Unapomsikia Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mstaafu Ole Sabaya akidai kesi yake ni "ya Kutengenezwa" unajifunza nini?

MATAGA wenzako wanaomba commercial break waburudishe watu kidogo hapa😁😁😁
 
Jana nilishtuka baada ya kumsikia aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai na Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama wa eneo hilo akidai kuwa kesi yake ya Uhujumu uchumi ni ya "Kutengeneza"...
Naona unajihami,kama ulishirikiana nae jiandae kisaikolojia.

Kama na yeye aliwatengenezea wenzake ngoja nae atengenezewe afu ale mvua za kutosha ndio mtapata akili.

Hata shetani ana watetezi.
 
Ye mwenyewe mbona aliwatengenezea wengi mikesi...
Muosha huowoshwa
Mchimba kaburi kaingia mwenyewe shimoni

Hiyo kawaida tu hutokea kwenye mifumo ya kiutawala,

Atulie tu akomae tu na kesi yake

Ova
Kwahiyo ni halali mtu yoyote kutengenezewa kesi?!
 
N vile hakuna wa kumsemea bwana ole sabaya

Angekuwa mpinzan angepata wa kumsemea...
Ndio wananchi tunataka viongozi wa kariba ya kina mtaka. Ndio walioelimika kwa manufaa ya jamii...Sio kina makonda, sabaya ambao hawajui jamii ilihitaji nini toka utumishi wao.

Wao walijali maisha yao binafsi kwa kumtukuza magu kinafiki nafiki. Kuna mwingine pia alifanyakazi kwa weledi sana kwa wananchi naye ni meck sadiki sijui yu wapi yule baba very wise man
 
*Anaenda garage kwa Morombo na wapambe wake, watu wanamuona.

*Anamtishia Mrosso kumbambikia kesi ya uhujumu uchumi, laasivyo ampe milioni 90 watu wanamsikia.

*Wanaenda mpaka Bank ya crdb pale kwa Morombo jamaa anaingia bank anamletea hela camera zinamuona.

*Anachukua hizo hela, anaenda Dar kununua shangingi la milioni 60, watu wanamuona.

Sasa nini kimetengenezwa hapo... Karma inarudi kumuadhibu. Mtu muovu dunia inamkataa na kumuondoa asiendelee kuumiza watu wa Mungu. Atulie tu. Bado Kuna kesi 4 hazijasikilizwa..huko Kilimanjaro bado kuna kesi kama 70 zinamsubiri
 
Kwahiyo ni halali mtu yoyote kutengenezewa kesi?!
Siyo halali.....

Watu wangapi washalalamika kuhusu mambo kama hayo....

Hata yule mfanyabiShara ntunze si katengenezewa zengwe....

Hiii dunia bwasheh uwanja wa fujo haiwezi kutulia....

Ila ukiishi na watu vizuri utaishia kuishi kwa amani,ukiishi na watu kwa kuwafanyia ubabe
Basi huko badaye huwezi jua

Ova
 
images (58).jpeg

Mtoa mada hebu pitia hapo kama lugha ni tatizo na uzee wote huo sina cha kukusaidia tu ila nikueleze hakuna awamu iliyoongozwa na washamba kama ile ya 5!

Hawakua na exposure pia waliamini matumizi ya ubabe kuliko akili , yaani hata mambo yasiyohitaji uwepo wa polisi wao walikua wanatumia..

Yule jamaa yenu msafara wake wote alikua anatembea na jopo zima la ulinzi kwanini ilhali mlituaminisha anapendwa na wanyonge ambao ndio wengi ?
 
Jana nilishtuka baada ya kumsikia aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai na Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama wa eneo hilo akidai kuwa kesi yake ya Uhujumu uchumi ni ya "Kutengeneza"

Nabaki najiuliza kumbe kuna kesi halisi na kesi za Kutengeneza?

Kwa wadhifa aliokuwa nao Ole Sabaya serikalini najikuta nalazimika kumuamini.

Kama Ole Sabaya anaweza kutengenezewa kesi inakuwaje kwa wapinzani kama akina Freeman, Sugu na hata yule Dude wa Songwe?

Dunia inaenda kasi sana kuelekea mwisho wake.

Maendeleo hayana vyama!
Kama yeye alikuwa bingwa wa kuchonga kesi unatarajia nini?
 
Back
Top Bottom