Unatumia unit ngapi za LUKU kwa siku?

Unatumia unit ngapi za LUKU kwa siku?

Mi nilinunua umeme wa buku 10 ukakaa miezi miwili.

Juzi ukaisha. Nikaweka wa buku 2 ile Alhamisi,nadhaniutakaa week 2.

Pasi, feni, chaja, PC, taa moja mbili.

Uwa sikai ghetto mchana.
una tarrif ipi?
 
Unit 1.5 kwa siku tupo wapangaji vyumba vitatu mimi kwangu nina tv music pas fridge japo huwa nazima wakat wa night na kuwasha wakat wa day hatushindi nyumban na wote ni bachelors nadhani hiyo ndo sabb umeme kidog unatumika
basi nyie ni tarrif zero
 
natamani mtaalamu mmoja wa umeme,atoe somo kuhusu tarrif za umeme zilivyo
Mkuu tarrif siyo shida!

Hata kama una tarrif zero kama una rundo la la vitu lazima matumizi yawe makubwa!
Ndio maana kuna watu walikuwa na tarrif zero ila mfumo ukawatoa kutokana na kukiuka masharti ya matumizi.

Tarrif zero unapata unit 70 kwa elfu 10 ila wanakwambia kwenye matumizi yako zisizidi unit 70 kwa mwezi, zikizidi mfumo unqkutoa ndio maana wengi wameshindwa maana itabidi utumie kwa kujibana sana, yani kwa siku zisizidi unit 2

Kiufupi ni kwamba umeme majumbani upo kama gari, injini kubwa mafuta mengi na kinyume chake.
 
Daaah faza hi nyumba nayofanyia.biashara aiseee kuna unywaji wa umeme na sio utumiaji aiseee....

Aaaah nyumba inakunywa umeme hii hapo ukisema uwashe friji jua kuna kubwiwa kwa umeme
 
Back
Top Bottom