Unampenda lakini hakupendi

Unampenda lakini hakupendi

Hata kama amerudia hii haiwezi kuunganishwa na ya mwanzoni kwani moderator wako bize kuziondoa au kuziunganisha thread za kisiasa na zinazokosoa utawala
 
Ukiona anakufanyia hivyo mwache fastaa aisee hakufai huyo, hiyo ndio tabia yake halisi
 
Habari wana JF,

Umemtumia mtu text lakini hajakujibu, meseji imepokelewa lakini hajajihangaisha kukujibu. Ukaamua kuiweka simu pembeni kuendelea na mambo mengine baadae unarudi bado unaona kimya hajakujibu.

Lakini ukitizama WhatsApp unaona yuko online busy akichati na kubadili DP na status. Unabaki ukijiuliza ana chat na nani mpaka asizione meseji zako na kuzijibu? Unabaki ukiendelea kujiuliza umemkosea nini?

Unaanza kujiambia kuwa labda amekuchoka. Inauma sana kupuuzwa na mtu umpendae kwa moyo wote. Je unajua kuna uwezekano nae anapitia kipindi kigumu kama hicho? Sawa anaweza akakwambia anakupenda au amekumiss, lakini anae mtu mwingine ambae anampenda haswa.

Unavyohangaika kumpigia, kumtumia meseji na asizijibu nae aweza kuwa anafanyiwa hivyo na ampendae. Anamtumia meseji, anamcall lakini nae simu zake hazipokelewi kama wewe. Nao wanapitia magumu kama wewe!

Kufikia hatua hii, unafikiri kukata tamaa juu ya huyo mtu lakini inakuwa sio rahisi. Unafikiri kumuacha huyo mtu, kumblock hata kum "unfriend" Fb lakini bado unaona moyo wako bado unampenda. Na unamatumaini ipo siku atarudi.

Kila muda unapotaka kuichukua simu yako unaomba Mungu ukute meseji yake lakini ukishika tu simu unakuta meseji ya TIGO wakikukumbusha kulipa deni ulilokopa kwa ajili ya muda wa maongezi.

Unajikuta unaichukia simu yako na unamchukia kila mtu anaye kuongelesha, unatamani uipasue simu vipande vipande. Lakini kwanini ifikie hatua hiyo? Kwa hali kama hiyo inaonesha kabisa wewe hupendwi labisa. Kwanini upoteze muda wako kumpenda mtu asiyekupenda?

Usimlazimishe akupende, wewe sio mzee kiasi kwamba huwezi kupata mtu mwingine. Usijipe stress kwa asiyekupenda kuwa na ujasiri wa kumuacha aende na wewe enenda na maisha yako.

Hata iwe vipi maisha lazima yaendelee.
Umegusa asilimia 99.8 ya jf member w humuu
 
kuwa ignored hta na hayo mapenz yatapungua km sio kuisha kabisa. I think i have too much pride or a big ego
 
Nimewahi kupenda sana na kupendwa mno, nadhani haya mawili yamenipa uzoefu mkubwa sana kimaisha maana kunyanyasika kimapenzi kwa kuwa nampenda mtu, huwa siwezi, hata nikijitahidi vipi kuwa zuzu,nilishashindwa, huwa nazinduka haraka sana mpaka mimi mwenyewe nakereka. Namic yale mapenzi ya upofu, kujiachia kama taahira hivi na kumkabidhi mpenzi moyo wote, wallet na ubongo wote lakini siwezi kabisa.
 
Nimewahi kupenda sana na kupendwa mno, nadhani haya mawili yamenipa uzoefu mkubwa sana kimaisha maana kunyanyasika kimapenzi kwa kuwa nampenda mtu, huwa siwezi, hata nikijitahidi vipi kuwa zuzu,nilishashindwa, huwa nazinduka haraka sana mpaka mimi mwenyewe nakereka. Namic yale mapenzi ya upofu, kujiachia kama taahira hivi na kumkabidhi mpenzi moyo wote, wallet na ubongo wote lakini siwezi kabisa.
Pole sanaaa//...
 
Hivi kweli mtu hujui kama hupendwi mpk ufanyiwe vituko au ndo love is blind, mpotezee na ww siku akiona umuhimu wako atakutafuta tu
Hahahaha
Unajua , sku nyingine humtafuti hata sku mbili ila baadaye we mwenyewe una anza kujichekesha, kwa kweli ukimpenda mtu asiye kupenda ni sawa na kuwa na sindano za masaa.
*ulisha wahi kukutana na mtu the best word unapenda kumwambia is i love you, lakini kwake ni the last word she/he will want you to say!!!?

Hahahaha worst experience kwenye love ndio hiyo
 
Hahahaha
Unajua , sku nyingine humtafuti hata sku mbili ila baadaye we mwenyewe una anza kujichekesha, kwa kweli ukimpenda mtu asiye kupenda ni sawa na kuwa na sindano za masaa.
*ulisha wahi kukutana na mtu the best wey you can say to him/her is i love you, lakini kwake ni the last word she will want you to say!!!?

Hahahaha worst experience kwenye love ndio hiyo
ntakupenda sawa lkn nikiona kila siku mm wa kuanza salaam apana kwakweli na mm nachuna najua ntakua naumia sana sbbu nakupenda sana lkn sina jinsi ntazoea tu mpk nakuja kukuona wa kawaida alaf ww sasa ndo unaludi kwa kasi
 
Hahahaha
Unajua , sku nyingine humtafuti hata sku mbili ila baadaye we mwenyewe una anza kujichekesha, kwa kweli ukimpenda mtu asiye kupenda ni sawa na kuwa na sindano za masaa.
*ulisha wahi kukutana na mtu the best word unapenda kumwambia is i love you, lakini kwake ni the last word she/he will want you to say!!!?

Hahahaha worst experience kwenye love ndio hiyo
Nomaaa sana
 
ntakupenda sawa lkn nikiona kila siku mm wa kuanza salaam apana kwakweli na mm nachuna najua ntakua naumia sana sbbu nakupenda sana lkn sina jinsi ntazoea tu mpk nakuja kukuona wa kawaida alaf ww sasa ndo unaludi kwa kasi
Hahaha
Haiwagi that simple shunie , katika vitu niliwahi kujifunza ila kwa taabu ni hiyo kitu
Mtu yaan unampenda mpaka unahisi umerogwa, halafu ukimuangalia yuko na wewe kwa sababu flani tuu, ila yuko disgusted yaan kuwa na wewe
Shidaaaaa!!
 
Back
Top Bottom