Umeya Dar: CCM waenda tena kortini

Umeya Dar: CCM waenda tena kortini

1. UDA itawekwa wazi
2. Mabasi yaendayo kasi itakuwa ishu
3. Mabango watu watafungwa
4. Miradi ya jiji itakula gichwa vya watu
5. Treni ya Mwakyembe itawekwa wazi
6. Viwanja vya wazi jipu kuu
7. Etc

UKAWA ikichukuwa madaraka CCM itapata shida sana na hasa waliojipa viwanja vya wazi
Inawezekana kuna mapato yanaenda kwenye chama chetu kileee!
 
bora amani ya moyo kuliko heshima!ccm na magufuli wanaogopa kushindwa kwani umeya ukienda ukawa,ccm watakosa mengi!pesa na pia maovu yao mengi yatakuwa uchi,halafu si unajua ukawa wanavyo jua kupiga domo...makonda na magufuli watakuwa on defensive kutetea madudu ya uda,dart na uchafu mwengine
Kamwe Magufuli hatutegemei aungane na majipu kuficha uozo! Rais Magufuli jiandae kutumbua majipu yatakayodhihirika! Tunakuaminia!
 
Jamani huu Umeya imekuwa mchezo wa kuigiza? Kila kukicha umeya tukiamka umeya! Mwishowe naona sasa waziri wa Serikali za Mitaa ambaye ni Rais anaweza kuamua kutumia rungu kama alilotumia Sumaye miaka ileee tukaona Tume ya Keenja!

Dar ndio moyo wa nchi, haiwezi kukaa miezi mingi hivi bila Meya. Tusubiri tu Tume
hicho ndicho wanachotafuta hakuna jengine
 
Uchaguzi wa umeya apewe Jecha tu kusimamia.Amefanya kazi nzuri visiwani.
 
Renatus Mkinga leo Jumapili asubuhi (Star TV) amewaambia CCM wananchi wameamua DSM iongozwe na UKAWA na hesabu ziko kinyume na CCM, hivyo waache unafiki wao wakubali yaishe.
 
Back
Top Bottom