Unaikumbuka hii siku ya kwanza..??

Unaikumbuka hii siku ya kwanza..??

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,914
Kwa wale ambao wapo kwenye uhusiano iwe wa kimapenzi au ndoa wana kumbukumbu ya ile siku ya kwanza ambayo walianza kuonana na mmmoja wao kuanza kumsemesha mwwenzake [mara nyingi ni wanaume] na hatimae kuwepo kwenye uhusiano waliopo leo

Leo nairudusha dunia nyuma hadi siku hiyooooooooooo.....!!!!!!!!!!

images


Leo siyo vibaya ukakumbusha ile siku yenu ya kwanza kuonana au kukutana
Je unakumbuka ilikuwa wapi?
Je unakumbuka siku jamaa alipoingiza "vesi"
Unakumbuka siku ulipoanza kumfukuzia?

Vip unajisikiaje?


images

Alipokuambia lengo lake ulijisikiaje?
Moyo ulikufa ganzi au??


images

Leo mko pamoja hebu shea nasi namna jamaa alivyoteseka hadi kukupata
Hebu shea nasi jinsi kijana ulivyosota hadi kumpata


images

Unakumbuka siku ya mtoko wenu wa kwanza?
Hebu tuambie namna ulivyojisikia siku hiyo
Ilikuwa Heaven on Earth au siyo

Hebu jipongezeni bana

images

Unaikumbuka siku hii ya kwanza??
Ulijisikiaje??

Huu ni wakati wako kushea nasi nyakati hizi murua kabisa kwenye maisha yako na ni wakati wa kujipongeza pia
Hongereni sana na mpendane milele....!

Kwetu sisi tulio single tuumie tu hapa ....lol!!!!!!!!!
 
Last edited by a moderator:
He he he, ilikuwa kanisani, and was just a teenager, hanijui simjui . . . .

For him, it was love at first sight, kwangu it was love at 'zombie' sight (hadi nlipogundua ni zombie wangu ndo nkampenda).

Alikuwa anatetemeka sana, sijui hata alisema nini, ila alikuwa anahangaika tu midomo inacheza cheza.

Out ya kwanza nayoikumbuka ilikuwa kwao, mama ake akanipikia msosi mtamu huo.
 
hahahaaaaa nani anaifahamu View Point Lushoto? mmmhh tulikua juu milimani tukiwa tunaitizama Mombo kule inakopita Barabara ya Arusha, unaangalia hadi Mazinde kuleee, kuna upepo balaaaa......Nilitoroka Shule nilikua nasoma High school Moja Tanga Mjini..... kama umeshasafiri kwenda Arusha ukipita Mombo ile milima kule juu unayoiona ndio tulikokuwa huko. Hahahaaaa Ilikua raha hadi basi nakumbuka tulikaa mahali kulikua na kiji-stream cha maji ya baridiiii, masafi kidume nimebeba juice na biskuti. MMMHHHH jamani nyie jamani jamani acha kabisa na appointment zetu ilikua kama vile wachawi yaani tukiachana leo tukisema tutaonana next week kwa mfano muda fulani, lazima itakua hivyo, muda ule ule saaa ile ile mahali pale pale unakula kona ya kwanza ya pili unamuona mupenzi huyoooooo.

Juzi kati nilienda Lushoto ikabidi nifike kule juuu, nusura machozi yanitoke, tumeshakuwa wakubwa saa hizi na watoto....aaaghh
 
Mie nilimuona kwenye Sherehe,waliishi karibu na my Best friend siku ya sherehe akaniambia huyu mkaka anaringa sana
mie nikamponda sana nikasema girlfriend wake ana shida sana mi siwezi kutoka na mkaka kama huyu hataa
kwanza anaonekana kama PLAYBOY tu..lakin rohoni nilimsifia He was such a GENTLEMAN for real

kuna siku akanikuta kwenye mgahawa fulani tunakula na my friend alikuwa ye na rafiki yake mara ya kwanza
walitupita walivopita tu tukaanza kuwasema hamad hao wakarudi wakatusalimia ka dk 2 then wakasepa...........
baadae akaniambia pale ndio ilikuwa first time kuniona na pale ndio moyo wake ulinidondokea

hakuwahi kunitongoza directly tulizoeana tukajikuta tunafall in LOVE tumepita mengi lakin we are still together

rafiki zangu hadi leo huwa wananicheka sana na kurecall yale maneno yangu niliosemaga kwenye ile sherehe
 
Mimi alinipigia simu kuniita kwenye interview...nilipofika tukachelewa kidogo kuanza interview so nikawa ofisini kwake...dah nilipotoka nikakuta kaacha kimemo kwenye bag langu nimtafute jioni....
 
hahahaaaa ina maana mpaka leo unampa mambo? ayayayayaaaaa roho inaumaje? hua nikiona comment zako hua najifarijikuwa Mpwa wangu huwa havuliwi nguo, kumbe kuna RIJAMAA RINAMTENGENEZA dada yangu bhana.....nisalimie kwake
Mie nilimuona kwenye Sherehe,waliishi karibu na my Best friend siku ya sherehe akaniambia huyu mkaka anaringa sana
mie nikamponda sana nikasema girlfriend wake ana shida sana mi siwezi kutoka na mkaka kama huyu hataa
kwanza anaonekana kama PLAYBOY tu..lakin rohoni nilimsifia He was such a GENTLEMAN for real

kuna siku akanikuta kwenye mgahawa fulani tunakula na my friend alikuwa ye na rafiki yake mara ya kwanza
walitupita walivopita tu tukaanza kuwasema hamad hao wakarudi wakatusalimia ka dk 2 then wakasepa...........
baadae akaniambia pale ndio ilikuwa first time kuniona na pale ndio moyo wake ulinidondokea

hakuwahi kunitongoza directly tulizoeana tukajikuta tunafall in LOVE tumepita mengi lakin we are still together

rafiki zangu hadi leo huwa wananicheka sana na kurecall yale maneno yangu niliosemaga kwenye ile sherehe
 
Mmmh!!

Sredi yako imefanya nikumbuke kibao cha huyu kijana wa miziki ya Bongo Flavor...kile cha Inaniuma Sana by Juma Nature
 
Kumbe kifulambeta ni wa kike?noumaa kweli.

Pingu niombe radhi...mi dume bwn sema alikolea na mimi tangu siku aliponipigia simu..alikuwa ni secretary kampuni flani hapa Arusha...so tulikutana kwa style hiyo na mpaka sasa tupo nae na kid tayari
 
^^
Sitaki hata kukumbuka chochote! Mwisho wa safari uliharibu uzuri wa mwanzo wake!
Ngoja nisome Best Memories za wenzangu
^^

Pole sana mkuu...!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom