Tuna changamoto ya manabii, nashauri kikao cha manabii wote tuitwe, upembuzi ufanyike, nabii mwongo afungiwe kabla ya kanisa zima kutukanwa.
Mtu kalewa pombe anasema Dar itaangamizwa kwa mafuriko, hayajatokea anaangaliwa tu, Mara sijui mwezi flani kutakuwa na tukio kubwa, miezi inapita na yeye anachekewa tu, sio sawa.
Utamjuaje nabii mwongo?
Biblia Ina jibu..
Kumbukumbu 18:22 Atakaponena nabii kwa jina la BWANA, lisifuate jambo lile wala kutimia, hilo ndilo neno asilolinena BWANA; kwa kujikinai amelinena huyo nabii, usimwogope.