Prakatatumba abaabaabaa
JF-Expert Member
- Aug 2, 2022
- 1,476
- 4,714
Mkuu ilo jambo lilinipa stress tukaenda na wenzangu pale ngome tukaishia kufukuzwa.Acha tu maisha hayana formula ni Afande ila kiumri very young,kila mtu na bahati yake hapa duniani.
Lazima usjisikie vibaya lakini mgawaji ni Mungu na hugawa kwa kadri inavyompendeza mwenyewe!Habari za Jumapili wanajukwaa,Pia poleni na majukumu ya kutafuta mkate wa kila siku.Niende kwenye mada husika hapo juu hivi huwa unajisikiaje hasa pale unapokutana na rafiki zako mliosoma wote kipindi hicho wako mbali sana kimaisha kuliko wewe?
Kwa Upande wangu hii imenikuta wakati natoka Kanisani na stress nyingi zimejaa kwenye kichwa ghafla napigiwa honi na Gari nyeusi aina ya BMW X5 nikashituka kuona linapaki pembeni na Mtu anashuka ananiita jina langu la Ukoo! Nikamkubuka ni rafiki yangu tuliyesoma wote.
Advance Level ila yeye Alibahatika baada ya kutoka mujibu wa sheria alijiunga na Taasisi nyeti, hapa nchini kwa sasa ni Afisa mkubwa.
Kwa upande wangu akaniuliza "ndugu kwa sasa unapiga mishe gani?", ikabidi niwe muwazi nikamwambia kwangu bado mambo hayajakaa sawa japo,nilijisikia Aibu kidogo yaani niliyekuwa nampita class,namfundisha kila siku,tunakesha wote kwenye madesa kashanizidi ilihali mimi bado sioni mwanga.
Nikajisemea Moyoni "basi mpaka pale zamu yangu itakapo fika niendele kuwapigia wenzangu makofi kwa tabasamu na upendo."
Nashukuru akanipa lift mpaka home maana nilikuwa sijawahi panda hizi BMW aisee kuna utofauti mkubwa sana na hizi IST. Naishia hapo wakuu Mungu atubariki sote Jumapili njema.
Ilo jambo huwa ni uongo Sana, sasa kwanini Mungu asimgawie na yeye? Kwahiyo Mungu yupo selective?Lazima usjisikie vibaya lakini mgawaji ni Mungu na hugawa kwa kadri inavyompendeza mwenyewe!
Basi mwanangu ndo alikuwa na bahati hioMkuu ilo jambo lilinipa stress tukaenda na wenzangu pale ngome tukaishia kufukuzwa.
Hiko hivi tulivyoenda kwa mujibu wa sheria walifanya usahili kambi tatu, sisi hawakufikia kambi yetu.
Tulivyoenda chuo wakapigiwa simu wakaacha chuo wakarudi jeshini wengine walipelekwa navy, urusi egpty n.k wapo mbali kiukweli na wanamiliki magari mazuri tu.
Na wengi tulipiga nao PCB matokeo yalikua yanafanana. Mimi nimeajiriwa vijijini huku.
Kuna watu wana bahati sana
Haya mambo ukiyafikiria negative sana utaishia kukufuru kikubwa.Thank God for the life na endelea kuwapigia wenzio makofi kwa upendo mkubwa mpaka zamu yako itakapofikaIlo jambo huwa ni uongo Sana, sasa kwanini Mungu asimgawie na yeye? Kwahiyo Mungu yupo selective?
Maneno ya mwisho yenye herufi kubwa, ukisoma Biblia ya kiingereza ni tofauti kidogo. Huo mstari unasema, "Bad luck happens to everyone"Mhu 9:11 SUV
Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; LAKINI WAKATI NA BAHATI HUWAPATA WOTE.
Kikubwa tusikate tamaa,japo I know what you feel wazungu wanasema life is a journey not a competition.Mim ni mmoja ya watu ambao marafiki zao zaid ya 80% wamepiga atua kubwa sana kimaisha, sio marafiki niliokuwa nao yaan childhood friends, Primary, secondary na chuo. most of them ni matajiri na bado ni machalii kabisa, maisha aya sio poa
wengine adi wanamiliki magari mawili mawili na minengo ya kibabe kabisa na biashara kubwa. life's not fair aisee
Kule pia nipo active mkuu, nabadili ladha ya mbogaKaka,nimekuona Twitani Ieo ume comment
Sasa kumbe ulikua unamuomgoza darasani πππYaan hadi mood na kazi huwa inakata kabisa,kibaya zaidi unakuta ni yule ambae darasani ulikuwa unamzidi
Pamoja Sana ndugu yanguKule pia nipo active mkuu, nabadili ladha ya mboga
Huu mstari kila ninapousoma unanikumbusha kisa cha mwanariadha mkongwe wa Tanzania John Stephen Akwari kilichotokea mwaka 1968 Mpaka akapachikwa jina 'The Champion who finished last'Mhu 9:11 SUV
Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; LAKINI WAKATI NA BAHATI HUWAPATA WOTE.