Sisi wanaume wengine tuna matatizo kweli, jana nilienda na familia kule kwenye michezo ya maji.......mimi kwa kweli huwa nanunuaga magazeti alafu naenda kaunta wakati wife anaogelea na watoto..... nikiwa nalelekea kule kaunta dada mmoja akaniomba gazeti alikua amelala kwenye viti vya kuotea jua huku amevaa miwani ya jua......kwa sababu nilikua nayo mengi nikampa moja nikamwambia asome akimaliza nitalipitia, yeye akasistize nisubiri alikua anapitia headings tu...wakati nasubiri akaja jamaa ...akanipita na kakikumbo flani hivi...akaenda akakaa pembeni ya yule dada..nikamsalimia Habari za saa hizi kaka... jamaa akapiga kimya wala hata hakuniangalia... yule dada akamgeukia akamuuliza Si unasalimiwa?... jamaa hakumjibu akaendelea kujifuta maji na taulo.... basi mimi nikaondoka yule dada badae akaniletea gazeti langu akaniomba samahani kwa niaba ya jamaa yake akaniambia.. Msamehe bure tu kaka yangu wanaume wengine wana mambo ya kizamani sana.