Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,018
- 20,489
Ninafikiri kwamba, Umri wa kustaafu utumishi wa umma ushuke na kuwa angalau miaka 45 hivi, ama tuweke ukomo wa utumishi wa umma uwe miaka 15 tu, ili mtu akistaafu apate fursa ya kuyaishi maisha mengine ya kujitafutia kipato nje ya utumishi akiwa na nguvu zake kamili, na kuruhusu kizazi kingine kushika nafasi yake.,
Utafiti wangu usiorasmi unaonyesha wastaafu wengi hawakai miaka 5 hadi 15 hivi baada ya kistaafu wanakumbwa na matatizo ya kiafya ikiwemo msongo wa mawazo na ugumu wa kupata kipato kipya.
Ajira zote ziwe na ukomo ili kutuhusu watu wengi nchi kutumikia serikali ya Tanzania, Wako watu katika utumishi wanavipawa vya biashara na fani nyingine nyingi za kujiajiri, lakini wanauwa talanta zao kwa kumezwa na utumishi hadi uzeeni. Watoke waje mtaani wafanye biashara waonje maisha ya umma wa kawaida.
Tutapunguza sana pengo la walalaheri na walala hoi, hata nidhamu ya utumishi dhidi ya umma itarejea.
Na Yericko Nyerere
Utafiti wangu usiorasmi unaonyesha wastaafu wengi hawakai miaka 5 hadi 15 hivi baada ya kistaafu wanakumbwa na matatizo ya kiafya ikiwemo msongo wa mawazo na ugumu wa kupata kipato kipya.
Ajira zote ziwe na ukomo ili kutuhusu watu wengi nchi kutumikia serikali ya Tanzania, Wako watu katika utumishi wanavipawa vya biashara na fani nyingine nyingi za kujiajiri, lakini wanauwa talanta zao kwa kumezwa na utumishi hadi uzeeni. Watoke waje mtaani wafanye biashara waonje maisha ya umma wa kawaida.
Tutapunguza sana pengo la walalaheri na walala hoi, hata nidhamu ya utumishi dhidi ya umma itarejea.
Na Yericko Nyerere