Umri wa dunia ni upi hasa?

Umri wa dunia ni upi hasa?

Ilikuwa ni hivyo na mpaka leo ingekuwa ulimwengu wa hivyo, ila Adamu na Hawa walitibua na hapo ndo ulimwengu wa binadamu kuchagua mwenyewe njia ya kwenda ulipoanzia.

Adam na Hawa walitibua nini..???
 
Ndiyo mkuu, maana Biblia ingependa watu wafanyiwe maombi tu ili wapone, maana Mungu ndiyo muweza wa yote na kifo hupanga yeye.

Kwa mtu aliyeshika dini sawasawa, hakuna sababu ya kufanyiwa chanjo au operation, maana kama Mungu amekupangia siku ya kufa utakufa tu hata ukifanyiwa lolote, ila kama hajapanga hata usipoenda hospitali huwezi kufa, je ninakosea Ishmael na Eiyer?

Umekosea .....!!
 
Ndiyo mkuu, maana Biblia ingependa watu wafanyiwe maombi tu ili wapone, maana Mungu ndiyo muweza wa yote na kifo hupanga yeye.

Kwa mtu aliyeshika dini sawasawa, hakuna sababu ya kufanyiwa chanjo au operation, maana kama Mungu amekupangia siku ya kufa utakufa tu hata ukifanyiwa lolote, ila kama hajapanga hata usipoenda hospitali huwezi kufa, je ninakosea Ishmael na Eiyer?

Do you know that healing is one of GOD'S attributes? Do you know that Doctors and medicine can't heal but treat while it is God who heals people?
 
hili swali nimekujibu vizuri tu lakini hutaki kuelewa na kuanza kunikimbia

Umejibu lakini jibu lako limezua swali ambalo hujalijibu.

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambao maovu yanawezekana?

Alishindwa kuumba ambao maovu hayawezekani?

Kama alishindwa ana uwezo wote kweli?

Au aliweza ila hakutaka tu?

Kama aliweza ila hakutaka tu, ni kweli ana upendo wote?
 
Hapa kuna watu kama wa3 wameshavuruga ladha ya uzi kwa kuendekeza ubishi wa kijinga. Kama mnataka kubishana si muanzishe uzi wenu? Watu wanajadili umri wa dunia nyie mnatuletea swaga za mungu hayupo mara yupo.

Swali la.mingu linahusika.na.umri wa dunia.

Kuna wengine wanaamini biblia ni neno la mungu halisi. Biblia inatupa mtiririko wa kutaka kutusadikisha kwamba dunia ina miaka 6,000.

Mtu akoweza kuonyesha kwamba mungu wa biblia ni wa uongo na biblia haitakiwi.kuchukuliwa kama authority katika kutaja umri wa dunia, atakuwa kashatusaidia.kutupilia mbali dhana ya kwamba dunia ina miaka 6,000.

Hiwezi kutenganisha utafiti wa dunia ina umri gani na jinsi ilivyoanza.

Huwezi kuongelea habari za dunia ilivyoanza bila kuongelea habari za mungu.
 
Ilikuwa ni hivyo na mpaka leo ingekuwa ulimwengu wa hivyo, ila Adamu na Hawa walitibua na hapo ndo ulimwengu wa binadamu kuchagua mwenyewe njia ya kwenda ulipoanzia.

Kwa nini mungu ambaye mnasema ana uwezo wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambao Adamu na Hawa wanaweza kutibua?

Alikuwa hawezi kuumba ulimwengu ambao Adamu na Hawa hawakuweza kutibua?

Kama hakuweza, je ni kweli anaweza yote?

Kama aliweza na akatubania tu, je ni kweli ana upendo wote?

Adamu na Hawa uwezo wa kufikiri wameupata kutoka wapi? Na kwa nini mungu kawapa uwezo mdogo mpaka watibue?
 
Jua Mungu siku zote hapingani na sayansi, Kitu Sayansi inafanya ni kugundua mambo Mungu aliyoyaweka. Huyu mdau hapa chini amepata mafunuo ambayo ndio yanaelezea kwanini tunaweza kuwa na dinosaurs waliokuwepo miaka mingi kabla ya dunia hii tunayoijua.

Ni kweli dunia ina miaka mingi. Takrabini milioni kadhaa. Sidhani kama itakuwa imefika kwenye bilioni. Katika kutafiti kwangu nilifahamu kuwa hapo zamani dunia ilikuwa ikikaliwa na viumbe mbali mbali kama Dinosaurs. Sasa baada ya vita ya kule mbinguni Shetani na malaika zake wakatupwa huku duniani. Wakafanya uharibifu mkubwa sana wa dunia. Mungu alipoona hivyo akakasirika akaigandisha dunia (ice age) kwa miaka mingi sana. Wale viumbe wote waliokaa duniani wakafa ikiwa ni pamoja na hao Dinosaurs. Baada ya miaka mingi Mungu akaaamua kuifufua dunia, sasa historia mpya ya dunia inaanzia kwenye biblia kitabu cha mwanzo ambapo dunia ilikuwa giza tupu na Roho wa Bwana akikaa juu ya maji. Ndipo Mungu akasema iwepo nuru nayo nuru ikawa. Akatenga nchi kavu na bahari and story goes on and on. So dunia hii sio ya leo. (hii ni kutokana na udadavuzi wangu wa maandiko. Sina uhakika wa asilimia mia na hiki wadau)
 
Do you know that healing is one of GOD'S attributes? Do you know that Doctors and medicine can't heal but treat while it is God who heals people?
Why take medicine while there is God who heals?
Ina maana Mungu hawezi kuponya hadi asaidiwe na madawa?
 
Swali la.mingu linahusika.na.umri wa dunia.

Kuna wengine wanaamini biblia ni neno la mungu halisi. Biblia inatupa mtiririko wa kutaka kutusadikisha kwamba dunia ina miaka 6,000.

Mtu akoweza kuonyesha kwamba mungu wa biblia ni wa uongo na biblia haitakiwi.kuchukuliwa kama authority katika kutaja umri wa dunia, atakuwa kashatusaidia.kutupilia mbali dhana ya kwamba dunia ina miaka 6,000.

Hiwezi kutenganisha utafiti wa dunia ina umri gani na jinsi ilivyoanza.

Huwezi kuongelea habari za dunia ilivyoanza bila kuongelea habari za mungu.

wapi biblia imeandika dunia ina miaka 6000 ??
 
Umejibu lakini jibu lako limezua swali ambalo hujalijibu.

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambao maovu yanawezekana?

Alishindwa kuumba ambao maovu hayawezekani?

Kama alishindwa ana uwezo wote kweli?

Au aliweza ila hakutaka tu?

Kama aliweza ila hakutaka tu, ni kweli ana upendo wote?

narudia kukujibu swali hili je binadamu mitazamo tunafanana ?
 
wapi biblia imeandika dunia ina miaka 6000 ??

Chronology ya vizazi kutoka Adam mpaka Yesu ni miaka 4,000. Chronology ya vizazi kutoka Yesu mpaka sasa.ni takeibani miaka 2,000. Jumla miaka 6,000.
 
Chronology ya vizazi kutoka Adam mpaka Yesu ni miaka 4,000. Chronology ya vizazi kutoka Yesu mpaka sasa.ni takeibani miaka 2,000. Jumla miaka 6,000.

wapi wameandika hayo ??
kwa nini unaamini ??
kama ulifanya uchunguzi weka data hapa unajua Adam aliishi miaka mingapi ??
 
narudia kukujibu swali hili je binadamu mitazamo tunafanana ?

Hatufanani.

Na hapo ndipo logic inapokuja kusawazisha nani ana make sense na nani hana sense.

Jibu lako limefeli mtihani wa logic.

Your answer is logically inconsistent.
 
Why take medicine while there is God who heals?
Ina maana Mungu hawezi kuponya hadi asaidiwe na madawa?
Do you speak for God? Medicine does not heal but treat. Get that fact correct. It is God who heals.

If medicine heals, why do people die after taking them?
 
[h=2]Mwanzo 1[/h]
[h=3]Kuumbwa ulimwengu[/h][SUP]1[/SUP]Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia.[SUP]2[/SUP]Dunia ilikuwa bila umbo na tupu. Giza lilikuwa limefunika vilindi vya maji na roho ya Mungu ilikuwa ikitanda juu ya maji.
[SUP]3[/SUP]Mungu akasema, “Mwanga uwe.” Mwanga ukawa. [SUP]4[/SUP]Mungu akauona mwanga kuwa ni mwema. Kisha Mungu akautenganisha mwanga na giza, [SUP]5[/SUP]mwanga akauita “Mchana” na giza akaliita “Usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya kwanza.
[SUP]6[/SUP]Mungu akasema, “Anga liwe katikati ya maji, liyatenge maji sehemu mbili.”[SUP]7[/SUP]Mungu akalifanya anga, akayatenga maji yaliyo juu ya anga na yale yaliyo chini ya anga hilo. Ikawa hivyo. [SUP]8[/SUP]Mungu akaliita anga “Mbingu.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya pili.
[SUP]9[/SUP]Mungu akasema, “Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, nchi kavu itokee.” Ikawa hivyo. [SUP]10[/SUP]Mungu akapaita mahali pakavu “Nchi” na kusanyiko la maji akaliita “Bahari.” Mungu akaona kuwa ni vyema.
[SUP]11[/SUP]Kisha Mungu akasema, “Nchi na ioteshe mimea. Mimea izaayo mbegu, na miti izaayo matunda yenye mbegu.” Ikawa hivyo. [SUP]12[/SUP]Basi, nchi ikaotesha mimea izaayo mbegu kwa jinsi yake, na miti izaayo matunda yenye mbegu kwa jinsi yake. Mungu akaona kuwa ni vyema. [SUP]13[/SUP]Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya tatu.
[SUP]14[/SUP]Mungu akasema, “Mianga na iweko angani, itenge mchana na usiku, ioneshe nyakati, majira, siku na miaka, [SUP]15[/SUP]na ingae angani na kuiangazia dunia.” Ikawa hivyo.[SUP]16[/SUP]Basi, Mungu akafanya mianga miwili mikubwa; ule mkubwa utawale mchana na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia. [SUP]17[/SUP]Mungu akaiweka mianga hiyo angani iiangazie dunia, [SUP]18[/SUP]ipate kutawala mchana na usiku, na kuutenga mwanga na giza. Mungu akaona kuwa ni vyema. [SUP]19[/SUP]Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya nne.
[SUP]20[/SUP]Mungu akasema, “Maji na yatoe makundi ya viumbe hai na ndege waruke angani.”[SUP]21[/SUP]Basi, Mungu akaumba wanyama wakubwa sana wa baharini na aina zote za viumbe vyote hai viendavyo na kujaa majini; akaumba na aina zote za ndege wote. Mungu akaona kuwa ni vyema. [SUP]22[/SUP]Mungu akavibariki, akasema, “Zaeni, muongezeke, muyajaze maji ya bahari; nao ndege waongezeke katika nchi.” [SUP]23[/SUP]Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya tano.
[SUP]24[/SUP]Mungu akasema, “Nchi na itoe aina zote za viumbe hai, wanyama wa kufugwa, viumbe vitambaavyo na wanyama wa porini wa kila aina.” Ikawa hivyo. [SUP]25[/SUP]Basi, Mungu akafanya aina zote za wanyama wa porini, wanyama wa kufugwa, na viumbe vitambaavyo. Mungu akaona kuwa ni vyema.
[SUP]26[/SUP]Kisha Mungu akasema, “Tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; atawale samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vitambaavyo.” [SUP]27[/SUP] Basi, Mungu akaumba mtu kwa mfano wake; naam, kwa mfano wake Mungu alimuumba. Aliwaumba mwanamume na mwanamke. [SUP]28[/SUP]Mungu akawabariki na kuwaambia, “Zaeni muongezeke, mkaijaze nchi na kuimiliki; muwatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kitembeacho duniani.”
[SUP]29[/SUP]Kisha Mungu akasema, “Tazama, nawapeni kila mmea duniani uzaao mbegu, na kila mti uzaao matunda yenye mbegu; mbegu zao au matunda yao yatakuwa chakula chenu. [SUP]30[/SUP]Nao wanyama wote duniani, ndege wote wa angani, viumbe vyote vitambaavyo, naam, kila kiumbe chenye uhai, chakula chao kitakuwa majani yote ya mimea.” Ikawa hivyo. [SUP]31[/SUP]Mungu akaona kila kitu alichokifanya kuwa ni chema kabisa. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya sita.
 
Back
Top Bottom