Unakumbuka nini katika enzi za gazeti la Sani?

Jarida la enzi ya wahenga hahaha siku hizi wanaita zilipendwa...niliona baadhi kwenye app ya m paper unalipia jero sijui buku??
 
IMG-20170904-WA0033.jpg

IMG-20170904-WA0025.jpg

IMG-20170904-WA0032.jpg

IMG-20170904-WA0031.jpg

IMG-20170904-WA0030.jpg

IMG-20170904-WA0029.jpg

IMG-20170904-WA0028.jpg

IMG-20170904-WA0027.jpg

IMG-20170904-WA0026.jpg

IMG-20170904-WA0025.jpg


Unakumbuka nini ,wapi Mhenga mwenzangu?

Na sijui hili gazeti lilipoteleaga wapi.
 
mtaani kuna jamaa alitushika masikio eti hao jamaa kuna nchi dunia hii walikuwa wanaishi
 
Hii ni Nakala ya gazeti la Sani la mwaka 1986 mwishoni kuelekea 1987 na kipindi hicho likiuzwa kwa shilingi 30 na Watanzania wakiburudika kwa katuni, hadithi, riwaya nk.

Wewe ulikuwa wapi kipindi hicho?

Tupe Taswira ya Taifa kipindi hicho (hata kama ulikuwa hujazaliwa ila umesoma au kuhadithiwa) katika nyanja za Elimu, Michezo, Burudani, Siasa nk.


Eleza kuhusu usafiri wa aina mbali mbali uliotumika miaka hiyo au hata kuweka picha zake.

Eleza kuhusu mavazi pendwa ya miaka hiyo na kila unachokijua kilitumia miaka hiyo na watu wa sasa hawavijui.

Lengo la uzi huu ni kukumbushana mambo ya miaka hiyo katika Taifa letu kwani wengine hawakupata fursa ya kuwepo miaka hiyo hivyo ni burudani tosha.

Picha ni muhimu sana....twende kazi.
IMG_20191105_092440_811.jpeg
 
Nilikuwepo, japo nilikuwa dogo lakini nilijua kusoma na kuandika. Hili toleo lilikuwa linatoka mara 1 kwa mwezi mara mbili kama sikosei.

Nilikuwa moshi ambapo ndio kwetu. Nakumbuka kipindi hiko mabasi ya town trip kcmc, kiboriloni yalikuwa ni SHIMAWIMO. Yaani (SHIrika la MAendeleo WIlaya ya MOshi)

Kumbi za cinema zilikuwa mbili. ABC na Plaza Cinema. Nilikuwa sikosi kwenda pale plaza kila jumapili saa nne kuangalia sinema. Hata kama sijapewa hela na mshua lazima niende ongalao niambulie fungulia mbwa.

Masteling wa wakati huo, Amitha Batchan, Mithuny Chakraborty, Rish Kopoor,Rajesh Kumar, Denzolpa, kwa upande wa kina mama walikuwepo kina Jaya, Hemma Malini, nk.

Movie nazozikumbika, Nasseb,Amne Samne, nk. Kotambo sana.

Kumbi za disco zilikuwa ni Vijana club, Libert hotel iliyokuwa karibu na green view ambayo ilikuja kuungua baadae.

Mafuta ya kupaka wakati huo ni YOU na YOLANDA yaliyokuwa kwenye mkebe. Mengine ni rays, Ashanti. Wajanja walikuwa wanavaa jenzi na rabber mtoni kama Ascot. Suruali za kitambaa zilikuwa Cacha rell, Mr Dio nk.

Wahusika wa kuu kwenye kazeti la Sani. Kipepe, Lodi lofa, Sokomoka, Pimbi, Madenge,na Yule mpiga roba nani sijui nimemsahau.

Mc Sukununu.

Hadithi zilizowahi kutamba wakati huo kwenye gazeti la sani na mtunzi akiwa marehemu Hammie Rajab ni pamoja na Pumbazo La moyo, Usiku waGiza ya Joyce na Dalanda na kibibi Gula.

Dah muda umeenda aisee, ila kama juzi tu.
 
Nilikuwepo, japo nilikuwa dogo lakini nilijua kusoma na kuandika. Hili toleo lilikuwa linatoka mara 1 kwa mwezi mara mbili kama sikosei.

Nilikuwa moshi ambapo ndio kwetu. Nakumbuka kipindi hiko mabasi ya town trip kcmc, kiboriloni yalikuwa ni SHIMAWIMO. Yaani (SHIrika la MAendeleo WIlaya ya MOshi)

Kumbi za cinema zilikuwa mbili. ABC na Plaza Cinema. Nilikuwa sikosi kwenda pale plaza kila jumapili saa nne kuangalia sinema. Hata kama sijapewa hela na mshua lazima niende ongalao niambulie fungulia mbwa.

Masteling wa wakati huo, Amitha Batchan, Mithuny Chakraborty, Rish Kopoor,Rajesh Kumar, Denzolpa, kwa upande wa kina mama walikuwepo kina Jaya, Hemma Malini, nk.

Movie nazozikumbika, Nasseb,Amne Samne, nk. Kotambo sana.

Kumbi za disco zilikuwa ni Vijana club, Libert hotel iliyokuwa karibu na green view ambayo ilikuja kuungua baadae.

Mafuta ya kupaka wakati huo ni YOU na YOLANDA yaliyokuwa kwenye mkebe. Mengine ni rays, Ashanti. Wajanja walikuwa wanavaa jenzi na rabber mtoni kama Ascot. Suruali za kitambaa zilikuwa Cacha rell, Mr Dio nk.

Wahusika wa kuu kwenye kazeti la Sani. Kipepe, Lodi lofa, Sokomoka, Pimbi, Madenge,na Yule mpiga roba nani sijui nimemsahau.

Mc Sukununu.

Hadithi zilizowahi kutamba wakati huo kwenye gazeti la sani na mtunzi akiwa marehemu Hammie Rajab ni pamoja na Pumbazo La moyo, Usiku waGiza ya Joyce na Dalanda na kibibi Gula.

Dah muda umeenda aisee, ila kama juzi tu.
Dah! Hongera mkuu...hakika miaka hiyo dunia ilikuwa na raha zake.
 
Back
Top Bottom