Katika kufatilia huku nimekuja kupata mkanganyiko kwa namna biblia inavyoelezea vizazi toka kuumbwa Dunia na vilivyomo pamoja na Adam ambapo hata miaka 10,000 haifiki!! Upande wa pili ukiwafatilia wanasayansi ni kwamba kilichoanza ni Big bang(miaka 13.7bilion iliyopita), zikafuatia nyota na baadaye sayari yetu dunia(miaka 4.6 bilion iliyopita).
Kitu kikubwa cha kujua hapa ni kuwa ushahidi tulio nao unafanana. Tatizo ni unatafsiri vipi ushahidi huo. Kila mtu ana mtazamo (framework) ambao anautumia kutafsiri. Mfano ukisema hakuna Mungu, kila kitu kinakuwa na tafsiri ambayo itakuwa na majibu yote isipokuwa "Mungu aliumba" maana falsafa yako ni hakuna Mungu. Kwa hiyo hata kama kitu Mungu aliumba huwezi kusema aliumba, utasenaje hivyo ilhali mtazamo wako ni kuwa hakuna Mungu?
Vivyo hivyo kwa mtu ambaye anaamini kuna Mungu Muumbaji,l kila atakapokutana na utendaji unaohitaji akili atasema kuwa kuna Mtu mwenye akili aliyefanya hili. Huu hapa mfano m adogo tu:
Watu wawili walikuwa wako ziwani, mara ikatokea Mv. Victoria. Ghafla wale watu wakaanza kubishana. Mmoja wao alidhania kuwa hakuna viwanda vya meli. na Mtazamo wa mwingine ni kuwa viwanda vipo. Yule wa kwanza akadai kuwa dude lile wanaloliona (meli) lilitokea lenyewe tu bahati mbaya baada ya Jumbo Jet kupata ajali somehow majivu ya jumbo Jet yali react na maji kupata meli. Mwingine alikataa, akamwambia kuna kiwanda na hata hivi karibunia alisoma manuals za meli zikielezea namna meli zinaundwa. Akajaribu kumshawishi kuwa anamjua hata mbunifu wa hizo meli na mtengenezaji. Yule mwingine aliendelea kubisha akisema HAIWEZEKANI meli iwe imetengeneza kwa kuwa HAKUNA KIWANDA.
Hapo utaona kuwa tatizo si ushahidi (meli) bali ni mgongano wa mitazamo. Na mitazamo huwa haipimwi kisayansi ila kifalsafa. Kwa hiyo unapaswa kupima mitazamo hii. Ni Aidha Mungu aliumba, au vitu vilijiumba vyenyewe.
Unaposema "Upande wa pili ukiwafatilia wanasayansi" unakosea. Wanasayansi wengi akiwemo Isaac Newton, Johan Keppler na hata leo wanasayansi wenye PhD kama Jason Lisle, Jonathan Sharfati, Henry Morris et al hawaamini hilo na bado ni wanasayansi wakubwa tu. Kwa hiyo badilisha na useme "Upande wa pili ukiwafatilia wasioamini uumbaji" hapo utakuwa sahihi. (Kiungwana utakuwa umetenda haki kufanya hivyo).
Sasa tujibu swali la msingi. Kwa kuwa tatizo ni mgongano wa falsafa na misingi ya kufanyia maamuzi, inabidi kujiuliza swali hili la msingi kabisa, "Tunajuaje tunachokijua?"
Kwa wale wasioamini juu ya Mungu wa biblia watabaki wanaelea. Hii ni kwa sababu mwanadamu hana uwezo wa kuthibitisha chochote. Akisema ajaribu tu kuanza kuthibitisha inabidi KWANZA AAMINI kuwa Ubongo wake unaaminika. Swali ni kuwa tunapimaje kama Ubongo wako unaaminika kabla hatuajutumia kuthibitisha chochote? Au akitaka kwend laboratory kufanya experiment itabidi AAMINI kuwa akifanya majaribio thamani ya gravity kwa mfano itakuwa ni ileile. Swali ni kuwa, KWA NINI aamini kuwa gravity itabakia kuwa ileile? kwa nini ASIAMINI kuwa somehow inaweza kubadilika randomly? Kwa hiyo bila Mungu wa BIBLIA, huwezi kuthibitisha chochote kile (let alone kuuliza swali).
Maswali haya ni rahisi sana kwa mtu mwenye kuamini Biblia. Mfano hatuanzi kupima chochote kwa fahamu zetu. Tunaanza na Neno la Mungu, anayejua yote na mkamilifu. Kwa hiyo basi tunajua hayo yote yatakuwa hiyo kwa kuwa Mungu aliyetuumba kwa mfano wake ametupa uwezo wa kufikiri (reasoning) na kwa hiyo tunaweza tumia uwezo huo kuthibitisha mambo mbalimbali. Gravity itabaki constant kwa kuwa Mungu ameamuru iwe hivyo na Yeye mwenyewe anaishikilia kwa nguvu ya Neno lake.
Kwa hiyo wasioamini juu ya Mungu wa Biblia ambaye ndiye Muumbaji, hawawezi kushndana hata kwa hoja kwa kuwa inabidi waanze na swali la msingi "unajuaje unachokijua" kabla hata hawajajaribu kupanga hoja. Na kwa kuwa hawawezi kujibu swali hili, mengine yote hayawezekani kwao
Je kwanini kuna tofauti kubwa sana kati ya kinachoitwa kitabu kitakatifu na sayansi ya ulimwengu, ni waandika biblia walidanganya au wanasayansi wanadanganya?
Biblia sio kitabu cha kiada cha sayansi. Lakini kila kinapoongelea mambo ya kisayansi kipo sahihi kabisa. Unaposema wanasayansi vs Biblia unakosea na sababu nimeisema hapo juu. Hope utabadili na hili pia.
Vipi kuhusu mabaki ya Dinosaurs yaliyogunduliwa na utafiti kuonesha hawa viumbe waliishi zaidi ya miaka 200 million iliyopita?
Hakuna utafiti wenye ushahidi unaonesha hivyo. Huo ni uzushi wa "wanasayansi" uaowaongelea ambao kiukweli ni wakana Mungu.
Dino mmoja aligundulika akiwa na "soft tissues" ambazo haziwezi ku survive miaka hata laki kadhaa. Sasa hii ya kuwa waliishi milioni nyingi hizi ushahidi wake uko wapi? Kuna mtu alikuwepo? Maana kwa tissue hizi kukutwa kwa Dino ni ushahidi tosha hawakuishi zama unazodai.
Hope umejua mbivu na mbichi
Tindikali