Unabii wa Nyerere umetimia Sudani

Unabii wa Nyerere umetimia Sudani

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
17,197
Reaction score
16,868
Katika moja ya hotuba zake mwl. Nyerere alituonya juu ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar na matokeo ya upande mmoja kuukimbia na kuuacha upande mwingine wa muungano ukishangaa na kuduaa kwa kukimbiwa na wenzao. Alisema upande utakaowakimbia wenzao hautabaki salama. Alisema Zanzibar ni Zanzibar na Tanganyika ni Tanganyika kwa sababu ya muungano, nje ya muungano hakuna Zanzibar bali kuna Unguja na Pemba, Wazanzibara na wazanzibari, Maalim Seif na Dr. Shein, Karume, na Tanganyika kuna Wasukuma, Wazanaki, Wachagga, Wapemba, Wazaramo, n.k.

Hebu ona kinachotokea sasa Sudan baada ya Sudani Kusini kuwakimbia wenzao wa Sudan Khartum. Sudan Khartum wamebaki salama na Sudan Juba waliowakimbia wenzao wakajikuta kumbe hakuna Sudan Kusini ila kuna makabila ya Dinka na Nuer. Ona sasa dhambi ya kuwakimbia wenzao wa Sudani Kaskazini inavyowatafuna S. Sudan, maelfu wanakufa na mamilioni wameyakimbia makazi yao. Kumbe Nyerere bana hasemi uongo ni mtakatifu kweli nilikuwa nawabishia wanaotaka kumtangaza ni mwenyeheri na mtakatifu, lakini kwa hili moja, naunga mkono kuitwa mtakatifu.

Zanzibar iwachukulie hatua madhubuti (upper hand) wale wote wanaotaka Zanzibar iwakimbie wenzao wa Tanganyika kwenye muungano. Tena iwachukulie hatua za wazi na bila kumung'unya maneno, hatua na vitendo watakavyowachukulia watu hao wenye ndoto ya kutaka Zanzibar ijitenge kutoka kwenye Muungano sasa na leoleo vinginevyo kinachotokea Sudani Kusini ni cha mtoto kwa kitakachotokea Zanzibar kama ikifanikiwa kujitenga, itakuwa vita ya Unguja dhidi ya majambia kutoka Uarabuni

Siasa za Zanzibar zina wadau wafuatao ambao watakuwa chanzo cha vurugu za Zanzibar ikijitenga:
1. Kisiwa cha Pemba na
Kisiwa cha Unguja
2. Watu wa Pemba na watu wa Unguja
3. Chama cha CUF na CCM
4. Watu wa Zanzibar waliotoka Tanganyika
5. Watu wa Pemba na Unguja walioko Tanganyika wanaokumbwa na sheria ya Ukazi ya Zanzibar
6. Wazanzibar walioko Tanganyika wanaotaka kugombea urais wa Zanzibar
7. Watu wa Unguja na Pemba wanaotaka kugombea Urais wa Zanzibar
8. Mgawanyo wa mali na rasilimali zilizoko Pemba na Unguja
9. Uislam na Ukristo Zanzibar
10. Historia ya mapinduzi ya Zanzibar

 
post yako ina ukweli fulani na uongo fulani.

Ukweli wake ni kuwa mnapoanza dhana ya kujitenga ni vigumu kufikiria mwisho wa kujitenga kama ambavyo Nyerere alivyosema. Nitaachia wengine waoangee uongo (inaccuracies) wa post yako
 
Nyerere aliokuwa kiongozi mwenye maono, maneno yake yataendelea kuishi, tusiwasema Sudan peka yao, hata hapa Tanzania tunaelekea huko, kwani tumeyaona mengi, mfano kiongozi anatamka kwenye jukwaa eti chama fulani ni cha dini fulani au cha watu wa kutoak ukanda fulani, hivi huyo kiongozi hajui kwamba anatengeneza chuki? Hivi hiyo dini aua huo ukanda wa hao watu wanapotoka cham chaka hakina wafuasi wala viongozi?
Tunawaona wabunge wanasimama bungeni 'mheshimiwa spika matatizo ya mkoa..... au jimbo... watuachie wenyewe" Watanzania tunabaki tumeduwaa na kujiuliza inamaana huo mkoa hauna maangiliano na mikoa mingine!
 
Yeye Mwl. Nyerere alitamka kuwa 'hiyo ni principle ya Mwenyezi Mungu na wala siyo sheria ya Nyerere', wale wote wanaodhani wakijitenga watanufaika kwa kujipatia madaraka na ukwasi, wanajidanganya-wataendelea kugombana kwa visingizio vya ukabila, udini au ukanda. Ni watu hasa waliofilisika kisiasa ndiyo wanapenda hizi short cuts.
 
Acha kujidhalilisha kwa kipi Zito kakifanya umfananishe na Massiah? Unadhani Zito hata akiondoka kwenye siasa nani atamkumbuka tena? Wewe ni kama wale wananchi waliotoa vilio siku Rostam anajivua gamba lakini leo hii ukienda kuwauliza hata hawamkumbuki tena.

Nyerere(RIP) alikua ametukuka kama Zito kabwe-massiah
 
Hakuna ukweli wala Uongo wowote ni Ujanja wa kupanda mbengu za WOGA kwa Wananchi.
 
Acha kujidhalilisha kwa kipi Zito kakifanya umfananishe na Massiah? Unadhani Zito hata akiondoka kwenye siasa nani atamkumbuka tena? Wewe ni kama wale wananchi waliotoa vilio siku Rostam anajivua gamba lakini leo hii ukienda kuwauliza hata hawamkumbuki tena.
mkuu kwani mbowe akijiuzulu wewe hutalia?kwakua chama chetu tumeamua kuwapenda viongozi badala ya chama mimi turufu yangu imeangua kwa ZZK na wewe mbowe!!aya tusihukumiane basi
 
Anko Sam acha kujichanganya, Hata principle inahitaji busara na akili ya kuweza kui apply, hata kama Nyerere alisema kwamba hiyo ni principle ya MwenyeziMungu na sio principle ya mwl Nyerere je hao wanaohangaika kutaka Zanzibar ijitenge hawaijui hiyo principle kama ipo? au ni mazezeta?
 
Hivi Rostam Azziz alikuwa mbunge wa wapi vile.
 
Umeambiwa na nani kwamba mi mwanachama au mshabiki wa Chadema? Nilikukosoa wewe kumfananisha Zito na massiah nikakuuliza kwa lipi alilowafanyia watanzania tangu awe mbunge hadi umwite hivyo? Hata akiacha siasa pengo lake halitaonekana,

mkuu kwani mbowe akijiuzulu wewe hutalia?kwakua chama chetu tumeamua kuwapenda viongozi badala ya chama mimi turufu yangu imeangua kwa ZZK na wewe mbowe!!aya tusihukumiane basi
 
Katika moja ya hotuba zake mwl. Nyerere alituonya juu ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar na matokeo ya upande mmoja kuukimbia na kuuacha upande mwingine wa muungano ukishangaa na kuduaa kwa kukimbiwa na wenzao. Alisema upande utakaowakimbia wenzao hautabaki salama. Alisema Zanzibar ni Zanzibar na Tanganyika ni Tanganyika kwa sababu ya muungano, nje ya muungano hakuna Zanzibar bali kuna Unguja na Pemba, Wazanzibara na wazanzibari, Maalim Seif na Dr. Shein, Karume, na Tanganyika kuna Wasukuma, Wazanaki, Wachagga, Wapemba, Wazaramo, n.k.

Hebu ona kinachotokea sasa Sudan baada ya Sudani Kusini kuwakimbia wenzao wa Sudan Khartum. Sudan Khartum wamebaki salama na Sudan Juba waliowakimbia wenzao wakajikuta kumbe hakuna Sudan Kusini ila kuna makabila ya Dinka na Nuer. Ona sasa dhambi ya kuwakimbia wenzao wa Sudani Kaskazini inavyowatafuna S. Sudan, maelfu wanakufa na mamilioni wameyakimbia makazi yao. Kumbe Nyerere bana hasemi uongo ni mtakatifu kweli nilikuwa nawabishia wanaotaka kumtangaza ni mwenyeheri na mtakatifu, lakini kwa hili moja, naunga mkono kuitwa mtakatifu.

Zanzibar iwachukulie hatua madhubuti (upper hand) wale wote wanaotaka Zanzibar iwakimbie wenzao wa Tanganyika kwenye muungano. Tena iwachukulie hatua za wazi na bila kumung'unya maneno, hatua na vitendo watakavyowachukulia watu hao wenye ndoto ya kutaka Zanzibar ijitenge kutoka kwenye Muungano sasa na leoleo vinginevyo kinachotokea Sudani Kusini ni cha mtoto kwa kitakachotokea Zanzibar kama ikifanikiwa kujitenga, itakuwa vita ya Unguja dhidi ya majambia kutoka Uarabuni

Siasa za Zanzibar zina wadau wafuatao ambao watakuwa chanzo cha vurugu za Zanzibar ikijitenga:
1. Kisiwa cha Pemba na
Kisiwa cha Unguja
2. Watu wa Pemba na watu wa Unguja
3. Chama cha CUF na CCM
4. Watu wa Zanzibar waliotoka Tanganyika
5. Watu wa Pemba na Unguja walioko Tanganyika wanaokumbwa na sheria ya Ukazi ya Zanzibar
6. Wazanzibar walioko Tanganyika wanaotaka kugombea urais wa Zanzibar
7. Watu wa Unguja na Pemba wanaotaka kugombea Urais wa Zanzibar
8. Mgawanyo wa mali na rasilimali zilizoko Pemba na Unguja
9. Uislam na Ukristo Zanzibar
10. Historia ya mapinduzi ya Zanzibar


Huwezi kufananisha Mungano wa Zanzibar na Tanganyika na Sudan,kumbuka Zanzibar na Tanganyika zilikuwa ni nchi huru zilizoamua kuungana kisiasa.

Sudan ilikuwa nchi moja iliyoamua kujigawa kisiasa,hii yote ni kutokana na ubadhilifu wa upande mmoja wa sudan ya warabu kuwabagua na kuwanyanyasa wenzao wa kusini Dinka na Nuer., ndio maana wasudani wakusini wakaamua kujitenga na wenzao wa kaskazini

Mungano wa Tanganyika na Zanzbar baada ya upande mmoja wa mungano kujifanya wanaume na upande wa pili kufanywa wanawake ndio maana upande wa wanawake(zanziabar) wameamua kujitoa kwenye ndoa ya muungano

Hiyo ni mifano ilioyofanana lakini iko tafauti.tafakari
 
katika moja ya hotuba zake mwl. Nyerere alituonya juu ya muungano wa tanganyika na zanzibar na matokeo ya upande mmoja kuukimbia na kuuacha upande mwingine wa muungano ukishangaa na kuduaa kwa kukimbiwa na wenzao. Alisema upande utakaowakimbia wenzao hautabaki salama. Alisema zanzibar ni zanzibar na tanganyika ni tanganyika kwa sababu ya muungano, nje ya muungano hakuna zanzibar bali kuna unguja na pemba, wazanzibara na wazanzibari, maalim seif na dr. Shein, karume, na tanganyika kuna wasukuma, wazanaki, wachagga, wapemba, wazaramo, n.k.

Hebu ona kinachotokea sasa sudan baada ya sudani kusini kuwakimbia wenzao wa sudan khartum. Sudan khartum wamebaki salama na sudan juba waliowakimbia wenzao wakajikuta kumbe hakuna sudan kusini ila kuna makabila ya dinka na nuer. Ona sasa dhambi ya kuwakimbia wenzao wa sudani kaskazini inavyowatafuna s. Sudan, maelfu wanakufa na mamilioni wameyakimbia makazi yao. Kumbe nyerere bana hasemi uongo ni mtakatifu kweli nilikuwa nawabishia wanaotaka kumtangaza ni mwenyeheri na mtakatifu, lakini kwa hili moja, naunga mkono kuitwa mtakatifu.

Zanzibar iwachukulie hatua madhubuti (upper hand) wale wote wanaotaka zanzibar iwakimbie wenzao wa tanganyika kwenye muungano. Tena iwachukulie hatua za wazi na bila kumung'unya maneno, hatua na vitendo watakavyowachukulia watu hao wenye ndoto ya kutaka zanzibar ijitenge kutoka kwenye muungano sasa na leoleo vinginevyo kinachotokea sudani kusini ni cha mtoto kwa kitakachotokea zanzibar kama ikifanikiwa kujitenga, itakuwa vita ya unguja dhidi ya majambia kutoka uarabuni

siasa za zanzibar zina wadau wafuatao ambao watakuwa chanzo cha vurugu za zanzibar ikijitenga:
1. Kisiwa cha pemba na
kisiwa cha unguja
2. Watu wa pemba na watu wa unguja
3. Chama cha cuf na ccm
4. Watu wa zanzibar waliotoka tanganyika
5. Watu wa pemba na unguja walioko tanganyika wanaokumbwa na sheria ya ukazi ya zanzibar
6. Wazanzibar walioko tanganyika wanaotaka kugombea urais wa zanzibar
7. Watu wa unguja na pemba wanaotaka kugombea urais wa zanzibar
8. Mgawanyo wa mali na rasilimali zilizoko pemba na unguja
9. Uislam na ukristo zanzibar
10. Historia ya mapinduzi ya zanzibar


na wewe na huyo nabii wako wa uongo....si huyo nyerere aki support hiyo sudan ijitenge?
Si yeye akisaidia kwa mafunzo?
Garang alikua hapa akisoma na kupata misaada....yote ni udini tuuuu
na anayo zungumzia nyerere kuhusu zanzibar ni udini pia haoni raha kuona waislam kule visiwani wakijitawala....walitawaliwa ...lakini ana ndoto ya kuwatawala ili kuhujumu uislamu

kwani kabla ya huu muungano si ilikuwapo zanzibar tena kubwa zaidi,

maneno ya nyerere ni ya unafiki na fikra za kikoloni..wagawe uwatawale....hii ndio falsafa yake kwa visiwa vile huu ni ukweli hata kiama...yule mzeee alikua ana chuki hasa na waislam wa zanzibar .
1995 nyerere alikuwepo akimpgia kampeni mkapa....alizunguka nchi nzima mpaka kapata ugonjwa ulomuondoa.
Kule zanzibar chama chake kilikua na hali ngumu...na matokeo rasmi ya wasimamizi ni kuwa ccm ilishindwa....CCM IKAPEWA USHINDI WA CHUMBANI tena kwa amri ya siri ya ccm na nyerere alukuwapo na anayajua haya,
mgogoro ukaibuka....watu wakatiwa misuko suko, walitiwa ndani na polisi walifanya uovu mbele ya camera za tv..nyerere yupo macho ..kama alikanyaga zanzibar mpaka amekufa....
Nyerere hakua na nia njema na zanzibar hata kidogo...aliacha ugomvi ule yeye akisulihisha migogoro ya watusi wenzake....zanzibar haikumhangaisha......zaidi ya kutoa matamko kama hayo ya kuwagawa.....alisema wazi kabla ya uhuru kuwa laiti angekuwa na uwezo basi angevi sokomeza mbali baharini visiwa hivi na kuvifukia...huyo ndio nyerere na zanzibar...
Wadanganye watoto na wanywa maji ya kijani
 
Back
Top Bottom