sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,032
Nakumbuka nikiwa Arusha nasoma chuo cha uhasibu miaka ya 2013 kama sijakosea, kuna siku nlishuka kituo cha SDA pale Njiro ili niende ghetto.
Basi nimetembea kama mita kumi hivi njia nzima nipo peke yangu mara nasikia kuna mtu kama anatembeaa ila kwa vishindo kidogo sana, kucheki nyuma kuna njemba hata sijui ilikotokea, kwa hatua za kiusalama akili ilifunguka nikaongeza mwendo ila nikienda kushoto nae anakuja kushoto nikienda kulia nae ni kulia anakuja kwa kuongeza mwendo, mara mbele yangu akatokea mwengine kama anataka anizibe flani hivi.
Nilitoka mbio, sikuruhusu kuwa ndani ya 18 zao maana kwa stori tulizokuwa tukiskia ni kwamba wale vijana ni hatari tupu, nlijidai kama nmesimama flani hivi, akilini nikawa nachora ramani nikimbilie wapi, basi ile nakariba kuwa ndani ya 18 nlitoka spidi nadhani ile siku ndio nlikimbia tangu nizaliwe, wakati nataka nianze kukimbia moja wao alinipiga na kitu kama ubao, nilivyofika geto nilikuwa na kanundu kwa mbali, walinifukuza kidogo ila kwa mbio nilizotoka naona walisanda huku wakinisindikiza na matusi mazito ila nashukuru niliwakwepa.
Basi nimetembea kama mita kumi hivi njia nzima nipo peke yangu mara nasikia kuna mtu kama anatembeaa ila kwa vishindo kidogo sana, kucheki nyuma kuna njemba hata sijui ilikotokea, kwa hatua za kiusalama akili ilifunguka nikaongeza mwendo ila nikienda kushoto nae anakuja kushoto nikienda kulia nae ni kulia anakuja kwa kuongeza mwendo, mara mbele yangu akatokea mwengine kama anataka anizibe flani hivi.
Nilitoka mbio, sikuruhusu kuwa ndani ya 18 zao maana kwa stori tulizokuwa tukiskia ni kwamba wale vijana ni hatari tupu, nlijidai kama nmesimama flani hivi, akilini nikawa nachora ramani nikimbilie wapi, basi ile nakariba kuwa ndani ya 18 nlitoka spidi nadhani ile siku ndio nlikimbia tangu nizaliwe, wakati nataka nianze kukimbia moja wao alinipiga na kitu kama ubao, nilivyofika geto nilikuwa na kanundu kwa mbali, walinifukuza kidogo ila kwa mbio nilizotoka naona walisanda huku wakinisindikiza na matusi mazito ila nashukuru niliwakwepa.