Six Man
JF-Expert Member
- Dec 19, 2017
- 254
- 892
Nimeona orodha mbalimbali ya watu wakiorodhesha idadi ya vitabu walivyosoma mwaka jana. Katika wote walioandika orodha zao mwandishi Fadhy Mtanga anaongoza kwa kusoma vitabu 107 kwa mwaka jana pekee.
Nimeona orodha ya mbunge wa Kigoma Mh Zitto Kabwe, orodha ya rais wa zamani wa Marekani Barack Obama na watu wengine kadhaa mashuhuri.
Kusoma vitabu ni jambo zuri na kujivunia kwakuwa vitabu ni chakula cha ubongo. Msomaji wa vitabu anaipumzisha akili yake kwa muda na kusoma akili za wenzake. Vitabu pia ni burudani murua kwa msomaji. Vitabu vinakukutanisha na watu ambao hukuwaza hata simu moja kukutana nao. Unataka kukutana na Bill Gate? Soma vitabu vyake. Unataka kukutana na Hussein Tuwa? Soma vitabu vyake. Unataka kukutana na Halfani Sudy? Soma vitabu vyake.
Tuwe jamii ya kupenda kusoma vitabu ili kujua mambo mbalimbali ulimwenguni.
Nikuulize wewe unayesoma uzi huu, umesoma vitabu vingapi mwaka 2017, tutajie kama unaweza na sio mbaya ukashauri wenzio vitabu vizuri vya kusom katika mwaka huu wa 2018.
Naitwa Six Man.
Nimeona orodha ya mbunge wa Kigoma Mh Zitto Kabwe, orodha ya rais wa zamani wa Marekani Barack Obama na watu wengine kadhaa mashuhuri.
Kusoma vitabu ni jambo zuri na kujivunia kwakuwa vitabu ni chakula cha ubongo. Msomaji wa vitabu anaipumzisha akili yake kwa muda na kusoma akili za wenzake. Vitabu pia ni burudani murua kwa msomaji. Vitabu vinakukutanisha na watu ambao hukuwaza hata simu moja kukutana nao. Unataka kukutana na Bill Gate? Soma vitabu vyake. Unataka kukutana na Hussein Tuwa? Soma vitabu vyake. Unataka kukutana na Halfani Sudy? Soma vitabu vyake.
Tuwe jamii ya kupenda kusoma vitabu ili kujua mambo mbalimbali ulimwenguni.
Nikuulize wewe unayesoma uzi huu, umesoma vitabu vingapi mwaka 2017, tutajie kama unaweza na sio mbaya ukashauri wenzio vitabu vizuri vya kusom katika mwaka huu wa 2018.
Naitwa Six Man.