Major, karibu migogoro yote inayotokea nchi za kiarabu imetengenezwa na nchi za Ulaya ikiongozwa na Marekani. Ukianzia Libya, Syria, Iraq, Afghanistani, Pakistan, Egypt, Yemen na kwingineko. Ikifahamika wazi kwamba migogoro hii italeta shida kubwa sana...shida ya wakimbizi kwenye nchi jirani kama Saudi Arabia, Lebanon, Jordan, Qatar, na UAE.
Hii maana yake ni kwamba,wakati shida itakapozikumba nchi walizofanikiwa kuchochea mapigano basi hata nchi jirani zilizo na utulivu zitaonja adha ya shida ya wakimbizi kutoka nchi zote zilizochafuka.
Katika hali kama hiyo, hakuna nchi itakayokuwa na ahueni na mkakati wa nchi za Ulaya na Marekani utakuwa umetimia.
Nadhani wakimbizi hawa sasa wamefikiri vema, badala ya kuzisumbua nchi jirani, waislam wenzao na waarabu wenzao, wameona njia bora ni kuwafuata hukohuko Ulaya bila kujali safari hizo zinawagharimu kiasi gani. Hii ni kuzifanya nchi wachochezi nao wavune wanachokipanda, wapokee adha ya wakimbizi ambao kiukweli ni mzigo mkubwa sana unaozielemea nchi za mashariki.
Hii ndio sababu kwanini wakimbizi hawa wamechagua kwenda Ulaya na si Saudi Arabia japokuwa ipo idadi kubwa tu ya wakimbizi nchini Uturuki, Lebanon, Jordan na Libya kiasi.
Binafsi nawapongeza na kuwaunga mkono kwamba kadri Marekani na Ulaya wanapojitajidi kutengeneza na kuchochea machafuko nchini mwao basi na wao wajitahidi kukimbilia Ulaya mamia kwa maelfu halafu baada ya miaka 10-20 tuone matokeo.