sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
Hello,
Kuna muda hasa utotoni na tukiwa vijana wadogo huwa ni kawaida mtu ajitetee kwa kupigana, Hata wanyama hupigana ili kutafuta haki ama kuonyesha dominance.
Sasa katika mapambano haya kuna muda unakuta huna tofauti na mtu alievamia mtumbwi wa vibwengo, unaishia kuchapika mbele ya hadhara, Loh aibu hiyo isikieni tu.
Binafsi nakumbuka katika siku niliyopoteza pambano ilikuwa nikiwa kidato cha tano (form 5), Pambano lilikuwa ni mimi mtoto wa town mwenye rekodi yangu nzuri tu tangu shule ya msingi na mtaani nishakalisha wengi, niliyakanyaga kwa jamaa flani katoka kijijini huko mikoani namuona mshamba mshamba.
Nilikuwa napenda kumtania tania ila kuna siku alimaindi sana tukiwa darasani, nikamwambia atulize mshono jogoo wa shamba hawiki mjini, darasani pale nusu tudundane lakini tukakubaliana tuyamalize baada ya vipindi, mida ya saa saba hivi baada ya kutoka kwenye vipindi tukaenda nyuma ya ukuta wa shule ndio ilikuwaga sehemu ya kuyamaliza matatizo kiume.
Nikawa naruka ruka ile kujiona kama tyson kumtambia huyo jamaa wa bush jinsi watoto wa mjini tunavyopasha kabla ya mfumuo, mtoto wa town nikatumia mbinu yangu ya surprise attack, ile hata hajajiandaa vizuri nikamrushia ngumi kama mbili hivi, hii mbinu nishaitumia kumaliza pambano mapema ila kwa huyu jamaa hali ikawa tofauti, kwake ni kama ngumi zangu zilimpapasa yani kama hazijamuingia hata, alinirushia ngumi nikakwepa nikaongeza ujazo kwenye ngumi yangu kudhania za kwanza sikuzijazia lakini jamaa ilikuwa ni kama napiga gunia la mchele daaah!
Yeye ngumi nyingi akirusha nakwepa ila chache zinazonikuta ni zinauma jamani, ni kama napigwa na mawe, maumivu haya yalinipa hasira nikawa namtupia upper cut lakini wapi, narusha za chembe lakini wapi, narusha teke lakini ni kama napiga gunia tu, aisee!
yeye ngumi yake akiirusha inauma jamani acheni tu.
Ilibidi nikimbie pambano lakini watu walikuwa wametuzunguka wananisukuma nirudi ulingoni, najaribu kuzikinga ngumi za jamaa lakini jamaa ngumi zake zinaumiza mpaka mikono nayotumia kujikinga, na nikimrushia jama ngumi ni kama napiga gunia la mchele, kiukweli nilikata tamaa, tena kuna muda alinisoma ile navyomrushia ngumi nae anarusha yake na ikinikuta ilikuwa inanipasua kweli kweli.
Bahati yangu viranja walikuja kutuachisha lakini nilikuwa nimetandikwa si mchezo.
Nakumbuka tu baada ya wiki tulikuwa marafiki sana na huyo jamaa lakini aibu niliyoipata ile siku siwezi kuja sahau.
Kuna muda hasa utotoni na tukiwa vijana wadogo huwa ni kawaida mtu ajitetee kwa kupigana, Hata wanyama hupigana ili kutafuta haki ama kuonyesha dominance.
Sasa katika mapambano haya kuna muda unakuta huna tofauti na mtu alievamia mtumbwi wa vibwengo, unaishia kuchapika mbele ya hadhara, Loh aibu hiyo isikieni tu.
Binafsi nakumbuka katika siku niliyopoteza pambano ilikuwa nikiwa kidato cha tano (form 5), Pambano lilikuwa ni mimi mtoto wa town mwenye rekodi yangu nzuri tu tangu shule ya msingi na mtaani nishakalisha wengi, niliyakanyaga kwa jamaa flani katoka kijijini huko mikoani namuona mshamba mshamba.
Nilikuwa napenda kumtania tania ila kuna siku alimaindi sana tukiwa darasani, nikamwambia atulize mshono jogoo wa shamba hawiki mjini, darasani pale nusu tudundane lakini tukakubaliana tuyamalize baada ya vipindi, mida ya saa saba hivi baada ya kutoka kwenye vipindi tukaenda nyuma ya ukuta wa shule ndio ilikuwaga sehemu ya kuyamaliza matatizo kiume.
Nikawa naruka ruka ile kujiona kama tyson kumtambia huyo jamaa wa bush jinsi watoto wa mjini tunavyopasha kabla ya mfumuo, mtoto wa town nikatumia mbinu yangu ya surprise attack, ile hata hajajiandaa vizuri nikamrushia ngumi kama mbili hivi, hii mbinu nishaitumia kumaliza pambano mapema ila kwa huyu jamaa hali ikawa tofauti, kwake ni kama ngumi zangu zilimpapasa yani kama hazijamuingia hata, alinirushia ngumi nikakwepa nikaongeza ujazo kwenye ngumi yangu kudhania za kwanza sikuzijazia lakini jamaa ilikuwa ni kama napiga gunia la mchele daaah!
Yeye ngumi nyingi akirusha nakwepa ila chache zinazonikuta ni zinauma jamani, ni kama napigwa na mawe, maumivu haya yalinipa hasira nikawa namtupia upper cut lakini wapi, narusha za chembe lakini wapi, narusha teke lakini ni kama napiga gunia tu, aisee!
yeye ngumi yake akiirusha inauma jamani acheni tu.
Ilibidi nikimbie pambano lakini watu walikuwa wametuzunguka wananisukuma nirudi ulingoni, najaribu kuzikinga ngumi za jamaa lakini jamaa ngumi zake zinaumiza mpaka mikono nayotumia kujikinga, na nikimrushia jama ngumi ni kama napiga gunia la mchele, kiukweli nilikata tamaa, tena kuna muda alinisoma ile navyomrushia ngumi nae anarusha yake na ikinikuta ilikuwa inanipasua kweli kweli.
Bahati yangu viranja walikuja kutuachisha lakini nilikuwa nimetandikwa si mchezo.
Nakumbuka tu baada ya wiki tulikuwa marafiki sana na huyo jamaa lakini aibu niliyoipata ile siku siwezi kuja sahau.