Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
CCM ni wanafiki, walaghai na waoga!
Hakuna ambaye anaweza kuniambia kuwa nyakati hizi na mambo yanayotokea Tanzania na ndani ya CCM kuwa kilichotokea Dodoma ndani ya CCM wiki iliyopita na kauli zote zilizofuatia si Unafiki, Ulaghai au Woga!
Naomba ni wakumbushe Wana-CCM wanapokuja na kauli zao za kujivua gamba na kwamba sasa wamejizatiti kivitendo kupigana na Uhujumu, Ufisadi, Rushwa na Uzembe, je mlikuwa wapi siku zote wakati Watanzania walipokuwa wakipiga kelele?
Je tuwaamini vipi safari hii, ilhali Mwenyekiti bado ni yule yule aliyefukia mambo mlipokutana Butiama na hata yeye kuwa hapo anatuhumiwa mengi?
KWa nini mlipokutana Butiama, mkijua tuhuma nzito za Ufisadi zikiwa zimekikabili Chama, anzia IPTL, ATCL, TRC, Rada, EPA, Richmond, Buzwagi na rip[oti ya miaka miwili ya CAG, kwa nini hamkuchukua hatua mnazodai kuzichukua leo hii?
Kwa nini hamkuwapa fursa mwaka ule waliotuhumiwa kwa orodha ya Ufisadi na ile barua ya Jeetu Patel wasijivue uongozi wa chama?
Leo hii, mnadai kuwa waliokitia chama madoa ya Ufisadi na Uzembe wanajijua, na mnawaomba, hebo mnawaomba! Kwa nini msiwataje kuwa jamani, wewe, wewe na yule mnatuhuma nyingi, tumetumia TAKUKURU, Polisi na hata makachero wa nje, na mmethibitika Vijisenti vyenu si vya halali!
Mnaoneana nini aibu? Hata kule UVCCM ambapo leo hii tunasikia shangwe kupongeza vijana kushika hatamu, nako ni majungu na shutuma tupu!
Tukubaliane moja, CCM ni waoga kushughulikia jini walilolizalisha ndani na kulitumia kwa manufaa yao. CCm ni Wazandiki na Wanafiki, wanawadanganya Watanzania kuwa wanajisahihisha.
Je mlipokaa chini na kuandika Tujisahihishe, tuwasamehe mara 70 kama Wakristo na mafundisho ya Kristo kugeuza shavu mpaka lini?
Acheni kutulaghai, nyinyi ni Wanafiki na Waoga mnaoogopana kutokana na kutumiana kwa manufaa yenu ya pamoja kama Chama kuihujumu Tanzania!
Hakuna ambaye anaweza kuniambia kuwa nyakati hizi na mambo yanayotokea Tanzania na ndani ya CCM kuwa kilichotokea Dodoma ndani ya CCM wiki iliyopita na kauli zote zilizofuatia si Unafiki, Ulaghai au Woga!
Naomba ni wakumbushe Wana-CCM wanapokuja na kauli zao za kujivua gamba na kwamba sasa wamejizatiti kivitendo kupigana na Uhujumu, Ufisadi, Rushwa na Uzembe, je mlikuwa wapi siku zote wakati Watanzania walipokuwa wakipiga kelele?
Je tuwaamini vipi safari hii, ilhali Mwenyekiti bado ni yule yule aliyefukia mambo mlipokutana Butiama na hata yeye kuwa hapo anatuhumiwa mengi?
KWa nini mlipokutana Butiama, mkijua tuhuma nzito za Ufisadi zikiwa zimekikabili Chama, anzia IPTL, ATCL, TRC, Rada, EPA, Richmond, Buzwagi na rip[oti ya miaka miwili ya CAG, kwa nini hamkuchukua hatua mnazodai kuzichukua leo hii?
Kwa nini hamkuwapa fursa mwaka ule waliotuhumiwa kwa orodha ya Ufisadi na ile barua ya Jeetu Patel wasijivue uongozi wa chama?
Leo hii, mnadai kuwa waliokitia chama madoa ya Ufisadi na Uzembe wanajijua, na mnawaomba, hebo mnawaomba! Kwa nini msiwataje kuwa jamani, wewe, wewe na yule mnatuhuma nyingi, tumetumia TAKUKURU, Polisi na hata makachero wa nje, na mmethibitika Vijisenti vyenu si vya halali!
Mnaoneana nini aibu? Hata kule UVCCM ambapo leo hii tunasikia shangwe kupongeza vijana kushika hatamu, nako ni majungu na shutuma tupu!
Tukubaliane moja, CCM ni waoga kushughulikia jini walilolizalisha ndani na kulitumia kwa manufaa yao. CCm ni Wazandiki na Wanafiki, wanawadanganya Watanzania kuwa wanajisahihisha.
Je mlipokaa chini na kuandika Tujisahihishe, tuwasamehe mara 70 kama Wakristo na mafundisho ya Kristo kugeuza shavu mpaka lini?
Acheni kutulaghai, nyinyi ni Wanafiki na Waoga mnaoogopana kutokana na kutumiana kwa manufaa yenu ya pamoja kama Chama kuihujumu Tanzania!