mafimboo
JF-Expert Member
- Oct 9, 2014
- 2,415
- 976
Tanzania bado ni nchi ya kusikitisha duniani ,inatia huruma ,tatizo kubwa la tanzania ni kuwa na wanasiasa sehemu ambazo zinahitaji wataalamu mathalani kama TCU,katika tangazao lao la kupandisha viwango vya ufaulu kuingia vyuo vikuu linaonekana kujaa siasa na ubabe na kuwalenga zaidi watoto wa shule za kata na watoto wa masikini wanaosoma kwenye shule zisizo na ubora tangazo linasomeka kifupi
1;'kutokana na wadau kulalamika kuwa wasomi wa sasa hawana ushindani (wabovu)kwenye soko la ajira'
2;vyuo vya kati vinakosa wanafunzi kwa sababu wengi wanakimbilia vyuo vikuu
sababu hizi ni dhaifu na fedhea kwa taasisi kubwa kama TCU
Mosi TCU haijawahi kukusanya maoni kuhusu ubora wa elimu ya vyuo vikuu,kama iliwahi kukusanya iwataje wadau waliotoa maoni ikiwemo vyuo vikuu husika pamoja na shule ,TCU inatakiwa ituambie sababu zilizotumika mwaka 2010 kupunguza viwango vya kuingilia vyuo vikuu,na kwanini watoe sababu hizo kipindi cha serikali mpya,walishindwa nini kuzitoa kipindi cha Jakaya
Pili vyuo vya kati kukosa wanafunzi inatokana na diploma zinazotolewa kukosa ubora na kutokujitosheleza kwenye soko la ajira ndio maana inakimbiwa elimu ya shahada ndio inayojitosheleza kidogo kwenye ajira
kitendo cha kupunguza idadi ya wasomi wa degree ni ajenda ya siri ya serikali ya awamu ya tano labla inalenga kuua baadhi ya vyuo ama kupunguza wasomi wa elimu ya juu,katika nchi yenye wakazi zaidi ya milioni 52.unadiriki kupunguza wasomi ni kuharibu taifa;
TCU imeshindwa kutambua kuwa elimu ni haki ya kimsingi ya mwananchi bila kumuwekea vikwanzo vya kisiasa ikifahamika wazi kuwa serikali shule zake nyingi hasa za kata hazina vigezo ,ikiwemo kukosa walimu,vitabu vya kiada ,madawati ,maabara na madarasa huwezi kutegemea mtoto wa shule ya kata aende chuo kikuu kwa mazingira haya haiwezekani,
Vyuo wataenda watoto wa shule za international za vigogo na matajiri tu wenye shule zilizokamilika na zenye gharama kubwa,na huu ni mwanzo wa kuanzisha na KUIMARISHA ELIMU YA MATABAKA,Kimsingi serikali ya jpm imelenga kuwadhoofisha watoto wa shule za kata kwa kudhamiria,hakuna sababu yoyote ya kuchangia madawati wakati watoto wetu hawatafanikiwa kusoma elimu ya vyuo
1;'kutokana na wadau kulalamika kuwa wasomi wa sasa hawana ushindani (wabovu)kwenye soko la ajira'
2;vyuo vya kati vinakosa wanafunzi kwa sababu wengi wanakimbilia vyuo vikuu
sababu hizi ni dhaifu na fedhea kwa taasisi kubwa kama TCU
Mosi TCU haijawahi kukusanya maoni kuhusu ubora wa elimu ya vyuo vikuu,kama iliwahi kukusanya iwataje wadau waliotoa maoni ikiwemo vyuo vikuu husika pamoja na shule ,TCU inatakiwa ituambie sababu zilizotumika mwaka 2010 kupunguza viwango vya kuingilia vyuo vikuu,na kwanini watoe sababu hizo kipindi cha serikali mpya,walishindwa nini kuzitoa kipindi cha Jakaya
Pili vyuo vya kati kukosa wanafunzi inatokana na diploma zinazotolewa kukosa ubora na kutokujitosheleza kwenye soko la ajira ndio maana inakimbiwa elimu ya shahada ndio inayojitosheleza kidogo kwenye ajira
kitendo cha kupunguza idadi ya wasomi wa degree ni ajenda ya siri ya serikali ya awamu ya tano labla inalenga kuua baadhi ya vyuo ama kupunguza wasomi wa elimu ya juu,katika nchi yenye wakazi zaidi ya milioni 52.unadiriki kupunguza wasomi ni kuharibu taifa;
TCU imeshindwa kutambua kuwa elimu ni haki ya kimsingi ya mwananchi bila kumuwekea vikwanzo vya kisiasa ikifahamika wazi kuwa serikali shule zake nyingi hasa za kata hazina vigezo ,ikiwemo kukosa walimu,vitabu vya kiada ,madawati ,maabara na madarasa huwezi kutegemea mtoto wa shule ya kata aende chuo kikuu kwa mazingira haya haiwezekani,
Vyuo wataenda watoto wa shule za international za vigogo na matajiri tu wenye shule zilizokamilika na zenye gharama kubwa,na huu ni mwanzo wa kuanzisha na KUIMARISHA ELIMU YA MATABAKA,Kimsingi serikali ya jpm imelenga kuwadhoofisha watoto wa shule za kata kwa kudhamiria,hakuna sababu yoyote ya kuchangia madawati wakati watoto wetu hawatafanikiwa kusoma elimu ya vyuo