Unachoona ni mipasuko kwenye dirisha la kioo!?

Unachoona ni mipasuko kwenye dirisha la kioo!?

Unakubuka wazo la shule za kata na jinsi zilivyokuwa zimepata upinzani bila ya wanaozipinga kutoa njia mbadala ya kuwafanya vijana kama sisi tusome? Unakumbuka shule hizo zilivyoanza kwenye mazingira magumu na sasa zilipo? hivi unajua kuna watu ambao ni PHD holders sasa na ni products ya shule hizo? unajua kuna wengine wanafanya kazi mpaka UN na ni product ya shule hizo?
mkuu unacho zungumka ni kweli labda niulize tukiweka katika mizani mafanikio ya shule za kata na kushindwa kwake kuna uiano upi?


unafahamu shule izo hutoa 0 na 4 nyingi kuliko 1-2-3. unaukumbuka mwaka hadi matokeo kurudiwa 60% walikuwa wamelamba 0.

je? tuendelee kusifia shule izi kisa kuna watu 4 wamefanikiwa hapo huku 900 wakishindwa
 
mkuu unacho zungumka ni kweli labda niulize tukiweka katika mizani mafanikio ya shule za kata na kushindwa kwake kuna uiano upi?


unafahamu shule izo hutoa 0 na 4 nyingi kuliko 1-2-3. unaukumbuka mwaka hadi matokeo kurudiwa 60% walikuwa wamelamba 0.

je? tuendelee kusifia shule izi kisa kuna watu 4 wamefanikiwa hapo huku 900 wakishindwa
Unapokuwa unafanya biashara lakini faida unayopata nikidogo, kama huna wazo bora zaidi la biashara linalotekelezeka zaidi ya biashara uliyonayo; unachotakiwa si kuacha biashara Bali kutafuta mbinu ambazo zitakusaidia kuongeza faida, na ukiona MTU anakushauri uache au anakukatisha tamaa huku hana wazo mbadala ujue mchawi!
 
1. Any way wewe umesoma shule gani kwanza na ni nini kinachoashiria kuwa uwezo wako wa uelewa wa mambo na kukabiliana na mazingira ili kuleta matokeo bora zaidi ni mkubwa kuliko wengine ?

2. Haujui kuwa CCM ndicho chama kinachoongonza kwa kuwa na able bodied and competent Human resources kwenye field ya uongozi? Rejea hapa,
Rasilimali watu ndani ya vyama vya siasa

Davos kuna nini kinachohusiana na mada hii, na unataka tufanye nini? inawezekana una wazo zuri ila tu hujaweza kulieleza vizuri.
Pole sana, Kama umesoma shule za kata na bado kichwa chako kina waza upande mmoja sio kosa lako, Jaribu kusoma sana vitabu, Kama huwezi soma vitabu tafuta pesa anza kutembelea baadhi ya nchi tulizopata nazo huru pamoja halafu uje ulinganishe na mawazo yako

Mawazo yako yamefungwa sana yawezekana umeishi sana sehemu moja hivyo unadhani wote wanafikiri kama eneo lenu

Vyeo havitafutwi hivyo ndani ya CCM, wewe huna unalowaza kichwani zaidi ya ccm

Shule za kata kiongozi gani atakubali mtoto wake akosome huko kwenye takataka zote, Hizo shule ni takataka kama na wewe umesoma huko ni takataka tu kama taka zingine
 
Unapokuwa unafanya biashara lakini faida unayopata nikidogo, kama huna wazo bora zaidi la biashara linalotekelezeka zaidi ya biashara uliyonayo; unachotakiwa si kuacha biashara Bali kutafuta mbinu ambazo zitakusaidia kuongeza faida, na ukiona MTU anakushauri uache au anakukatisha tamaa huku hana wazo mbadala ujue mchawi!
mkuu acha janja nyani, mpaka leo 50+yrs ccm imeshindwa kila idara/sekta unayo fahamu wewe. ila hautaki tuzione nyufa (mabaya yao ambao ni makubwa) kuliko maghorofa na madhari mengine (ambayo ni mazuri)

mkuu kubali tu tunapo chungulia nje tunaziona hizi nyufa kwa kuwa ni kubwa na za kutisha ndo maana tunaziongelea.

ila kwa rasilimali tulizo nazo na walicho fanya ccm ni hakuna. sawa na mtoto wa st. marys ama mariani apate ziro bado mzazi useme yuko vzr maana ametoka anajua kusoma na kuhesabu kwa kiingereza.

mambo ya iput kubwa alafu output kdg ndo unateta et tuendelee na biashara ya faida kidogo wakati mtaji unateketea
 

Unapoangalia nje kupitia dirisha la kioo, kuna vitu vingi vinavyoweza kuonekana. Hata hivyo utakachokiona itategemeana na dhamira, malengo na hali ya kifikra uliyonayo kwenye kichwa chako.

Kupitia kwenye dirisha hilo hilo, kuna atakayeona majengo mazuri, kuna atakayeona jinsi jua linavyochomoza, kuna atakayeona maji, kuna atakayeona kizunguzungu kama anataka kudondoka, kuna atakayeona kama jengo linadondoka kuna atakayeona kioo kina mpasuko n.k Yaani kwa Ujumla kila mmoja ataona vile alivyoji “ tune” kuona na hapo ndipo kufanikiwa au kufeli huanzia.

Kwa bahati mbaya, Watanzania tuliowengi kila tunapochungulia kwenye dirisha la nyumba yetu; hakuna tunachoona zaidi ya mipasuko iliopo kwenye kioo. Yaani kila anayechungulia anarudi kuwaambia wenzake hivi mshachungulia dirishani? Kuna mipasuko pale kwenye kioo halafu kama inaendelea vile!? kisha kila mtu anarudi ndani na kuwatisha wenzake na wote wanaungana kuogopa "creaks" kwenye kioo na baada ya hapo wote wanarudi ndani huku wakiwashawishi wale wanaoona possible opportunities nao waone creaks dirishani kisha wa - concentrate hapo tu!

Ni kweli inawezekana kuwe na mipasuko lakini hiyo haikufanyi usione vitu vingine vizuri kupitia dirisha hilo hilo na kufikiria namna ya kuvitumia vile uvionavyo kwa manufaa yako na ya wengine wakati pia unafikiria ni kwa vipi utakabiliana na mpasuko bila kuharibu dirisha.

Nitoe mfano kwenye Sekta ya Elimu. Zilivyoanzishwa shule za kata; walikuwepo watu miongoni mwetu ambao walizipinga sana kuwa hazifai kabisa wakasema "ma" –CCM yanapoteza muda. Hoja yao ilikuwa kwamba hazina waalimu, hazina madawati hazina maabara n.k na hivyo wakahitimisha kuwa hizo si shule bali ni bomu. Badala ya kuona zaidi positive side and possible opportunities zilizokuwepo kwenye shule hizo na kushauri namna ya kuzitumia na kuboresha panapostahili, wao walikuwa wanaona vikwazo tu na hivyo kuwakatisha tamaa wengine. Sasa leo watu wangapi wamenifaika na shule hizo?

Sasa ni shule hizo hizo ambazo wengine waliona zaidi positive side na wakazitumia vizuri na wengine sahizi wana Phd’s. Wengine hawana Phd’s lakini wana elimu ambayo imewasaidia kuwa na na mchango muhimu kwenye nchi hii na Miongoni mwa wanafaika wa shule hizi ni mimi mwenyewe na zisingekuwepo nisingezoma.

Kwa hiyo kama Nchi tuna changamoto nyingi, CCM wanafanya mambo mengi mazuri tu ila changamoto nazo bado zipo nyingi. Hata hivyo hakuna namna ambayo tunaweza tusipite kwenye changamoto kwa sababu hivyo ndivyo dunia ilivyo. Ili ufanikiwe lazima Pia ufeli wakati mwingine, upite kwenye maumivu na sulubu mbalimbali. Ndio maana unaona Nyerere alilaumiwa kwa mambo mengi sana, kadhalika Mzee Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Sasa Rais Magufuli licha ya kwamba hawa wote wana staili tofauti za ku approach mambo mbali mbali.

Kwa hiyo, inafaa tuwe tunaona ni fursa gani ambazo kupitia mazinngira yaliyopo na sera hizi hizi za CCM tunaweza kuzitumia kuifanya Tanzania kuwa sehemu bora zaidi ya kuishi. Pale ambapo kuna changamoto, tuwe “optimists” kwa kuchangua njia ambayo angalau inaweza kuwa na matokeo bora zaidi.

Kwa mfano, kama unaona mwenzako si mwana demokrasia wa kweli, hiyo kwako ni fursa ya wewe kuwa mwana demokrasia ili uwe mfano. Kama unaona mwenzako hana utu, huruma, ubinadamu, Kama unaona mwenzako ana lugha za kuudhi, basi wewe kuwa na lugha nzuri ili watu wajifunze kwako n.k wewe kuwa kinyume chake. Tujifunze kuangalia mambo kwa jicho positive na tutaona fursa nyingi ambazo tukizitumia vizuri kwa pamoja tunaweza kuifanya Tanzania kuwa nchi bora zaidi na ni katika msingi huo tunaweza kupata maendeleo ya kweli.

Ukiona kila ukitazama kwenye dirisha la kioo wewe unachoona ni mipasukopasuko tu, ujue una tatizo kubwa kwenye mfumo wako wa kufikiri na hiyo ndio huitwa “Pessimism” .Tuangalieni ni vitu gani ambavyo vinaweza kutusaidia kupiga hatua badala ya kung’ang’ania kuzungukia kwenye kamduara ambako hakatusaidii.

Hata nchi zilizoendelea ambazo wengi hupenda kukimbilia, uzuri wake ni matokeo ya staili za kufikiri za watu wake.
muda wa kuandika upuuzi unautoa wapi?
 

Unapoangalia nje kupitia dirisha la kioo, kuna vitu vingi vinavyoweza kuonekana. Hata hivyo utakachokiona itategemeana na dhamira, malengo na hali ya kifikra uliyonayo kwenye kichwa chako.

Kupitia kwenye dirisha hilo hilo, kuna atakayeona majengo mazuri, kuna atakayeona jinsi jua linavyochomoza, kuna atakayeona maji, kuna atakayeona kizunguzungu kama anataka kudondoka, kuna atakayeona kama jengo linadondoka kuna atakayeona kioo kina mpasuko n.k Yaani kwa Ujumla kila mmoja ataona vile alivyoji “ tune” kuona na hapo ndipo kufanikiwa au kufeli huanzia.

Kwa bahati mbaya, Watanzania tuliowengi kila tunapochungulia kwenye dirisha la nyumba yetu; hakuna tunachoona zaidi ya mipasuko iliopo kwenye kioo. Yaani kila anayechungulia anarudi kuwaambia wenzake hivi mshachungulia dirishani? Kuna mipasuko pale kwenye kioo halafu kama inaendelea vile!? kisha kila mtu anarudi ndani na kuwatisha wenzake na wote wanaungana kuogopa "creaks" kwenye kioo na baada ya hapo wote wanarudi ndani huku wakiwashawishi wale wanaoona possible opportunities nao waone creaks dirishani kisha wa - concentrate hapo tu!

Ni kweli inawezekana kuwe na mipasuko lakini hiyo haikufanyi usione vitu vingine vizuri kupitia dirisha hilo hilo na kufikiria namna ya kuvitumia vile uvionavyo kwa manufaa yako na ya wengine wakati pia unafikiria ni kwa vipi utakabiliana na mpasuko bila kuharibu dirisha.

Nitoe mfano kwenye Sekta ya Elimu. Zilivyoanzishwa shule za kata; walikuwepo watu miongoni mwetu ambao walizipinga sana kuwa hazifai kabisa wakasema "ma" –CCM yanapoteza muda. Hoja yao ilikuwa kwamba hazina waalimu, hazina madawati hazina maabara n.k na hivyo wakahitimisha kuwa hizo si shule bali ni bomu. Badala ya kuona zaidi positive side and possible opportunities zilizokuwepo kwenye shule hizo na kushauri namna ya kuzitumia na kuboresha panapostahili, wao walikuwa wanaona vikwazo tu na hivyo kuwakatisha tamaa wengine. Sasa leo watu wangapi wamenifaika na shule hizo?

Sasa ni shule hizo hizo ambazo wengine waliona zaidi positive side na wakazitumia vizuri na wengine sahizi wana Phd’s. Wengine hawana Phd’s lakini wana elimu ambayo imewasaidia kuwa na na mchango muhimu kwenye nchi hii na Miongoni mwa wanafaika wa shule hizi ni mimi mwenyewe na zisingekuwepo nisingezoma.

Kwa hiyo kama Nchi tuna changamoto nyingi, CCM wanafanya mambo mengi mazuri tu ila changamoto nazo bado zipo nyingi. Hata hivyo hakuna namna ambayo tunaweza tusipite kwenye changamoto kwa sababu hivyo ndivyo dunia ilivyo. Ili ufanikiwe lazima Pia ufeli wakati mwingine, upite kwenye maumivu na sulubu mbalimbali. Ndio maana unaona Nyerere alilaumiwa kwa mambo mengi sana, kadhalika Mzee Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Sasa Rais Magufuli licha ya kwamba hawa wote wana staili tofauti za ku approach mambo mbali mbali.

Kwa hiyo, inafaa tuwe tunaona ni fursa gani ambazo kupitia mazinngira yaliyopo na sera hizi hizi za CCM tunaweza kuzitumia kuifanya Tanzania kuwa sehemu bora zaidi ya kuishi. Pale ambapo kuna changamoto, tuwe “optimists” kwa kuchangua njia ambayo angalau inaweza kuwa na matokeo bora zaidi.

Kwa mfano, kama unaona mwenzako si mwana demokrasia wa kweli, hiyo kwako ni fursa ya wewe kuwa mwana demokrasia ili uwe mfano. Kama unaona mwenzako hana utu, huruma, ubinadamu, Kama unaona mwenzako ana lugha za kuudhi, basi wewe kuwa na lugha nzuri ili watu wajifunze kwako n.k wewe kuwa kinyume chake. Tujifunze kuangalia mambo kwa jicho positive na tutaona fursa nyingi ambazo tukizitumia vizuri kwa pamoja tunaweza kuifanya Tanzania kuwa nchi bora zaidi na ni katika msingi huo tunaweza kupata maendeleo ya kweli.

Ukiona kila ukitazama kwenye dirisha la kioo wewe unachoona ni mipasukopasuko tu, ujue una tatizo kubwa kwenye mfumo wako wa kufikiri na hiyo ndio huitwa “Pessimism” .Tuangalieni ni vitu gani ambavyo vinaweza kutusaidia kupiga hatua badala ya kung’ang’ania kuzungukia kwenye kamduara ambako hakatusaidii.

Hata nchi zilizoendelea ambazo wengi hupenda kukimbilia, uzuri wake ni matokeo ya staili za kufikiri za watu wake.
Hii ni falsafa zaidi...Kuna watu humu wataanza matusi Na kukutuhumu kutafuta vyeo badala ya kutafakari hoja
 
Unakubuka wazo la shule za kata na jinsi zilivyokuwa zimepata upinzani bila ya wanaozipinga kutoa njia mbadala ya kuwafanya vijana kama sisi tusome? Unakumbuka shule hizo zilivyoanza kwenye mazingira magumu na sasa zilipo? hivi unajua kuna watu ambao ni PHD holders sasa na ni products ya shule hizo? unajua kuna wengine wanafanya kazi mpaka UN na ni product ya shule hizo?

Mkuu hao PhD holders hata kama shule za kata zisingekuwepo wangukuwepo tu. Ulipaswa kuonyesha mafanikio ya hizo shule kwa ujumla kulinganisha na nyingine. Mkuu kumbuka hata nchi yetu ni masikini lakini haimaanishi haina watu matajiri.
 
Andiko zuri lkn ulicho chemsha ni kutoa mfano wa shule za kata. Hujiuliz kwa nn viongozi yeyote yule serikalini hapeleki mtoto wake shule ya kata? Me nilikutana na watoto wa mbagala secondary, walishindwa kuitikia salaam ya How are you ambayo mtoto wa chekechea anaweza. sasa hawa ndo wanakimbia Maths na Sience kwakuwa hazina waalimu eti wanataka kusoma Arts! Arts wkt hawajui kuandika sentensi hata moja ya kiingereza? Hapa kuna siasa tu za ccm kuwahadaa watu kuwa wamejenga sekondari na watoto wanasoma bure. Kitu ambacho serikali ingefanya ingeongeza zile shule zake km za mwanzo, ingeongeza maslah kwa waalimu hasa wa sayansi af wangejenga vyuo vya ufund vingi ambavyo vingekuwa vinawapa vijana utaalamu wa kuweza kujiajiri na kuajiliwa mfano ufundi, usafi, utalii, uvuvi, kilimo, ufugaji n.k. Sasa mtoto anapoteza miaka minne, wazaz ni masikini, unamkomboa vip huyu mtoto? %90 ya wanafunz shule za kata wanapoteza muda hiki ndo ambacho wengi wamekiona, hatoki na maarifa yoyote bara angekuwa veta 4 years angejifunza mengi. Wenzetu wanavyo tuita Shitholes ni kwa mambo km hayo. Ni vzr kuwa na shule za kata lkn ingekua kwa stages huku wakihakikisha kila kitu kipo sawa.
 
Naona kama shule za kata zimefanikiwa tu kutuongezea
ma 'yes men, cheerleaders, hero worshippers, na facebook literates'.
 
Naona mjadala umejikita katika mfano wa hoja moja ambayo imeteuliwa kama sifa jumuishi ya ujenzi wa fikra za uzi huu
Mzee baba kumbuka utamu na ubora wa chai haupimwi kwa rangi ya kikombe
 
Mtoa mada mbona ujaweka namba za simu ? Mana si kwa kujipendekeza uku.
 
Kwa hiyo wenye PHD ambao hawana impact kwenye jamii ni wale waliosoma shule za kata na waliosoma shule nyingine wana PHD na pia wana impact kwenye jamii? usipinge vitu tu ili mradi upinge.

Hoja yangu ni kwamba inapotokea chama, serikali au hata mtu aka innovate wazo linalolenga kutatua tatizo fulani nchini, badala ya kukatishana tamaa, tunatakiwa tuangalie possible opportunities zilizopokwenye wazo hilo na kuzitumia kwa maslahi ya wote na ikibidi tuboreshe badala ya kukatishana tamaa ili tubaki pale pale.
Yaani unatengeneza tatizo wewe mwenyewe, unalitatua wewe mwenyewe kwa kiwango duni hafifu na finyu halafu unaona unakatishwa tamaa.Na ukiona unapondwa sana kwa hizo possible opportunities zako lazma ujue kuna njia nyingine bora zaidi ya unayoitumia ndio maana unapondwa. Kuhusu PHD zenyu mpaka sasa mchango wake katika taifa ni negligible kwa hiyo dont even start!
 
Ukiona dude refu kama nini ujue ni pointless.....

mboyoyo mingi + utumbo mixer na makujipendekeza.
 
Umeanzisha post, mimi bila kujali maudhui yake kwani nimepitia na nimeogopa kuchangia zaidi ya hii post yako. Hao vijana wa chama kingine ambao hawana chuki na wana uwezo mpana wa kufikiri, mbona hawatokei kuchangia kwakuwa ni wazo zuri? Umeandika post nzuri, na ukaweka paragraph vizuri ili kila mtu aweze kusoma hata kama hataelewa. In short uko vizuri kwenye uandishi hata mawazo, ila wachangiaji wako wapi hasa wa hicho chama unachodhani kina watu smart? Nilitaraji hao vijana au washabiki wa hicho chama wangekuwa wamefikisha huu uzi page ya tano kwa jinsi ulivyotoa points, ila hawapo bali waliopo ni hao wa hicho chama unachokidharau. Jitafakari.
Angemtukana jpm au umbea wowote angepata wachangiaji wengi sana. Na unajua jukwaa hili wamejaa watu toka ufipa so kwa hili andiko wanapita kushoto.Kwani viewers ni wangap?
 
Angemtukana jpm au umbea wowote angepata wachangiaji wengi sana. Na unajua jukwaa hili wamejaa watu toka ufipa so kwa hili andiko wanapita kushoto.Kwani viewers ni wangap?

Kwani kuna aliyewazuia ccm kuingia humu jukwaani? Au kwakuwa huku hakuna mbeleko ya polisi hivyo inakuwa ngumu kwao kupambana kwa hoja? Huyo JPM anatukanwa na nani, sema anapewa ukweli wake na huko mtaani hakuna anayethubutu kumpa ukweli wake zaidi ya kumsifia hata kinafiki, hivyo akipewa ukweli wake hapa jukwaani inaonekana kama katukanwa. Mfano mimi sijawi kumtukana JPM hata siku moja, lakini namkosoa waziwazi ila watetezi wake wanatafsiri kukosolewa kwake ni kutukanwa.
 
Ila kitu kingine pengine nikuelimishe tu, huwa kwa kawaida mada zenye wachangiaji wengi ni zile zisizokuwa na mashiko, kwa hiyo unapoleta mada usilete ili upate wachangiaji wengi bali ili ufikishe ujumbe unaodhani ni sahihi na muhimu. Ushiishi kwa kupenda kushangiliwa na mob Psychology.
Umeniacha hapo kwenye mstari wa mwisho. Mob psychology inawezaje kushangilia ili hali siyo kiumbe?
 
Usiwe na akili za [emoji706] [emoji706] [emoji706] [emoji706]

Nini kisichoeleweka?
 
Back
Top Bottom