BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Mkuu Mwanajamvi...
Nimeona mara nyingi wanaume wakikaa pamoja utawasikia...Yule si anashauriwa na mkewe?..Ndo maana yuko kama amechanganyikiwa muda wote!
Ina maana wanawake wana ushauri mbaya sana?
Ni ushauri upi tuupokee na upi tuukatae toka kwa hawa raia?
Si kweli kabisa Wanawake wana ushauri mbaya. Na sioni ubaya wowote kwa Mume/Boyfriend kupokea na kuukubali ushauri wa Mwanamke kwani Wanawake ni binadamu kama sisi na wana uwezo mkubwa sana wa kutoa ushauri mzuri katika mambo mbali mbali. Kama Mwanamke anaweza kuwa Prime Minister wa UK na pia Waziri wa Mambo ya Nje US na kushika nyadhifa nyingine za juu katika nchi mbali mbali duniani, basi sioni sababu yoyote ile ya Wanaume kuukataa ushauri wa Mwanamke kutokana na jinsia yao tu. Tuacheni fikra potofu za mwaka 47 za kuwadhalilisha Wanawake kutokana na jinsia yao tu, hawa viumbe wana uwezo wa kufanya maamuzi mazuri tu kama Wanaume na kuna ushahidi wa kutosha kuhusu hili.