Iran ni mtoto wa mjini kwenye masuala ya proxy wars. Yeye anajua kabisa kutuma vijana waliolishwa sumu ya jihad na hii ni rahisi sana kwa Waarabu kufanya hivo maana tumeona hata jana Turkey inakusanya vijana kutoka Syria kwenda kupigana Libya kwa malipo ya kati ya 200 -1500 USD. U.S wenyewe wamekiri kuwa Qurds ndo walikuwa wanafundisha vikosi vya magaidi kutengeneza IEDs na zimeua jumla ya mamia ya wanajeshi.
Pia ikumbukwe Hezbollah na Hamas wana uhusiano mzuri na Iran na ndo inawapa uwezo wa kutengeneza maroketi ya kisasa ambayo yako reserve, sio haya yanayorushwa Israel na kutunguliwa na Iron Dome.
Kule Yemen, Houthi wamepata teknolojia ya kuwapiga Saudi Arabia hasa kwa maroketi kutoka Iran. Kingine ndo inarudi suala la balozi za U.S na watu wake sehemu mbalimbali duniani ambao wanaweza kuwa target. Haya yote Iran akiyafanya atakana kabisa, hawa sio al-Qaeda wanaofanya kitu wakajimwambafai.
Kwa U.S huwa hawapendi kupoteza idadi kubwa ya wanajeshi kama ilivyotokea kule Vietnam au Korea peninsula. Na pia hapendi lawama kutoka kwa wazungu kwani vita itapandisha bei ya mafuta na uchumi uwe mgumu.
Hivo anaweza tafuta coalition ili kugawana lawama au kufanya proxy war, aite vijana wa-Sunni awape training na silaha waende kupigana na Iran. Chochote kitakachotokea uchumi utayumba maana Iran ni wehu wanaweza fanya ile tukose wote wakaharibu biashara pale Hormuz strait na pipeline za mafuta. Mawazo yangu tu.