Watu walionufaishwa na Usomaji wa Vitabu

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2023
4,694
6,396
Msomaji wa Vitabu anafahamu jinsi Vitabu vilivyo na umuhimu mkubwa sana katika maisha ya kila siku. Vilikuwa muhimu tokea zamani, lakini katika zama hizi, umuhimu umeongezeka mara nyingi sana.

Pamoja na umuhimu huo, kungali kuna idadi kubwa ya Waafrika, Watanzania wakiwemo, ambao hawaupi vitabu umuhimu unaoastahiki.

Kutokuvipa vitabu kipaumbele huenda kumechochewa na kutokufahamu faida zake.

Hiyo ndiyo sababu iliyonipelekea kuanzisha huu uzi, kwa lengo la kuwatia moyo Watanzania wenzangu, kwamba kusoma vitabu vizuri kamwe hakuwezi kuwa upotevu.

Naamini pia humu jukwaani kuna magwiji wenye taarifa zilizoshiba, zao binafsi na za watu wengine walionufaishwa na usomaji wa Vitabu.

Tafadhali ikiwa unafahamu chochote kuhusiana na hilo, naomba uandike humu kwa manufaa ya wengi.

Hawa ni miongoni mwa watu waliofanikiwa kutokana na tabia zao za usomaji.

1. Warren Buffett
Ni C.E.O wa Berkshire Hathaway. Pamoja na umri wake mkubwa, miaka 92, bado anatumia asilimia themanini ya muda wake kusoma vitabu.

Alianza kusoma vitabu tokea akiwa na miaka 7, na ameendelea na hiyo tabia mpaka uzeeni mwake.

Anahusianisha mafanikio yake na tabia ya usomaji.

Alipoulizwa jinsi ya kufanikiwa, alishauri kusoma kurasa 500 za kitabu kila siku. Maarifa mtu anayojikisanyia hatimaye yatakuwa sehemu ya maisha yake.

2. Dr. Ben Carson
Wakati akiwa madarasa ya chini, aliaminika kuwa ndiye mwanafunzi kilaza kuliko wote darasani kwao. Hata yeye aliamini hivyo pia.

Jitihada za mama yake kumlazimisha kusoma Vitabu kulizaa matunda. Miezi kama sita baada ya kuuanza huo utaratibu, kulimpelekea kufanya ugunduzi mkubwa sana maishani mwake, kwamba yeye naye ana akili.

Ugunduzi huo ulimfanya ainuke kitaaluma, kutoka kuwa mkia hadi kuongoza darasani. Baadaye alikuja kuwa daktari bingwa aliyesaidia wagonjwa wengi ndani na nje ya Marekani.

3. Mohamed Said
Simfahamu sana huyu mzee. Nimeanza kusoma makala zake Jamii Forum hivi karibuni. Makala chache nilizozisoma zimenihakikishia kuwa ni msomaji mzuri wa Vitabu. Nina uhakika kuwa ni kati ya watu walio na mafanikio katika maisha yao.

Bado sijafanikiwa kukisoma kitabu alichokiandika, lakini hakitaweza kunipiga chenga. Nitavitafuta.

4. Bill Gates
Pamoja na kuwa na mambo mengi, bado anajitahidi kusoma vitabu visivyopungua 50 kwa mwaka.

Anakiri kuwa Vitabu ndiyo chanzo kikuu cha maarifa yaliyomwezesha kuwa na mafanikio makubwa kiuchumi.

5. Eric Shigongo.
Naamini wengi wanamfahamu. Yeyote aliyewahi kufuatilia Historia ya maisha yake, atakubaliana nami kuwa mtaji mkuu wa mafanikio yake ni Vitabu.

Sijawahi kukutana naye ana kwa ana, lakini nilifanikiwa kusoma makala kadhaa yanayohusu maisha yake na mafanikio. Nilishakisoma na kitabu chake kinachofundiaha na kuhamasisha mafanikio.

Kwa ufupi, yuko vizuri kichwani.

Shigongo ni mfanyabiashara na mbunge katika Bunge la JAMHURI ya Muungano wa Tanzania. Na kama nilivyosema, mafanikio aliyo nayo, msingi wake mkuu ni usomaji Vitabu.

5. Christopher Mwakasege
Ingawa ni Mchumi kitaaluma, lakini pia ni Mhubiri. Ameshaandika Vitabu vingi, hasa vya mafundisho ya Kikristo ambavyo baadhi vina mwelekeo wa Kiuchumi. Wasomaji wa Vitabu wanafahamu kuwa waandishi wazuri wa Vitabu ni wasomaji wazuri pia. Ukisoma Vitabu vyake utang'amua kuwa ni msomaji mzuri.

6. Julius K. Nyerere
Huyu naye alifanya urafiki na Vitabu. Mzee Said Mohamed alishawahi kuandika makala yaliyoonesha kuwa baba wa Taifa alikuwa ni mtu wa Vitabu.

Naamini hata mbinu alizozichagua kutumia wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika, kulichagizwa na usomaji wake wa Vitabu. Aliufahamu vyema ulimwengu wa wakati wake.

7. Richard Branson
Ni mmoja wa mabilionea wa Uingereza. Aliacha shule akiwa na miaka 15, lakini hakupeana talaka na vitabu. Anakisifia kitabu cha kiuchumi kiitwacho SMALL IS BEAUTIFUL kuwa ndiko alikopata mawazo yaliyofanya mapinduzi katika biashara zake. Ni kawaida yake kutembea na notebook kwa ajili ya kuandika mawazo mapya anayoyapata kwa njia mbalimbali ikiwemo Vitabu.

8. Tony Robbins
Alipokuwa High School, alikuwa ameshasoma zaidi ya Vitabu 500, vingi vikiwa vya Saikolojia.

Kupitia Usomaji, alijikusanyia maarifa aliyokuja kuyageuza kuwa mtaji na hatimaye kuwa miongoni mwa watu wenye mafanikio makubwa sana ulimwenguni.

Kwa mifano hiyo michache, ni wazi kuwa tokea zamani hata sasa, Vitabu vimeendelea kuwa na umuhimu mkubwa sana katika kuchochea maendeleo.

Naomba kuwasilisha.
 
Joe Navarro we Lofa umeona HEKIMA hizi ?
Anapoanguka Mzee jua maktaba imeondoka hasa kama hakuacha maneno na mafundisho yake yaishi kwa mfumo wa sauti au maandiko.
Maarifa ni jambo jema ila maarifa sahihi ni jambo jema zaidi maana bora kuwa hujui kitu kuliko kushikiria taarifa za uongo.
Soma na chalenji taarifa kwa Fikra au taarifa kwa taarifa.
Kwa kupitia maandiko wengi wameondoa a na dharau za wajuvi.

Uzi umekaa kitaalam🥇🥇🥇
 
Thomas Edson alihudhuria darasani kwa miezi michache tu, lakini hilo halikumfanya asiwe msomi.

Baada ya kushindikana kuendelea na masomo, mama yake alichukua jukumu la kumfundisha kusoma na kuandika nyumbani.

Kujua kwake kusoma na kuandika kulikuwa mlango wa mafanikio yake. Alipenda sana vitabu.

Kupenda kwake kusoma sana kullimwezesha kujielimisha na kuwa mmoja wa wanasayansi wakubwa sana ulimwenguni. Alifanya gunduzi za Kisayansi zaidi ya elfu moja.
 
Msomaji wa Vitabu anafahamu jinsi Vitabu vilivyo na umuhimu mkubwa sana katika maisha ya kila siku. Vilikuwa muhimu tokea zamani, lakini katika zama hizi, umuhimu umeongezeka mara nyingi sana.

Pamoja na umuhimu huo, kungali kuna idadi kubwa ya Waafrika, Watanzania wakiwemo, ambao hawaupi vitabu umuhimu unaoastahiki.

Kutokuvipa vitabu kipaumbele huenda kumechochewa na kutokufahamu faida zake.

Hiyo ndiyo sababu iliyonipelekea kuanzisha huu uzi, kwa lengo la kuwatia moyo Watanzania wenzangu, kwamba kusoma vitabu vizuri kamwe hakuwezi kuwa upotevu.

Naamini pia humu jukwaani kuna magwiji wenye taarifa zilizoshiba, zao binafsi na za watu wengine walionufaishwa na usomaji wa Vitabu.

Tafadhali ikiwa unafahamu chochote kuhusiana na hilo, naomba uandike humu kwa manufaa ya wengi.

Hawa ni miongoni mwa watu waliofanikiwa kutokana na tabia zao za usomaji.

1. Warren Buffett
Ni C.E.O wa Berkshire Hathaway. Pamoja na umri wake mkubwa, miaka 92, bado anatumia asilimia themanini ya muda wake kusoma vitabu.

Alianza kusoma vitabu tokea akiwa na miaka 7, na ameendelea na hiyo tabia mpaka uzeeni mwake.

Anahusianisha mafanikio yake na tabia ya usomaji.

Alipoulizwa jinsi ya kufanikiwa, alishauri kusoma kurasa 500 za kitabu kila siku. Maarifa mtu anayojikisanyia hatimaye yatakuwa sehemu ya maisha yake.

2. Dr. Ben Carson
Wakati akiwa madarasa ya chini, aliaminika kuwa ndiye mwanafunzi kilaza kuliko wote darasani kwao. Hata yeye aliamini hivyo pia.

Jitihada za mama yake kumlazimisha kusoma Vitabu kulizaa matunda. Miezi kama sita baada ya kuuanza huo utaratibu, kulimpelekea kufanya ugunduzi mkubwa sana maishani mwake, kwamba yeye naye ana akili.

Ugunduzi huo ulimfanya ainuke kitaaluma, kutoka kuwa mkia hadi kuongoza darasani. Baadaye alikuja kuwa daktari bingwa aliyesaidia wagonjwa wengi ndani na nje ya Marekani.

3. Mohamed Said
Simfahamu sana huyu mzee. Nimeanza kusoma makala zake Jamii Forum hivi karibuni. Makala chache nilizozisoma zimenihakikishia kuwa ni msomaji mzuri wa Vitabu. Nina uhakika kuwa ni kati ya watu walio na mafanikio katika maisha yao.

Bado sijafanikiwa kukisoma kitabu alichokiandika, lakini hakitaweza kunipiga chenga. Nitavitafuta.

4. Bill Gates
Pamoja na kuwa na mambo mengi, bado anajitahidi kusoma vitabu visivyopungua 50 kwa mwaka.

Anakiri kuwa Vitabu ndiyo chanzo kikuu cha maarifa yaliyomwezesha kuwa na mafanikio makubwa kiuchumi.

5. Eric Shigongo.
Naamini wengi wanamfahamu. Yeyote aliyewahi kufuatilia Historia ya maisha yake, atakubaliana nami kuwa mtaji mkuu wa mafanikio yake ni Vitabu.

Sijawahi kukutana naye ana kwa ana, lakini nilifanikiwa kusoma makala kadhaa yanayohusu maisha yake na mafanikio. Nilishakisoma na kitabu chake kinachofundiaha na kuhamasisha mafanikio.

Kwa ufupi, yuko vizuri kichwani.

Shigongo ni mfanyabiashara na mbunge katika Bunge la JAMHURI ya Muungano wa Tanzania. Na kama nilivyosema, mafanikio aliyo nayo, msingi wake mkuu ni usomaji Vitabu.

5. Christopher Mwakasege
Ingawa ni Mchumi kitaaluma, lakini pia ni Mhubiri. Ameshaandika Vitabu vingi, hasa vya mafundisho ya Kikristo ambavyo baadhi vina mwelekeo wa Kiuchumi. Wasomaji wa Vitabu wanafahamu kuwa waandishi wazuri wa Vitabu ni wasomaji wazuri pia. Ukisoma Vitabu vyake utang'amua kuwa ni msomaji mzuri.

6. Julius K. Nyerere
Huyu naye alifanya urafiki na Vitabu. Mzee Said Mohamed alishawahi kuandika makala yaliyoonesha kuwa baba wa Taifa alikuwa ni mtu wa Vitabu.

Naamini hata mbinu alizozichagua kutumia wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika, kulichagizwa na usomaji wake wa Vitabu. Aliufahamu vyema ulimwengu wa wakati wake.

7. Richard Branson
Ni mmoja wa mabilionea wa Uingereza. Aliacha shule akiwa na miaka 15, lakini hakupeana talaka na vitabu. Anakisifia kitabu cha kiuchumi kiitwacho SMALL IS BEAUTIFUL kuwa ndiko alikopata mawazo yaliyofanya mapinduzi katika biashara zake. Ni kawaida yake kutembea na notebook kwa ajili ya kuandika mawazo mapya anayoyapata kwa njia mbalimbali ikiwemo Vitabu.

8. Tony Robbins
Alipokuwa High School, alikuwa ameshasoma zaidi ya Vitabu 500, vingi vikiwa vya Saikolojia.

Kupitia Usomaji, alijikusanyia maarifa aliyokuja kuyageuza kuwa mtaji na hatimaye kuwa miongoni mwa watu wenye mafanikio makubwa sana ulimwenguni.

Kwa mifano hiyo michache, ni wazi kuwa tokea zamani hata sasa, Vitabu vimeendelea kuwa na umuhimu mkubwa sana katika kuchochea maendeleo.

Naomba kuwasilisha.
Dunia ni kubwa sana mkuu kuna watu billion 8 sahivi na mafanikio uja kwa njia mbalimbali mfano mzuri baba levo, kinamwijaku na the like wanamafanikio mazuri tu kibongobongo sababu ya uchawa .
Diamond, mario, kiba , joti, mayele, feisali na the like wamefanikiwa na kuwa maarufu kwa vipaji vyao.

Kwangu mm usomaji wa vitabu ni utamaduni wa wazungu sisi tunanjia yetu ya kupeana maarifa iliyokuwepo enzi na enzi ya masimulizi kutoka kizazi kimoja kwenda kingine na km unafatilia kwa makini watu wetu hawapendi utaratibu wa kusoma vitabu ila masimulizi utawapata wengi sana mfano kipindi cha masimulizi the story book kinawafuasi wengi sana..

Ingawa nakiri kwamba masimulizi mengi tuliyonayo sasa ni udaku zaidi hivyo jamii inalishwa udaku zaidi kuliko maarifa chanya
 
Benjamin Franklin ni mmoja wa Wamerekani wanaoaminika wametoa mchango mkubwa sana katika Taifa lake. Alikuwa ni mwanadiplomasia, mwanauchumi, na mwanasayansi.

Ingawa alishaaga dunia siku nyingi, bado Wamarekani wanaendelea kumkumbuka hata sasa. Wameitenga tarehe 17 January kila mwaka kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa. Amekuwa mtu muhimu sana kwa Taifa lake.

Lakini alifikaje huko kote?

Kwanza, alihudhuria shule kwa kipindi kisichozidi miaka miwili tu. Hali duni ya kiuchumi ya familia yake ilimlazimu kukatisha masomo.

Lakini hilo halikumfanya aache kujielimisha. Alipenda sana kujisomea. Inasemekana, alikuwa anatumiapaka hela ya chakula kumnunulia Vitabu.

Alipenda sana kusoma vitabu na tabia hiyo ilikuja kumlipa sana, si yeye tu, na Taifa lake pia.
 
Joe Navarro we Lofa umeona HEKIMA hizi ?
Anapoanguka Mzee jua maktaba imeondoka hasa kama hakuacha maneno na mafundisho yake yaishi kwa mfumo wa sauti au maandiko.
Maarifa ni jambo jema ila maarifa sahihi ni jambo jema zaidi maana bora kuwa hujui kitu kuliko kushikiria taarifa za uongo.
Soma na chalenji taarifa kwa Fikra au taarifa kwa taarifa.
Kwa kupitia maandiko wengi wameondoa a na dharau za wajuvi.

Uzi umekaa kitaalam🥇🥇🥇
Dogo propaganda inaweza kushawishi sifuri ikawa Mia, Daima usije ukaa mini ukweli watakuwekea kene and ishi never.
 
Zitto Kabwe ni mwasisi na kiongozi mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo.

Mwaka 2022, alisoma viatabu 33

Mwaka 2021, Vitabu 29

Mwaka 2020, vitabu 16,

Na Mwaka 2019, Vitabu 34.

Sijabahatika kusoma popote jinsi vitabu vilivyomsaidia kufika alipo kisiasa n.k., lakini naamini lazima vina mchango mkubwa kwenye mafanikio yake.

Vitabu na mafanikio ni kama Pete na chanda.
 
Msomaji wa Vitabu anafahamu jinsi Vitabu vilivyo na umuhimu mkubwa sana katika maisha ya kila siku. Vilikuwa muhimu tokea zamani, lakini katika zama hizi, umuhimu umeongezeka mara nyingi sana.

Pamoja na umuhimu huo, kungali kuna idadi kubwa ya Waafrika, Watanzania wakiwemo, ambao hawaupi vitabu umuhimu unaoastahiki.

Kutokuvipa vitabu kipaumbele huenda kumechochewa na kutokufahamu faida zake.

Hiyo ndiyo sababu iliyonipelekea kuanzisha huu uzi, kwa lengo la kuwatia moyo Watanzania wenzangu, kwamba kusoma vitabu vizuri kamwe hakuwezi kuwa upotevu.

Naamini pia humu jukwaani kuna magwiji wenye taarifa zilizoshiba, zao binafsi na za watu wengine walionufaishwa na usomaji wa Vitabu.

Tafadhali ikiwa unafahamu chochote kuhusiana na hilo, naomba uandike humu kwa manufaa ya wengi.

Hawa ni miongoni mwa watu waliofanikiwa kutokana na tabia zao za usomaji.

1. Warren Buffett
Ni C.E.O wa Berkshire Hathaway. Pamoja na umri wake mkubwa, miaka 92, bado anatumia asilimia themanini ya muda wake kusoma vitabu.

Alianza kusoma vitabu tokea akiwa na miaka 7, na ameendelea na hiyo tabia mpaka uzeeni mwake.

Anahusianisha mafanikio yake na tabia ya usomaji.

Alipoulizwa jinsi ya kufanikiwa, alishauri kusoma kurasa 500 za kitabu kila siku. Maarifa mtu anayojikisanyia hatimaye yatakuwa sehemu ya maisha yake.

2. Dr. Ben Carson
Wakati akiwa madarasa ya chini, aliaminika kuwa ndiye mwanafunzi kilaza kuliko wote darasani kwao. Hata yeye aliamini hivyo pia.

Jitihada za mama yake kumlazimisha kusoma Vitabu kulizaa matunda. Miezi kama sita baada ya kuuanza huo utaratibu, kulimpelekea kufanya ugunduzi mkubwa sana maishani mwake, kwamba yeye naye ana akili.

Ugunduzi huo ulimfanya ainuke kitaaluma, kutoka kuwa mkia hadi kuongoza darasani. Baadaye alikuja kuwa daktari bingwa aliyesaidia wagonjwa wengi ndani na nje ya Marekani.

3. Mohamed Said
Simfahamu sana huyu mzee. Nimeanza kusoma makala zake Jamii Forum hivi karibuni. Makala chache nilizozisoma zimenihakikishia kuwa ni msomaji mzuri wa Vitabu. Nina uhakika kuwa ni kati ya watu walio na mafanikio katika maisha yao.

Bado sijafanikiwa kukisoma kitabu alichokiandika, lakini hakitaweza kunipiga chenga. Nitavitafuta.

4. Bill Gates
Pamoja na kuwa na mambo mengi, bado anajitahidi kusoma vitabu visivyopungua 50 kwa mwaka.

Anakiri kuwa Vitabu ndiyo chanzo kikuu cha maarifa yaliyomwezesha kuwa na mafanikio makubwa kiuchumi.

5. Eric Shigongo.
Naamini wengi wanamfahamu. Yeyote aliyewahi kufuatilia Historia ya maisha yake, atakubaliana nami kuwa mtaji mkuu wa mafanikio yake ni Vitabu.

Sijawahi kukutana naye ana kwa ana, lakini nilifanikiwa kusoma makala kadhaa yanayohusu maisha yake na mafanikio. Nilishakisoma na kitabu chake kinachofundiaha na kuhamasisha mafanikio.

Kwa ufupi, yuko vizuri kichwani.

Shigongo ni mfanyabiashara na mbunge katika Bunge la JAMHURI ya Muungano wa Tanzania. Na kama nilivyosema, mafanikio aliyo nayo, msingi wake mkuu ni usomaji Vitabu.

5. Christopher Mwakasege
Ingawa ni Mchumi kitaaluma, lakini pia ni Mhubiri. Ameshaandika Vitabu vingi, hasa vya mafundisho ya Kikristo ambavyo baadhi vina mwelekeo wa Kiuchumi. Wasomaji wa Vitabu wanafahamu kuwa waandishi wazuri wa Vitabu ni wasomaji wazuri pia. Ukisoma Vitabu vyake utang'amua kuwa ni msomaji mzuri.

6. Julius K. Nyerere
Huyu naye alifanya urafiki na Vitabu. Mzee Said Mohamed alishawahi kuandika makala yaliyoonesha kuwa baba wa Taifa alikuwa ni mtu wa Vitabu.

Naamini hata mbinu alizozichagua kutumia wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika, kulichagizwa na usomaji wake wa Vitabu. Aliufahamu vyema ulimwengu wa wakati wake.

7. Richard Branson
Ni mmoja wa mabilionea wa Uingereza. Aliacha shule akiwa na miaka 15, lakini hakupeana talaka na vitabu. Anakisifia kitabu cha kiuchumi kiitwacho SMALL IS BEAUTIFUL kuwa ndiko alikopata mawazo yaliyofanya mapinduzi katika biashara zake. Ni kawaida yake kutembea na notebook kwa ajili ya kuandika mawazo mapya anayoyapata kwa njia mbalimbali ikiwemo Vitabu.

8. Tony Robbins
Alipokuwa High School, alikuwa ameshasoma zaidi ya Vitabu 500, vingi vikiwa vya Saikolojia.

Kupitia Usomaji, alijikusanyia maarifa aliyokuja kuyageuza kuwa mtaji na hatimaye kuwa miongoni mwa watu wenye mafanikio makubwa sana ulimwenguni.

Kwa mifano hiyo michache, ni wazi kuwa tokea zamani hata sasa, Vitabu vimeendelea kuwa na umuhimu mkubwa sana katika kuchochea maendeleo.

Naomba kuwasilisha.
vitabu vina manufaa makubwa sana,mimi vinanisaidia sana kuongeza maarifa ya kuijua dunia vizuri sana
 
Kwangu mm usomaji wa vitabu ni utamaduni wa wazungu sisi tunanjia yetu ya kupeana maarifa iliyokuwepo enzi na enzi ya masimulizi kutoka kizazi kimoja kwenda kingine na km unafatilia kwa makini watu wetu hawapendi utaratibu wa kusoma vitabu ila masimulizi utawapata wengi sana mfano kipindi cha masimulizi the story book kinawafuasi wengi sana..

Ingawa nakiri kwamba masimulizi mengi tuliyonayo sasa ni udaku zaidi hivyo jamii inalishwa udaku zaidi kuliko maarifa chanya
Mkuu, Mzungu hana hati miliki ya usomaji wa Vitabu. Ipo wazi kwa kila binadamu. Kwa kuwa tu wametangulia kufahamu umuhimu wa kusoma vitabu hakuwapi hati miliki ya hilo.

Kama wametutangulia, si kosa na sisi kuiga, maadam tu ni jambo jema. Mbona, hata hivyo, tumeshaiga vingi tu?

Simu janja imetoka kwa Mzungu

Unywaji chai haikuwa utamaduni wetu. Uliletwa na Mzungu.

Ugali usingekuwa moja ya vyakuka vyety kama tusingekubali kupokea cha Mzungu. Ni kupitia Wareno, kama sikosei, mahindi yaliingia Tanzania

Wali nao vipi? Mapishi yake hayakubuniwa na Watanzania. Yana asili ya Bara la Asia, nafikiri kwa Wahindi au Wachina.

Kusoma na kuandika nao pia ni utamaduni uliletwa na watu wa nje.

Kusoma Vitabu ni haki ya kila mtu. Kuwamilikisha Wazungu peke yao ni kuwakabidhi hatma yako.
 
Mkuu, Mzungu hana hati miliki ya usomaji wa Vitabu. Ipo wazi kwa kila binadamu. Kwa kuwa tu wametangulia kufahamu umuhimu wa kusoma vitabu hakuwapi hati miliki ya hilo.

Kama wametutangulia, si kosa na sisi kuiga, maadam tu ni jambo jema. Mbona, hata hivyo, tumeshaiga vingi tu?

Simu janja imetoka kwa Mzungu

Unywaji chai haikuwa utamaduni wetu. Uliletwa na Mzungu.

Ugali usingekuwa moja ya vyakuka vyety kama tusingekubali kupokea cha Mzungu. Ni kupitia Wareno, kama sikosei, mahindi yaliingia Tanzania

Wali nao vipi? Mapishi yake hayakubuniwa na Watanzania. Yana asili ya Bara la Asia, nafikiri kwa Wahindi au Wachina.

Kusoma na kuandika nao pia ni utamaduni uliletwa na watu wa nje.

Kusoma Vitabu ni haki ya kila mtu. Kuwamilikisha Wazungu peke yao ni kuwakabidhi hatma yako.
Ni kweli ila tukubaliane tu jamii yetu haipendelei usomaji ila inapendelea masimulizi zaidi.
 
Dunia ni kubwa sana mkuu kuna watu billion 8 sahivi na mafanikio uja kwa njia mbalimbali mfano mzuri baba levo, kinamwijaku na the like wanamafanikio mazuri tu kibongobongo sababu ya uchawa .
Diamond, mario, kiba , joti, mayele, feisali na the like wamefanikiwa na kuwa maarufu kwa vipaji vyao.

Kwangu mm usomaji wa vitabu ni utamaduni wa wazungu sisi tunanjia yetu ya kupeana maarifa iliyokuwepo enzi na enzi ya masimulizi kutoka kizazi kimoja kwenda kingine na km unafatilia kwa makini watu wetu hawapendi utaratibu wa kusoma vitabu ila masimulizi utawapata wengi sana mfano kipindi cha masimulizi the story book kinawafuasi wengi sana..

Ingawa nakiri kwamba masimulizi mengi tuliyonayo sasa ni udaku zaidi hivyo jamii inalishwa udaku zaidi kuliko maarifa chanya
Asilimia kubwa ya wanaosoma vitabu wanatumia maarifa wanayoyapata kwenye vitabu kutatua Changamoto za Dunia hii....achana na habari za akina diamond
 
Asilimia kubwa ya wanaosoma vitabu wanatumia maarifa wanayoyapata kwenye vitabu kutatua Changamoto za Dunia hii....achana na habari za akina diamond
Na hilo ndilo lengo la maarifa, kutatua matatizo.

Fedha nyingi, majumba mazuri na magari ya kifahari si kipimo pekee cha kuyapima mafanikio ya mtu, hata jambazi anaweza kupata vyote hivyo kwa njia ya ujambazi.
 
Mnaotaka kuanza kusoma vitabu anzeni na na hivi vitabu kama unapitia changamoto kazini au za ajira na nyingine ndogo ndogo za maisha.

1.THE MAGIC OF THINKING BIG
2.THE POWER OF POSITIVE THINKING
3.HOW TO STOP WORRYING AND START LIVING

Anza kusoma kimoja na hautajutia maishani mwako.
 
Na hilo ndilo lengo la maarifa, kutatua matatizo.

Fedha nyingi, majumba mazuri na magari ya kifahari si kipimo pekee cha kuyapima mafanikio ya mtu, hata jambazi anaweza kupata vyote hivyo kwa njia ya ujambazi.
Watanzania wengi hawapendi kusoma vitabu ndio maana ruge aliwakamata kwasababu alikuwa anasoma sana vitabu na kuwasikiliza watu kama Elon musk na Jack ma interview zao misemo mengi ilikuwa anatoa huko kwa mfano ile kauli yake ya kwamba hapendi watu wanaolalamika kaitoa kwa Jack ma na ile ukitaka nyota pambana kupata mwezi ili hata ukikosa utapata nyota ambayo ndio lengo lako yaani tuwaze vitu vikubwa ametoa kwenye kita cha the magic of THINKING big. I'm out.
 
Tambua tu kwamba wewe kama husomi vitabu umekwisha, uko gizani na umepitwa sana na unaendelea kupitwa.

Mtu asiye msomaji wa vitabu ni sawa na mtu mfu anayetembea. Asiye msomaji wa vitabu hawezi kujua faida na manufaa ya usomaji wa vitabu. Usomaji wa vitabu ni chakula cha akili, huimarisha uwezo wa kufikiri na uwezo wa kujenga hoja. Usomaji wa vitabu huchangamsha akili, huongeza maarifa, huimarisha msamiati na hukuza uwezo wa lugha. Huboresha kumbukumbu, hujenga uwezo wa uchambuzi wa masuala mbalimbali, hujenga uwezo wa kuandika na umakini na pia njia bora ya kupunguza sononi.

Msomaji wa vitabu ana maudhui ya kutosha (Content) kuliko asiyesoma vitabu. Hata inapotokea ubishani au uchangiaji mada utaiona waziwazi tofauti ya wasomaji na wasio wasomaji wa vitabu. Wasio wasomaji badala ya kujadili hoja watapayuka, wataonesha ghadhabu, watashambulia mtu binafsi badala ya kutetea hoja yake. Mara nyingi wasomaji wa vitabu watachangia hoja kwa utulivu, kwa kujenga hoja na mifano na rejea mbalimbali kutoka kwenye vitabu alivyosoma, bila ghadhabu wala kupayuka.


Is reading the key to success?
It has been proven that children who read better, preform better in school and have a more active imagination, leading to a larger world and more possibilities for success.
 
Mnaotaka kuanza kusoma vitabu anzeni na na hivi vitabu kama unapitia changamoto kazini au za ajira na nyingine ndogo ndogo za maisha.

1.THE MAGIC OF THINKING BIG
2.THE POWER OF POSITIVE THINKING
3.HOW TO STOP WORRYING AND START LIVING

Anza kusoma kimoja na hautajutia maishani mwako.
Napendekeza, aanze na HOW TO STOP WORRYING AND START LIVING by Dale Carnegie kisha THE POWER OF POSITIVE THINKING by Dr. Norman V. P.

Hata kama hana changamoto yoyote, avisome tu. Naamini atakuja kubaini kuwa muda alioutumia kuvisoma hakuupoteza bali kauwekeza.
 
Watanzania wengi hawapendi kusoma vitabu ndio maana ruge aliwakamata kwasababu alikuwa anasoma sana vitabu na kuwasikiliza watu kama Elon musk na Jack ma interview zao misemo mengi ilikuwa anatoa huko kwa mfano ile kauli yake ya kwamba hapendi watu wanaolalamika kaitoa kwa Jack ma na ile ukitaka nyota pambana kupata mwezi ili hata ukikosa utapata nyota ambayo ndio lengo lako yaani tuwaze vitu vikubwa ametoa kwenye kita cha the magic of THINKING big. I'm out.
😂😂😂🙏

Usomaji pia utamsaidia mhusika kuepukana na umbea.

Wasomaji wa vitabu wanapokutana, ni kawaida yao kujadili "ideas", lakini wale wengine sasa! Wakikosa cha kuongea huishia kuwajadili watu.
 
Back
Top Bottom