchi. Awe mzuri au awe mbaya, ni lazima dola lifanye kazi ya ziada kumlinda hadi pale anapomaliza muda wake. Tulikubaliana kwamba ni miaka kumi kwa kila Raisi. Huu utaratibu uvunjwe tu kwasababu asilia, lakini kama ni sababu za kisiasa au mkono wa mtu, nchi ni lazima iingie kwenye matatizo. Inaweza isiwe leo au kesho, lakini lazima matokeo myaone tu.

Mzee Nyerere alitengeneza mfumo wa aina yake hapa nchini. Hadi kufika mwaka 1985 alifanyiwa majaribio mengi na watu waliotaka kuwa wakina Sankara, Rawlings na Gaddafi. Mara zote alipona, siyo kwasababu ya kuwa na mfumo wenye nguvu, ila kwasababu wengi ndani ya mfumo walifahamu madhara ambayo yangetokea endapo mtu kama Nyerere angeondolewa kiholela. Hata wale ambao walikuwa hawakubaliana na sera zake walifahamu vizuri madhara yake ukizingatia hali ya siasa za Afrika wakati huo. Dola ilihakikisha mzee anakuwa salama, na mambo yalivyoenda kombo walimpa ushauri ang'atuke.

Baada ya kung'atuka ukajengeka utamaduni kwamba Raisi hawezi kugusika. Hivyo tutashika sharubu za watu wote lakini siyo za Raisi. Wengi akiwemo Mzee Nyerere hawakumkubali Mzee Mwinyi, lakini kuheshimu taratibu za nchi na kudumisha amani, ilikuwa ni lazima amalize muda wake akiwa salama. Alitoka Warioba na baraza zima lakini Mwinyi akabaki. Huu utaratibu ulienda hadi kwa Mzee Kikwete, ambaye mbali na kuwa na kashfa kibao za ufisadi, walitolewa kafara wengine lakini yeye dola lilimlinda.

Hata wale wasiomkubali Mzee Kikwete na kuyatambua madhaifu yake, walimlinda kwasababu ya utaratibu uliowekwa nchini, kwamba Raisi hagusiki. Hili wanasiasa, wanausalama na raia tunalifahamu vizuri. Hata Tundu Lissu wakati wa kashfa ya TEGETA ESCROW alisema dhahiri, kwamba Raisi akitolewa madarakani utatokea mtikisiko mkubwa nchini, hivyo tushughulike na hawa watu wa chini yake. Wanausalama wengi waliishia kumkomesha tu kwa kuvujisha taarifa za kinachoendelea Ikulu, lakini waliacha amalize salama.

Utaratibu ulienda vizuri, mpaka pale ulipoharibiwa mwaka 2021. Kuna madhara makubwa kwenye makosa yaliyofanyika mwaka 2021. Mfano mbaya mno umewekwa, A bad precedent, kwamba Raisi anaweza akatolewa madarakani kwa namna yoyote ile bila madhara kutokea. Kama mwendazake ambaye alilindwa kuliko maraisi wote aliondoka na hayajatokea madhara yoyote, nini kitazuia mwingine asitolewe endapo kundi fulani ndani ya chama tawala au taasisi za kiusalama litataka mtawala atoke ?

Watanzania wengi, hasa wale wa kwenye vyombo vya usalama ambako mara zote watu aina ya Sankara na Rawlings hutokea huko wameshakula A Forbidden Fruit, hivyo macho yao ya kutambua mema na mabaya yamefunguka. Aheri wangeendelea kuaminishwa kwamba Raisi hagusiki, na akigusika yanaweza kutokea madhara. Kinyume chake wameoneshwa kwamba hakuna ambaye hagusiki hapa nchini. Siku za mbeleni, wanaweza wasiwe hawa mnaowaita Sukuma-Gang, bali genge jingine kabisa ambalo litazua taharuki kubwa, chama tawala ndivyo kilivyo.

Katika mahojiano na wahaini wa mwaka 1982, walikiri kuogopa madhara ambayo yangetokea kwa serikali yao endapo Mzee Nyerere angekutwa na jambo baya, kuuwawa au kutolewa madarakani. Katika taarifa zao wanasema kwamba Tanzania ingevamiwa na nchi jirani kama Msumbuji, Angola na Uganda ambazo maraisi wake walikuwa ni wafuasi kindakindaki wa Mzee Nyerere. Walikuja na mkakati kwamba pindi wamepindua nchi, basi kuidhibiti Msumbiji wangeanzisha mahusiano na magaidi ya Renamo na kuidhibiti Angola wangeanzisha mahusiano na UNITA. Haya yangetokea Tanzania isingetawalika.

Kule dola la Roma, kuna kipindi walipitia majanga kwa zaidi ya miaka 50, A Third Century Crisis. Kipindi hiki hakuna mfalme ndani ya dola la Rumi aliyefanikiwa kukaa kwenye kiti zaidi ya miaka saba bila kuuwawa au kupinduliwa na wanajeshi wake. Mambo yalianza kimzaha mzaha baada ya wanajeshi na majasusi kumuua mfalme Severus Alexander na kumuweka mtu mwingine. Wanajeshi na majasusi baada ya kuona kwamba wanaweza kumtoa mfalme ambaye alikuwa anachukuliwa kama mungu mtu, huu ndiyo ukawa utamaduni wao mpya kwa miaka zaidi ya hamsini.

Msihangaike na upinzani, chama tawala kimegawanyika kuliko wakati wowote ule. Huku ndiko upinzani utaanzia. Kuna watu wanaviziana na endapo kundi linalotawala leo hii litafanya makosa kidogo tu, basi tunaweza kuongelea mengine. Baada ya mwendazake lilifanyika jaribio kubwa ambalo halikufanikiwa. Huu ni ushahidi tosha kwamba nyumba imegawanyika, ndiyo maana inatumika nguvu kubwa mno kumsifia mtawala wa sasa huku tukimchafua mtawala wa zamani.
 
Mkuu 'GWAMAKA USWEGE', nimekusoma, nikatoka na akili iliyochanganyikiwa nisijue nishike lipi niache lipi.

Lakini nimekusoma kwa utulivu kabisa, toka mstari wa kwanza hadi wa mwisho.
 
Tanzania ni nchi yenye usiri mkubwa mno, na bahati mbaya sana wananchi wengi tuna kasumba ya kushindwa kusoma nyakati. Kuhusu kutokea wakina Sankara, tayari hilo lishafanyika mwaka 2021 sema kwasababu ya mihemko ya kisiasa wengi tulishindwa kulitazama katika mapana yake. Mwendazake alienda, wengine waliumia, wengine walifurahia.

Tatizo lipo sehemu moja tu, katika lugha za kiusalama nchini Tanzania, Raisi ni alama muhimu mno ya ustawi wa nchi. Awe mzuri au awe mbaya, ni lazima dola lifanye kazi ya ziada kumlinda hadi pale anapomaliza muda wake. Tulikubaliana kwamba ni miaka kumi kwa kila Raisi. Huu utaratibu uvunjwe tu kwasababu asilia, lakini kama ni sababu za kisiasa au mkono wa mtu, nchi ni lazima iingie kwenye matatizo. Inaweza isiwe leo au kesho, lakini lazima matokeo myaone tu.

Mzee Nyerere alitengeneza mfumo wa aina yake hapa nchini. Hadi kufika mwaka 1985 alifanyiwa majaribio mengi na watu waliotaka kuwa wakina Sankara, Rawlings na Gaddafi. Mara zote alipona, siyo kwasababu ya kuwa na mfumo wenye nguvu, ila kwasababu wengi ndani ya mfumo walifahamu madhara ambayo yangetokea endapo mtu kama Nyerere angeondolewa kiholela. Hata wale ambao walikuwa hawakubaliana na sera zake walifahamu vizuri madhara yake ukizingatia hali ya siasa za Afrika wakati huo. Dola ilifanya ilihakikisha mzee anakuwa salama, na mambo yalivyoenda kombo walimpa ushauri ang'atuke.

Baada ya kung'atuka ukajengeka utamaduni kwamba Raisi hawezi kugusika. Hivyo tutashika sharubu za watu wote lakini siyo za Raisi. Wengi akiwemo Mzee Nyerere hawakumkubali Mzee Mwinyi, lakini kuheshimu taratibu za nchi na kudumisha amani, ilikuwa ni lazima amalize muda wake akiwa salama. Alitoka Warioba na baraza zima lakini Mwinyi akabaki. Huu utaratibu ulienda hadi kwa Mzee Kikwete, ambaye mbali na kuwa na kashfa kibao za ufisadi, walitolewa kafara wengine lakini yeye dola lilimlinda.

Hata wale wasiomkubali Mzee Kikwete na kuyatambua madhaifu yake, walimlinda kwasababu ya utaratibu uliowekwa nchini, kwamba Raisi hagusiki. Hili wanasiasa, wanausalama na raia tunalifahamu vizuri. Hata Tundu Lissu wakati wa kashfa ya TEGETA ESCROW alisema dhahiri, kwamba Raisi akitolewa madarakani utatokea mtikisiko mkubwa nchini, hivyo tushughulike na hawa watu wa chini yake. Wanausalama wengi waliishia kumkomesha tu kwa kuvujisha taarifa za kinachoendelea Ikulu, lakini waliacha amalize salama.

Utaratibu ulienda vizuri, mpaka pale ulipoharibiwa mwaka 2021. Kuna madhara makubwa kwenye makosa yaliyofanyika mwaka 2021. Mfano mbaya mno umewekwa, A bad precedent, kwamba Raisi anaweza akatolewa madarakani kwa namna yoyote ile bila madhara kutokea. Kama mwendazake ambaye alilindwa kuliko maraisi wote aliondoka na hayajatokea madhara yoyote, nini kitazuia mwingine asitolewe endapo kundi fulani ndani ya chama tawala au taasisi za kiusalama litataka mtawala atoke ?

Watanzania wengi, hasa wale wa kwenye vyombo vya usalama ambako mara zote watu aina ya Sankara na Rawlings hutokea huko wameshakula A Forbidden Fruit, hivyo macho yao ya kutambua mema na mabaya yamefunguka. Aheri wangeendelea kuaminishwa kwamba Raisi hagusiki, na akigusika yanaweza kutokea madhara. Kinyume chake wameoneshwa kwamba hakuna ambaye hagusiki hapa nchini. Siku za mbeleni, wanaweza wasiwe hawa mnaowaita Sukuga-Gang, bali genge jingine kabisa ambalo litazua taharuki kubwa, chama tawala ndivyo kilivyo.

Katika mahojiano na wahaini wa mwaka 1982, walikiri kuogopa madhara ambayo yangetokea kwa serikali yao endapo Mzee Nyerere angekutwa na jambo baya, kuuwawa au kutolewa madarakani. Katika taarifa zao wanasema kwamba Tanzania ingevamiwa na nchi jirani kama Msumbuji, Angola na Uganda ambazo maraisi wake walikuwa ni wafuasi kindakindaki wa Mzee Nyerere. Walikuja na mkakati kwamba pindi wamepindua nchi, basi kuidhibiti Msumbijia wangeanzisha mahusiano na magaidi ya Renamo na kuidhibiti Angola wangeanzisha mahusiano na UNITA. Haya yangetokea Tanzania isingetawalika.

Kule dola la Roma, kuna kipindi walipitia majanga kwa zaidi ya miaka 50, The Third Century Crisis. Kipindi hiki hakuna mfalme ndani ya dola la Rumi aliyefanikiwa kukaa kwenye kiti zaidi ya miaka saba bila kuuwawa au kupinduliwa na wanajeshi wake. Mambo yalianza kimzaha mzaha baada ya wanajeshi na majasusi kumuua mfalme Severus Alexander na kumuweka mtu mwingine. Wanajeshi na majasusi baada ya kuona kwamba wanaweza kumtoa mfalme ambaye alikuwa anachukuliwa kama mungu mtu, huu ndiyo ukawa utamaduni wao mpya kwa miaka zaidi ya hamsini.

Msihangaike na upinzani, chama tawala kimegawanyika kuliko wakati wowote ule. Huku ndiko upinzani utaanzia. Kuna watu wanaviziana na endapo kundi linalotawala leo hii litafanya makosa kidogo tu, basi tunaweza kuongelea mengine. Baada ya mwendazake lilifanyika jaribio kubwa ambalo halikufanikiwa. Huu ni ushahidi tosha kwamba nyumba imegawanyika, ndiyo maana inatumika nguvu kubwa mno kumsifia mtawala wa sasa huku tukimchafua mtawala wa zamani.
Much respect to you, ww Si mvuja JASHO kama wengine, umeandika kama mtu mwenye uhakika wa kula.

Kwa uchambuzi wako murua,

Njia pekee ni Dola kuhakikisha inapatikana KATIBA mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA.

Ikikosekana hiyo, basi inabidi turudi misri tu, hamna namna.

Bila mijeledi,chakula hakijaingia kinywani Bado.
 
Nadhani hatuna namna tena kwa hali inavyokwenda.

Hili la kutokea machafuko au jeshi kupindua serikali ndio litaleta mabadiliko ya kweli ya kiutawala ndani ya nchi hii. Siku za nyuma kidogo naona ulikuwa huamini katika ukweli huu, lakini sasa unaanza kuuona ukweli huu. Hongera kwa kuuona ukweli huu.
 
Tanzania ni nchi yenye usiri mkubwa mno, na bahati mbaya sana wananchi wengi tuna kasumba ya kushindwa kusoma nyakati. Kuhusu kutokea wakina Sankara, tayari hilo lishafanyika mwaka 2021 sema kwasababu ya mihemko ya kisiasa wengi tulishindwa kulitazama katika mapana yake. Mwendazake alienda, wengine waliumia, wengine walifurahia.

Tatizo lipo sehemu moja tu, katika lugha za kiusalama nchini Tanzania, Raisi ni alama muhimu mno ya ustawi wa nchi. Awe mzuri au awe mbaya, ni lazima dola lifanye kazi ya ziada kumlinda hadi pale anapomaliza muda wake. Tulikubaliana kwamba ni miaka kumi kwa kila Raisi. Huu utaratibu uvunjwe tu kwasababu asilia, lakini kama ni sababu za kisiasa au mkono wa mtu, nchi ni lazima iingie kwenye matatizo. Inaweza isiwe leo au kesho, lakini lazima matokeo myaone tu.

Mzee Nyerere alitengeneza mfumo wa aina yake hapa nchini. Hadi kufika mwaka 1985 alifanyiwa majaribio mengi na watu waliotaka kuwa wakina Sankara, Rawlings na Gaddafi. Mara zote alipona, siyo kwasababu ya kuwa na mfumo wenye nguvu, ila kwasababu wengi ndani ya mfumo walifahamu madhara ambayo yangetokea endapo mtu kama Nyerere angeondolewa kiholela. Hata wale ambao walikuwa hawakubaliana na sera zake walifahamu vizuri madhara yake ukizingatia hali ya siasa za Afrika wakati huo. Dola ilifanya ilihakikisha mzee anakuwa salama, na mambo yalivyoenda kombo walimpa ushauri ang'atuke.

Baada ya kung'atuka ukajengeka utamaduni kwamba Raisi hawezi kugusika. Hivyo tutashika sharubu za watu wote lakini siyo za Raisi. Wengi akiwemo Mzee Nyerere hawakumkubali Mzee Mwinyi, lakini kuheshimu taratibu za nchi na kudumisha amani, ilikuwa ni lazima amalize muda wake akiwa salama. Alitoka Warioba na baraza zima lakini Mwinyi akabaki. Huu utaratibu ulienda hadi kwa Mzee Kikwete, ambaye mbali na kuwa na kashfa kibao za ufisadi, walitolewa kafara wengine lakini yeye dola lilimlinda.

Hata wale wasiomkubali Mzee Kikwete na kuyatambua madhaifu yake, walimlinda kwasababu ya utaratibu uliowekwa nchini, kwamba Raisi hagusiki. Hili wanasiasa, wanausalama na raia tunalifahamu vizuri. Hata Tundu Lissu wakati wa kashfa ya TEGETA ESCROW alisema dhahiri, kwamba Raisi akitolewa madarakani utatokea mtikisiko mkubwa nchini, hivyo tushughulike na hawa watu wa chini yake. Wanausalama wengi waliishia kumkomesha tu kwa kuvujisha taarifa za kinachoendelea Ikulu, lakini waliacha amalize salama.

Utaratibu ulienda vizuri, mpaka pale ulipoharibiwa mwaka 2021. Kuna madhara makubwa kwenye makosa yaliyofanyika mwaka 2021. Mfano mbaya mno umewekwa, A bad precedent, kwamba Raisi anaweza akatolewa madarakani kwa namna yoyote ile bila madhara kutokea. Kama mwendazake ambaye alilindwa kuliko maraisi wote aliondoka na hayajatokea madhara yoyote, nini kitazuia mwingine asitolewe endapo kundi fulani ndani ya chama tawala au taasisi za kiusalama litataka mtawala atoke ?

Watanzania wengi, hasa wale wa kwenye vyombo vya usalama ambako mara zote watu aina ya Sankara na Rawlings hutokea huko wameshakula A Forbidden Fruit, hivyo macho yao ya kutambua mema na mabaya yamefunguka. Aheri wangeendelea kuaminishwa kwamba Raisi hagusiki, na akigusika yanaweza kutokea madhara. Kinyume chake wameoneshwa kwamba hakuna ambaye hagusiki hapa nchini. Siku za mbeleni, wanaweza wasiwe hawa mnaowaita Sukuga-Gang, bali genge jingine kabisa ambalo litazua taharuki kubwa, chama tawala ndivyo kilivyo.

Katika mahojiano na wahaini wa mwaka 1982, walikiri kuogopa madhara ambayo yangetokea kwa serikali yao endapo Mzee Nyerere angekutwa na jambo baya, kuuwawa au kutolewa madarakani. Katika taarifa zao wanasema kwamba Tanzania ingevamiwa na nchi jirani kama Msumbuji, Angola na Uganda ambazo maraisi wake walikuwa ni wafuasi kindakindaki wa Mzee Nyerere. Walikuja na mkakati kwamba pindi wamepindua nchi, basi kuidhibiti Msumbijia wangeanzisha mahusiano na magaidi ya Renamo na kuidhibiti Angola wangeanzisha mahusiano na UNITA. Haya yangetokea Tanzania isingetawalika.

Kule dola la Roma, kuna kipindi walipitia majanga kwa zaidi ya miaka 50, The Third Century Crisis. Kipindi hiki hakuna mfalme ndani ya dola la Rumi aliyefanikiwa kukaa kwenye kiti zaidi ya miaka saba bila kuuwawa au kupinduliwa na wanajeshi wake. Mambo yalianza kimzaha mzaha baada ya wanajeshi na majasusi kumuua mfalme Severus Alexander na kumuweka mtu mwingine. Wanajeshi na majasusi baada ya kuona kwamba wanaweza kumtoa mfalme ambaye alikuwa anachukuliwa kama mungu mtu, huu ndiyo ukawa utamaduni wao mpya kwa miaka zaidi ya hamsini.

Msihangaike na upinzani, chama tawala kimegawanyika kuliko wakati wowote ule. Huku ndiko upinzani utaanzia. Kuna watu wanaviziana na endapo kundi linalotawala leo hii litafanya makosa kidogo tu, basi tunaweza kuongelea mengine. Baada ya mwendazake lilifanyika jaribio kubwa ambalo halikufanikiwa. Huu ni ushahidi tosha kwamba nyumba imegawanyika, ndiyo maana inatumika nguvu kubwa mno kumsifia mtawala wa sasa huku tukimchafua mtawala wa zamani.
Kwahiyo inawezekana Maridhiano ni mbinu ya kulilinda Kundi fulani dhidi ya jingine.?
 
Hili la kutokea machafuko au jeshi kupindua serikali ndio litaleta mabadiliko ya kweli ya kiutawala ndani ya nchi hii. Siku za nyuma kidogo naona ulikuwa huamini katika ukweli huu, lakini sasa unaanza kuuona ukweli huu. Hongera kwa kuuona ukweli huu.
KATIBA mpya itawaondolea hiyo appetite ya kula nyama za ww..tu.
 
CCM kimekuwa chama chenye milengo mbalimbali (rangi nyingi), na kwa maoni yangu hii ni sababu mojawapo inayofanya vyama vya upinzani wapate taabu sana kukikabiri barabara chama hiki na kukiondoa kwenye madaraka.

Ni hoja yangu kwamba, ni ndani ya CCM hiyo hiyo kwa kuwa na makundi mbalimbali, yenye milengo mbalimbali kiasi kwamba hivi vyama vya upinzani vilivyoko nje ya chama hicho, mahitaji yao (wenzao wenye milengo kama wao) tayari wamo ndani ya CCM.

Kwa hiyo, kwa chama kama CHADEMA, walipata taabu sana toka kwa kundi lililo upande wa Magufuli, huku wenzao waliomo ndani ya chama hicho, kutokana na muundo wa chama, hawakuweza kuinua kidole na kuwatetea CHADEMA.
Baada ya Magufuli kuondoka, kama alivyoondoka, na kundi lililokuwa limenyamaza likiwa upande wa akina Samia, sasa ndio wanaotawala anga. Kundi hili ni kundi lenye misimamo inayokubaliana karibu kwa kila kitu na CHADEMA, kasoro kuwaachia washike serikali. CHADEMA imejikuta haina wigo wa kumkabiri Samia, ambaye naye hatumii njia zilezile za kuwakandamiza kama alizotumia Magufuli.

Kwa hali hii, ni ajenda gani wanayoweza kuishika na kumkabiri nayo Samia? Ukandamizaji hakuna, Katiba Mpya, inazungumzika, Tume Huru, hili tutalifanyia kazi. Sasa CHADEMA imebaki na kitu gani kuwapelekea wananchi wawaunge mkono!

Mbowe kautazama ukweli huu, na kuamua kama alivyo amua ni nini chama chake kifanye.

Wakati huo huo, huko ndani ya CCM vikelele vya kundi la Magufuli linatafutiwa dawa. Kamati Kuu na Kamati mhimu zinasukwa upya kuondoa takataka za Magufuli huko. Hawa wanaopiga kelele pembeni, wakati wakiwa ndani ya chama, wengi wanatupiwa minofu, na wale ambao ni sugu kama akina Polex2, akina Bashiru, akina Kalamaganda wote wamekwishawekwa pembeni.

Hiyo ndiyo CCM, ambayo, kwa rangi zake mabalimbali na uwezo wa kujigeuza kila mara, imeapa" kutawala nchi hii milele"! Kweli?

Kama vyama vyote vya upinzani tayari wanayo makundi yao ndani ya CCM, yako wapi tena matumaini ya waTanzania?

Kwa mwendo huu huu, kuna siku tutajikuta akina Thomas Sankara wakiibuka bila ya kutegemewa. Hilo ndilo litakaloiondoa CCM na makundi yake yote, ndani na nje ya chama.

Sikuhariri chochote, naomba usinilaumu kwa makosa ya uandishi.

Ni kweli CCM imefanya mengi , Hizi ndizo sera za CCM zilivyotupeleka juu kwenye Elimu

 
Tanzania ni nchi yenye usiri mkubwa mno, na bahati mbaya sana wananchi wengi tuna kasumba ya kushindwa kusoma nyakati. Kuhusu kutokea wakina Sankara, tayari hilo lishafanyika mwaka 2021 sema kwasababu ya mihemko ya kisiasa wengi tulishindwa kulitazama katika mapana yake. Mwendazake alienda, wengine waliumia, wengine walifurahia.

Tatizo lipo sehemu moja tu, katika lugha za kiusalama nchini Tanzania, Raisi ni alama muhimu mno ya ustawi wa nchi. Awe mzuri au awe mbaya, ni lazima dola lifanye kazi ya ziada kumlinda hadi pale anapomaliza muda wake. Tulikubaliana kwamba ni miaka kumi kwa kila Raisi. Huu utaratibu uvunjwe tu kwasababu asilia, lakini kama ni sababu za kisiasa au mkono wa mtu, nchi ni lazima iingie kwenye matatizo. Inaweza isiwe leo au kesho, lakini lazima matokeo myaone tu.

Mzee Nyerere alitengeneza mfumo wa aina yake hapa nchini. Hadi kufika mwaka 1985 alifanyiwa majaribio mengi na watu waliotaka kuwa wakina Sankara, Rawlings na Gaddafi. Mara zote alipona, siyo kwasababu ya kuwa na mfumo wenye nguvu, ila kwasababu wengi ndani ya mfumo walifahamu madhara ambayo yangetokea endapo mtu kama Nyerere angeondolewa kiholela. Hata wale ambao walikuwa hawakubaliana na sera zake walifahamu vizuri madhara yake ukizingatia hali ya siasa za Afrika wakati huo. Dola ilifanya ilihakikisha mzee anakuwa salama, na mambo yalivyoenda kombo walimpa ushauri ang'atuke.

Baada ya kung'atuka ukajengeka utamaduni kwamba Raisi hawezi kugusika. Hivyo tutashika sharubu za watu wote lakini siyo za Raisi. Wengi akiwemo Mzee Nyerere hawakumkubali Mzee Mwinyi, lakini kuheshimu taratibu za nchi na kudumisha amani, ilikuwa ni lazima amalize muda wake akiwa salama. Alitoka Warioba na baraza zima lakini Mwinyi akabaki. Huu utaratibu ulienda hadi kwa Mzee Kikwete, ambaye mbali na kuwa na kashfa kibao za ufisadi, walitolewa kafara wengine lakini yeye dola lilimlinda.

Hata wale wasiomkubali Mzee Kikwete na kuyatambua madhaifu yake, walimlinda kwasababu ya utaratibu uliowekwa nchini, kwamba Raisi hagusiki. Hili wanasiasa, wanausalama na raia tunalifahamu vizuri. Hata Tundu Lissu wakati wa kashfa ya TEGETA ESCROW alisema dhahiri, kwamba Raisi akitolewa madarakani utatokea mtikisiko mkubwa nchini, hivyo tushughulike na hawa watu wa chini yake. Wanausalama wengi waliishia kumkomesha tu kwa kuvujisha taarifa za kinachoendelea Ikulu, lakini waliacha amalize salama.

Utaratibu ulienda vizuri, mpaka pale ulipoharibiwa mwaka 2021. Kuna madhara makubwa kwenye makosa yaliyofanyika mwaka 2021. Mfano mbaya mno umewekwa, A bad precedent, kwamba Raisi anaweza akatolewa madarakani kwa namna yoyote ile bila madhara kutokea. Kama mwendazake ambaye alilindwa kuliko maraisi wote aliondoka na hayajatokea madhara yoyote, nini kitazuia mwingine asitolewe endapo kundi fulani ndani ya chama tawala au taasisi za kiusalama litataka mtawala atoke ?

Watanzania wengi, hasa wale wa kwenye vyombo vya usalama ambako mara zote watu aina ya Sankara na Rawlings hutokea huko wameshakula A Forbidden Fruit, hivyo macho yao ya kutambua mema na mabaya yamefunguka. Aheri wangeendelea kuaminishwa kwamba Raisi hagusiki, na akigusika yanaweza kutokea madhara. Kinyume chake wameoneshwa kwamba hakuna ambaye hagusiki hapa nchini. Siku za mbeleni, wanaweza wasiwe hawa mnaowaita Sukuga-Gang, bali genge jingine kabisa ambalo litazua taharuki kubwa, chama tawala ndivyo kilivyo.

Katika mahojiano na wahaini wa mwaka 1982, walikiri kuogopa madhara ambayo yangetokea kwa serikali yao endapo Mzee Nyerere angekutwa na jambo baya, kuuwawa au kutolewa madarakani. Katika taarifa zao wanasema kwamba Tanzania ingevamiwa na nchi jirani kama Msumbuji, Angola na Uganda ambazo maraisi wake walikuwa ni wafuasi kindakindaki wa Mzee Nyerere. Walikuja na mkakati kwamba pindi wamepindua nchi, basi kuidhibiti Msumbijia wangeanzisha mahusiano na magaidi ya Renamo na kuidhibiti Angola wangeanzisha mahusiano na UNITA. Haya yangetokea Tanzania isingetawalika.

Kule dola la Roma, kuna kipindi walipitia majanga kwa zaidi ya miaka 50, The Third Century Crisis. Kipindi hiki hakuna mfalme ndani ya dola la Rumi aliyefanikiwa kukaa kwenye kiti zaidi ya miaka saba bila kuuwawa au kupinduliwa na wanajeshi wake. Mambo yalianza kimzaha mzaha baada ya wanajeshi na majasusi kumuua mfalme Severus Alexander na kumuweka mtu mwingine. Wanajeshi na majasusi baada ya kuona kwamba wanaweza kumtoa mfalme ambaye alikuwa anachukuliwa kama mungu mtu, huu ndiyo ukawa utamaduni wao mpya kwa miaka zaidi ya hamsini.

Msihangaike na upinzani, chama tawala kimegawanyika kuliko wakati wowote ule. Huku ndiko upinzani utaanzia. Kuna watu wanaviziana na endapo kundi linalotawala leo hii litafanya makosa kidogo tu, basi tunaweza kuongelea mengine. Baada ya mwendazake lilifanyika jaribio kubwa ambalo halikufanikiwa. Huu ni ushahidi tosha kwamba nyumba imegawanyika, ndiyo maana inatumika nguvu kubwa mno kumsifia mtawala wa sasa huku tukimchafua mtawala wa zamani.
Umeandika point tupu, hongera sana mkuu ila umemaliza vibaya.
 
Mkuu 'GWAMAKA USWEGE', nimekusoma, nikatoka na akili iliyochanganyikiwa nisijue nishike lipi niache lipi.

Lakini nimekusoma kwa utulivu kabisa, toka mstari wa kwanza hadi wa mwisho.
Jamaa kaandika maelezo mengi lakini hayachoshi kusoma
 
Tanzania ni nchi yenye usiri mkubwa mno, na bahati mbaya sana wananchi wengi tuna kasumba ya kushindwa kusoma nyakati. Kuhusu kutokea wakina Sankara, tayari hilo lishafanyika mwaka 2021 sema kwasababu ya mihemko ya kisiasa wengi tulishindwa kulitazama katika mapana yake. Mwendazake alienda, wengine waliumia, wengine walifurahia.

Tatizo lipo sehemu moja tu, katika lugha za kiusalama nchini Tanzania, Raisi ni alama muhimu mno ya ustawi wa nchi. Awe mzuri au awe mbaya, ni lazima dola lifanye kazi ya ziada kumlinda hadi pale anapomaliza muda wake. Tulikubaliana kwamba ni miaka kumi kwa kila Raisi. Huu utaratibu uvunjwe tu kwasababu asilia, lakini kama ni sababu za kisiasa au mkono wa mtu, nchi ni lazima iingie kwenye matatizo. Inaweza isiwe leo au kesho, lakini lazima matokeo myaone tu.

Mzee Nyerere alitengeneza mfumo wa aina yake hapa nchini. Hadi kufika mwaka 1985 alifanyiwa majaribio mengi na watu waliotaka kuwa wakina Sankara, Rawlings na Gaddafi. Mara zote alipona, siyo kwasababu ya kuwa na mfumo wenye nguvu, ila kwasababu wengi ndani ya mfumo walifahamu madhara ambayo yangetokea endapo mtu kama Nyerere angeondolewa kiholela. Hata wale ambao walikuwa hawakubaliana na sera zake walifahamu vizuri madhara yake ukizingatia hali ya siasa za Afrika wakati huo. Dola ilifanya ilihakikisha mzee anakuwa salama, na mambo yalivyoenda kombo walimpa ushauri ang'atuke.

Baada ya kung'atuka ukajengeka utamaduni kwamba Raisi hawezi kugusika. Hivyo tutashika sharubu za watu wote lakini siyo za Raisi. Wengi akiwemo Mzee Nyerere hawakumkubali Mzee Mwinyi, lakini kuheshimu taratibu za nchi na kudumisha amani, ilikuwa ni lazima amalize muda wake akiwa salama. Alitoka Warioba na baraza zima lakini Mwinyi akabaki. Huu utaratibu ulienda hadi kwa Mzee Kikwete, ambaye mbali na kuwa na kashfa kibao za ufisadi, walitolewa kafara wengine lakini yeye dola lilimlinda.

Hata wale wasiomkubali Mzee Kikwete na kuyatambua madhaifu yake, walimlinda kwasababu ya utaratibu uliowekwa nchini, kwamba Raisi hagusiki. Hili wanasiasa, wanausalama na raia tunalifahamu vizuri. Hata Tundu Lissu wakati wa kashfa ya TEGETA ESCROW alisema dhahiri, kwamba Raisi akitolewa madarakani utatokea mtikisiko mkubwa nchini, hivyo tushughulike na hawa watu wa chini yake. Wanausalama wengi waliishia kumkomesha tu kwa kuvujisha taarifa za kinachoendelea Ikulu, lakini waliacha amalize salama.

Utaratibu ulienda vizuri, mpaka pale ulipoharibiwa mwaka 2021. Kuna madhara makubwa kwenye makosa yaliyofanyika mwaka 2021. Mfano mbaya mno umewekwa, A bad precedent, kwamba Raisi anaweza akatolewa madarakani kwa namna yoyote ile bila madhara kutokea. Kama mwendazake ambaye alilindwa kuliko maraisi wote aliondoka na hayajatokea madhara yoyote, nini kitazuia mwingine asitolewe endapo kundi fulani ndani ya chama tawala au taasisi za kiusalama litataka mtawala atoke ?

Watanzania wengi, hasa wale wa kwenye vyombo vya usalama ambako mara zote watu aina ya Sankara na Rawlings hutokea huko wameshakula A Forbidden Fruit, hivyo macho yao ya kutambua mema na mabaya yamefunguka. Aheri wangeendelea kuaminishwa kwamba Raisi hagusiki, na akigusika yanaweza kutokea madhara. Kinyume chake wameoneshwa kwamba hakuna ambaye hagusiki hapa nchini. Siku za mbeleni, wanaweza wasiwe hawa mnaowaita Sukuga-Gang, bali genge jingine kabisa ambalo litazua taharuki kubwa, chama tawala ndivyo kilivyo.

Katika mahojiano na wahaini wa mwaka 1982, walikiri kuogopa madhara ambayo yangetokea kwa serikali yao endapo Mzee Nyerere angekutwa na jambo baya, kuuwawa au kutolewa madarakani. Katika taarifa zao wanasema kwamba Tanzania ingevamiwa na nchi jirani kama Msumbuji, Angola na Uganda ambazo maraisi wake walikuwa ni wafuasi kindakindaki wa Mzee Nyerere. Walikuja na mkakati kwamba pindi wamepindua nchi, basi kuidhibiti Msumbijia wangeanzisha mahusiano na magaidi ya Renamo na kuidhibiti Angola wangeanzisha mahusiano na UNITA. Haya yangetokea Tanzania isingetawalika.

Kule dola la Roma, kuna kipindi walipitia majanga kwa zaidi ya miaka 50, The Third Century Crisis. Kipindi hiki hakuna mfalme ndani ya dola la Rumi aliyefanikiwa kukaa kwenye kiti zaidi ya miaka saba bila kuuwawa au kupinduliwa na wanajeshi wake. Mambo yalianza kimzaha mzaha baada ya wanajeshi na majasusi kumuua mfalme Severus Alexander na kumuweka mtu mwingine. Wanajeshi na majasusi baada ya kuona kwamba wanaweza kumtoa mfalme ambaye alikuwa anachukuliwa kama mungu mtu, huu ndiyo ukawa utamaduni wao mpya kwa miaka zaidi ya hamsini.

Msihangaike na upinzani, chama tawala kimegawanyika kuliko wakati wowote ule. Huku ndiko upinzani utaanzia. Kuna watu wanaviziana na endapo kundi linalotawala leo hii litafanya makosa kidogo tu, basi tunaweza kuongelea mengine. Baada ya mwendazake lilifanyika jaribio kubwa ambalo halikufanikiwa. Huu ni ushahidi tosha kwamba nyumba imegawanyika, ndiyo maana inatumika nguvu kubwa mno kumsifia mtawala wa sasa huku tukimchafua mtawala wa zamani.
Umeongea mengi kwa kutazamisha kwamba tabia iliozuiliwa kwa gharama kubwa tangu kipindi cha waasisi leo hii imetendeka. Hivyo kuna uwezekano wakujirudia tena.

Labda nifupishe ulikusudia kusema kwamba 'Mtu akishahonja nyama ya mtu hataacha kamwe'.
 
CCM kimekuwa chama chenye milengo mbalimbali (rangi nyingi), na kwa maoni yangu hii ni sababu mojawapo inayofanya vyama vya upinzani wapate taabu sana kukikabiri barabara chama hiki na kukiondoa kwenye madaraka.

Ni hoja yangu kwamba, ni ndani ya CCM hiyo hiyo kwa kuwa na makundi mbalimbali, yenye milengo mbalimbali kiasi kwamba hivi vyama vya upinzani vilivyoko nje ya chama hicho, mahitaji yao (wenzao wenye milengo kama wao) tayari wamo ndani ya CCM.

Kwa hiyo, kwa chama kama CHADEMA, walipata taabu sana toka kwa kundi lililo upande wa Magufuli, huku wenzao waliomo ndani ya chama hicho, kutokana na muundo wa chama, hawakuweza kuinua kidole na kuwatetea CHADEMA.
Baada ya Magufuli kuondoka, kama alivyoondoka, na kundi lililokuwa limenyamaza likiwa upande wa akina Samia, sasa ndio wanaotawala anga. Kundi hili ni kundi lenye misimamo inayokubaliana karibu kwa kila kitu na CHADEMA, kasoro kuwaachia washike serikali. CHADEMA imejikuta haina wigo wa kumkabiri Samia, ambaye naye hatumii njia zilezile za kuwakandamiza kama alizotumia Magufuli.

Kwa hali hii, ni ajenda gani wanayoweza kuishika na kumkabiri nayo Samia? Ukandamizaji hakuna, Katiba Mpya, inazungumzika, Tume Huru, hili tutalifanyia kazi. Sasa CHADEMA imebaki na kitu gani kuwapelekea wananchi wawaunge mkono!

Mbowe kautazama ukweli huu, na kuamua kama alivyo amua ni nini chama chake kifanye.

Wakati huo huo, huko ndani ya CCM vikelele vya kundi la Magufuli linatafutiwa dawa. Kamati Kuu na Kamati mhimu zinasukwa upya kuondoa takataka za Magufuli huko. Hawa wanaopiga kelele pembeni, wakati wakiwa ndani ya chama, wengi wanatupiwa minofu, na wale ambao ni sugu kama akina Polex2, akina Bashiru, akina Kalamaganda wote wamekwishawekwa pembeni.

Hiyo ndiyo CCM, ambayo, kwa rangi zake mabalimbali na uwezo wa kujigeuza kila mara, imeapa" kutawala nchi hii milele"! Kweli?

Kama vyama vyote vya upinzani tayari wanayo makundi yao ndani ya CCM, yako wapi tena matumaini ya waTanzania?

Kwa mwendo huu huu, kuna siku tutajikuta akina Thomas Sankara wakiibuka bila ya kutegemewa. Hilo ndilo litakaloiondoa CCM na makundi yake yote, ndani na nje ya chama.

Sikuhariri chochote, naomba usinilaumu kwa makosa ya uandishi.
Ukiona wazee wa chama wanatoka hadharani kujisifu juu ya yaliyomtokea mtangulizi,

Jua kuwa wameshagawana fito za nyumba Yao.
 
Hili la kutokea machafuko au jeshi kupindua serikali ndio litaleta mabadiliko ya kweli ya kiutawala ndani ya nchi hii. Siku za nyuma kidogo naona ulikuwa huamini katika ukweli huu, lakini sasa unaanza kuuona ukweli huu. Hongera kwa kuuona ukweli huu.
Hapana.
Nilijua hunielewi ninaandika nini na inawezekana ukawa hunielewi kwa haya niliyoandika hapa.

Tuliyoshindwa kuelewana kati yetu huko nyuma yako wazi kabisa. Usidhani nimebadili msimamo juu yake. sasa.
 
Ni kweli CCM imefanya mengi , Hizi ndizo sera za CCM zilivyotupeleka juu kwenye Elimu

View attachment 2545909
Kwani yule Waziri wa "Pesa" mwenye gari la gharama ya Tsh 600 milioni anasemaje kuhusu hali hii mkuu 'Gavana'.

Ni kwamba CCM imetufikisha mbali kweli kama mtu anaweza kutembelea Tsh 600 millioni!

Hao unaowaona hapo kwenye hiyo picha wakipiga maneno mengi sana, na wao wanapigania hicho hicho ili wanufaike.

Mtu kama Samia, hayo ya hao watoto kuwa 'innovative' katika kujitafutia elimu yeye hayo hayamhusu, na wala hayamo moyoni mwake hata kidogo. Yeye anawaza kutafuta maendeleo ya Tanzania kutoka nje ya nchi.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom