Unajua kampuni zisizolipa NSSF? Dili hiyo!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,150
Kama unajua kampuni ambyo ailipi pesa za wafanyakazi wake nssf weka hapa na aandika anwani yako upate donge nono kutoka kampuni ya NSSF.ni PM ni kupe line!!!kazi kwenu!!ukiogopa kuweka adress pm m
 
toa hapa majina ya kampuni na wakurugenzi wao

mfano halisi

KAMPUNI.... WAKURUGENZI

TOMMYSPADES THOMAS LYIMO

HABARICORPORATION .......................................??

GO ON!!
 
Si lazima kujiunga NSSF, unaweza kujiunga pia PPF. NSSF hilo donge nono wanalitoaje na watafaidika vp? Nashindwa kuelewa kwa nini PPF nao wasitoe donge nono. Maana mtu anaweza kuripotiwa NSSF akalipa say fine kwa mujibu wa sheria halafu akapeleka wafanyakazi wake PPF.
 
Kuna kampuni inaitwa Highway Carriers ya Azim Dewji na nduguze, ilikuwa inahusika na mambo ya Freight and Carco clearance na Transporatation.

Babangu kafanya kazi hapo kwa karibu 10 siku alipoamua kuacha kazi niliamua kwenda NSF kuulizia mafao yake nikakuta Highway hawalipi NSSF na wapo Dar. Mzee akaamua kususa hata mafao yake ya zamani ya NSSF (PPF) maana tangu 1967 hadi 1986 akiba zilikuwa 400,000/- (Laki nne) sasa hao NSSF wenyewe wanatuibia kwa kutoangalia thamani ya pesa ambayo babangu alianza kuweka miaka ya 1960 mshahara ukiwa shilingi 10 na hadi mwaka 1986 ana 400,000/- (pamoja na faida), kama si mzaha ni nini?

NSSF sidhani kama wataweza kutusaidia dhidi ya wizi wa Waajiri wetu. Mfano mdogo tu, mimi nina akiba ya NSSF shs 8,000,000/- hadi June 2006 na nikakuta faida walonipa ni shs 6,000/- tu. Sasa sio wizi huo? Mapesa yetu wanapeleka wapi au ndo hizo Serikali yajichotea tu kwenye chaguzi?
Ok, pamoja na hayo nimekupa Jina la Mwajiri ambaye hapeleki michango ya Wananchama tangu 1987 hadi 1996. nasubiri bingo yangu.
 
nnnhhh!!nzozo wa mizozo !!!washaondoka kazi kwako@#####
 
jamani kuna makampuni ambayo hayajawaandikisha wafanyakazi wake kwenye mfuko wowote ule wa pensheni, hawa wanafanywaje? makampuni yapo miaka mingi lakini hakuna hata mfanyakazi mmoja anayepata mafao wakati wa kustaafu au hata kusimamishwa kazi.

Hawa wanapelekwa wapi ili wajue wanatakiwa kujiunga na hii mifuko? Wako wengi ambao wanawaumiza ndugu zetu na marafiki zetu kwa muda mrefu sasa ninataka niwatolee usongo. Maelekezo tafadhali.
 
suala la kujua au kutokujua ni la mwajili...wewe mwajiliwa huwezi jua kama pesa yako inapelekwa au la mpaka siku umestaafu na unafuatilia mafao yako...hiyo ni kazi ya nssf kufuatilia kwenye database zao pamoja na za msajiri wa makampuni ili kujua tanzania kuna makampuni mangapi mpaka sasa na ni mangapi hayapeleki makato ya wafanyakazi wao......kazi rahisiiiii kwao kama wasipoingiza na UFISADI....ni hayo tu..!
 
suala la kujua au kutokujua ni la mwajili...wewe mwajiliwa huwezi jua kama pesa yako inapelekwa au la mpaka siku umestaafu na unafuatilia mafao yako...hiyo ni kazi ya nssf kufuatilia kwenye database zao pamoja na za msajiri wa makampuni ili kujua tanzania kuna makampuni mangapi mpaka sasa na ni mangapi hayapeleki makato ya wafanyakazi wao......kazi rahisiiiii kwao kama wasipoingiza na UFISADI....ni hayo tu..!

MKUU MTIMTI MFANYAKAZI ANAYO HAKI YA KUJUA AMA PESA ZAKE ZINAPELEKWA KWENYE MIFUKO YA PENSION AMA LAH!!!!!
 
suala la kujua au kutokujua ni la mwajili...wewe mwajiliwa huwezi jua kama pesa yako inapelekwa au la mpaka siku umestaafu na unafuatilia mafao yako...hiyo ni kazi ya nssf kufuatilia kwenye database zao pamoja na za msajiri wa makampuni ili kujua tanzania kuna makampuni mangapi mpaka sasa na ni mangapi hayapeleki makato ya wafanyakazi wao......kazi rahisiiiii kwao kama wasipoingiza na UFISADI....ni hayo tu..!

We mkubwa ...pole inaonekana hujui hii mifuko ya Pension inafanya kazi vipi! Aliyekwambia suala la kujua au kutokujua kama pesa ya NSSF /PPF/PSPF etc inawasilishwa au la ni ya mwajili ni nani? Kwani hiyo ni hela ya mwajiri?

Kijana kama hiyo ni hela yako kitu unachotakiwa kufanya 1. Ukipokea mshahara lazima upewe salary slip...humo pamoja na vitu vingine huonyeshwa makato katika mwezi husika (kwa kuorodhesha) ikiwepo michango ya NSSF etc, hivyo kwa kuangalia hiyo slip, unaweza ukahakikisha kama michango hiyo imekatwa au la!

2. Kila mwisho wa mwaka (Fiscal Year) NSSF kwa mfano huandaa report ya michango ya wanachama wao...hivyo huwa ni jukumu lako kwenda na ID yako kwenye ofisi zao na wanakuprintia statement ya michango yako tangia ulipo anza kuchangia. So kama mwajiri hapeleki michango huko, huwezi pewa hiyo statement!

Na dhani umenipata vilivyo!
 
Wewe mwana JM suala la kujua kama mwajiri wako anapeleka miochango yako kwenye hz taasisi za fedha either NSSF,PPF au zinginezo bado ni la kwako. Manke mwisho wa utendaji wako huna budi kupokea fedha yako iliyokuwa imeifadhiwa na mifuko hii na ka faida kadogo
Manake mwajiri anakuchangia sehemu fulani na we sehemu fulani, nadhani nusu kwa nusu.
 
Back
Top Bottom