Umuhimu wa A level kwangu ni huu

Umuhimu wa A level kwangu ni huu

NTA Level 4 ni Certificate au mkuu ulitaka kusema level 6 ?

A level ni muhimu na unaelewa mambo mengi Sana

Kuliko hizo Diploma za kukariri na kuokota okota maelezo google

Hata ukiitwa Six leaver Ina sound great.

Na hata wazungu wanalijua hilo Mpaka jeshini kuna mshahara wake kabisa wa MTU aliyefika six
 
Labda uzungumzie mtu Aliyesoma diploma peke ake ila ambaye ameunganisha degree usimchukulie poa

Picha linaanzia chuo tu mtu wa a level asilimia 90 ya vitu vinakuwa vipya ila wa diploma ni kama anafanya muendelezo wa aliyoyasoma
Mtu mwenye D4 hafu ambaye hana msingi wa sayansi. Kumpa hizo degree na diploma zilisho sheheni Maarifa ya miaka 1950s. Nikumtishwa mzigo mzito sana
 
Mtu mwenye D4 hafu ambaye hana msingi wa sayansi. Kumpa hizo degree na diploma zilisho sheheni Maarifa ya miaka 1950s. Nikumtishwa mzigo mzito sana
Best student wa Muhas Mwaka huu hajatokea advance Amesoma diploma halafu kingine sio kila anayesoma diploma Amepata d4 watu wana vibanda vyao wanaenda diploma na kuacha a level

Stuka mzee usikariri
 
Hatuzungumzii mshahara tunazungumzia elimu.. ushaelewa nini namaanisha nimesoma A level, nimesoma Diploma, nimesoma Degree kwa hio naelewa ninachosema kote nimepiga kwata...

Mimi pia nimesoma level zote hizo Ila hauwezi kuichukulia poa Advance ni noma Sana .
 
1. A-level inaruhusu kufanya makosa kwasababu unaweza feli mwanzoni, mwishoni ukakaza ukafaulu NECTA. GPA ya kila semester inaamua hatma yako kwenye Diploma.

2. Vyuo vingi vya nje havitambui diploma, ni ngumu kwenda bila ACSEE.

3. Diploma ni mwaka 1 zaidi wa kukaa shule. Kumaliza shule mapema kuna faida zake.

4. Mara nyingi A-level ni nafuu kuliko Diploma.

5. Kwa masomo ya sayansi na uhandisi, A-level inajenga msingi mzuri sana wa hisabati na fizikia. Haya masomo yanafundishwa Diploma ila wanafunzi hawashurutishwi(fimbo😁) mwishowe wanashika machache.



Hayo ni maoni yangu kama mtu wa Diploma.
 
Best student wa Muhas Mwaka huu hajatokea advance Amesoma diploma halafu kingine sio kila anayesoma diploma Amepata d4 watu wana vibanda vyao wanaenda diploma na kuacha a level

Stuka mzee usikariri
Sasa mimi ninavyokwambia mambo mengi yanayosomwa huko diploma na degree. Mengi ni outdated haijalisha ni best student au last student wote wapo hapo hapo. Wakati huohuo advance shehemu kubwa ni sayansi yenyewe haibadiliki ndio msingi. Ukiwa nayo itakusaidi kufanya judgement huko mbeleni.
 
Inanifanya niweze kusoma mambo mengine nje na fani niliyoanza kuisoma. Pia inanifanya niweze kusoma mambo mapya kwenye fani. Kwakuwa mengi yanayosomwa diploma ni outdated
Umesema mambo mengi,tutajie mambo matatu tu katika hayo mambo mengi.

Pia,kwanini umeenda (umerudi) kusoma diploma wakati umesoma A-level?
 
Sasa mimi ninavyokwambia mambo mengi yanayosomwa huko diploma na degree. Mengi ni outdated haijalisha ni best student au last student wote wapo hapo hapo. Wakati huohuo advance shehemu kubwa ni sayansi yenyewe haibadiliki ndio msingi. Ukiwa nayo itakusaidi kufanya judgement huko mbeleni.
Ulizingua uliposema watu wa diploma ni wa d4 ndiyo maana nikakupinga

Hili siwez kulipinga maana me diploma sijasoma ila kwa jinsi nilivyowaona watu wa dilploma tulivyoingia bachelor kuna kitu wamepiga hatua kuliko sis wa advance
 
Kwanza level 4 sio diploma ni cheti.4&5=cheti
5&6=diploma
6&7=degree
8&----
Kwanza diploma anasomea ujuzi kazi anaweza kuajiliwa.six Bado elimu jumla huna ujuzi wowote.
 
Advanced diploma is equivalent degree

Hata Mwl Nyerere hana degree Ila Ana masters
Nimesema Diploma sio Advanced Diploma.. na kuna yule kiongozi katoka hapa na Certificate kaenda UK kapewa Masters hio pia utakataa?
 
Back
Top Bottom