Umesoma vitabu gani mwaka 2021?

Nmemaliza mwaka with this book by Curtis Jackson aka 50 Cent ni kizuri sana aina ya uandishi aliyotumia will make you read it non stop ameelezea maisha yake na mziki challenges alizopata,mkasa wake wa kupigwa risasi tisa na bado akainuka,pia kina principles nzuri za maisha ambazo alitumia mpk kufika hapo alipo, yan nlivosoma hichi kitabu ndo nimegundua mziki Marekani unalipa sanaa ndo maana Wasanii wa mbele kuwa na expensive things ni kawaida this book is great
IMG_20211222_163948_498.JPG
 
Apple store haipo bado. Na kwenye android ni Tz na Kenya tu.
Asante sana. Mimi navitafuta sana vitabu vya Shaaban Robert nisome. Ninacho cha Kusadikika. Na vingine pia nilishavisoma ila nataka tu kuvirudia. Zamani sekondari walikuwa wanavitumia kwenye fasihi. Sijui kama siku hizi bado vinatumika lakini mimi nadhani ili kumuenzi Shaaban Robert ilitakiwa vitumike ili kila mtanzania amsome. Vina fasihi nzuri sana na mafundisho yake ni mazuri. BTW nime-note wewe ni mpenzi wa vitabu. Kuna kitabu cha Trevor Noah kinaitwa Born Crime umeshakisoma? Kama bado basi jitahidi ukisome. Pia kuna kitabu kinaitwa ''I heard you paint houses'' kinaelezea kisa cha kweli kuhusu kupotea kwa Jimmy Hoffa, aliyekuwa kiongozi wa vyama vya wafanyakzi USA. Nacho ni kizuri mno. Na movie yake ipo inaitwa ''The Irishman'' (2019)
 
Asante sana. Mimi navitafuta sana vitabu vya Shaaban Robert nisome. Ninacho cha Kusadikika. Na vingine pia nilishavisoma ila nataka tu kuvirudia. Zamani sekondari walikuwa wanavitumia kwenye fasihi. Sijui kama siku hizi bado vinatumika lakini mimi nadhani ili kumuenzi Shaaban Robert ilitakiwa vitumike ili kila mtanzania amsome. Vina fasihi nzuri sana na mafundisho yake ni mazuri. BTW nime-note wewe ni mpenzi wa vitabu. Kuna kitabu cha Trevor Noah kinaitwa Born Crime umeshakisoma? Kama bado basi jitahidi ukisome. Pia kuna kitabu kinaitwa ''I heard you paint houses'' kinaelezea kisa cha kweli kuhusu kupotea kwa Jimmy Hoffa, aliyekuwa kiongozi wa vyama vya wafanyakzi USA. Nacho ni kizuri mno. Na movie yake ipo inaitwa ''The Irishman'' (2019)
Shaaban yupo vizuri sana. Ni mtu anayestahili tuzo za kimataifa. Kwenye app vipo vitabu vyake vitano(nilivyoorodhesha). Bahati mbaya ndiyo inapatikana Tz na Kenya kwenye android. Born a crime nimekisoma maana Noah namkubali sana, kitabu kizuri.

Nilicheki movie ya The Irishman. Inaonekana kuna mambo mengi sana yalikuwa yanamzunguka huyo bwana(Pacino). Kitabu hicho nimeshaweka kwenye list ya mwakani. Shukrani sana.
 
Kuna kipindi nilipata passion ya kusoma vitabu sijui iliyeyukia wapi, BTW nilifanikiwa kusoma
1. Rich dad, poor dad
2. Think big
3. The Monk who sold his ferrari
4. As a man thinketh
5. Power of subconscious mind
5. How to win and influence people ( sikumaliza)
6. Fools die ( sikumaliza ) .... na vingine vingi nimegusa kidogo
 
Ni mwisho wa mwaka. Kama kawaida tushirikishane vitabu tulivyosoma mwaka huu. Inasaidia kujua vitabu vizuri na kushirikishana maarifa. Mi nimesoma vitabu vifuatavyo, baadhi vilipendekezwa na members humu JF.

1. Bad Samaritans.

Kitabu hiki kinaelezea jinsi ambavyo mataifa tajiri yanavyoshauri, na kulazimisha mataifa masikini kufuata sera za kiuchumi ambazo haziwezi kuwatoa kwenye umaskini. Wanakuwa kama wanazisaidia lakini kumbe wanazididimiza zaidi, ndiyo maana kawaita wasamaria wabaya. Kitabu kizuri sana.

View attachment 2050292

2. Shoe dog

Ni hadithi ya maisha ya muanzilishi wa kampuni ya Nike. Story nzuri sana, huwezi kukiweka chini ukikianza. Kuna muda unaona kabisa jamaa anaenda kufeli. Kitabu hiki ni ushahidi wa kauli "Fortune favors the bold."
View attachment 2050311

3. The fortunes of Africa.

Ukitaka kujua historia ya bara la Africa kwa undani basi soma kitabu hiki. Historia ya kila nchi na kila kona ya Africa imezungumzwa humu. Mtazamo wangu juu ya Africa na watu wake umebadilika sana baada ya kusoma kitabu hiki. Kutokana na kitabu hiki nimeanza kusoma African origin of civilization cha Cheikh Anta Diop.
View attachment 2050313

4. Silmarillion

View attachment 2050295
Hii hadithi inazungumza habari za kabla ya The hobbit na Lord of the rings. Kinazungumza jinsi middle earth ilivyoanza. Ni kizuri kusoma kwa wapenda fantasy.

5. Prisoners of Geography.
View attachment 2050296
Kitabu juu ya global geopolitics. Kitabu kizuri.

6. Mzingile

View attachment 2050297
Mwaka huu nilinunua vitabu vitatu vya Kezilahabi. Hiki Ni moja ya vitabu vigumu kuwahi kukisoma, nahisi kama nimeelewa nusu. Ni kama anazungumzia juu ya dini, siasa, elimu(sayansi). Pengine jinsi sayansi itavyoua dini. Ni kitabu kizuri kama unapenda mambo tata.

7. Rosa Mistika
View attachment 2050300
Riwaya nzuri, labda inahusu malezi ya watoto wakike. Japo binafsi sikubaliani na maoni ya muandishi.

8. Gamba la nyoka

Kitabu hiki kinazungumzia habari za ujamaa na uanzishwaji wa vijiji vya ujamaa. Kizuri sana, pia kimetumia lugha ya kuvutia sana.
View attachment 2050303

9. And then there were none.

Hadithi(mystery) nzuri ya Agatha Christie. Moja ya vitabu vilivyouza sana duniani.

Vitabu vingine ilibidi kuvisoma sababu tulikuwa tunavitafsiri na kuviedit ili kuviweka kwenye maktaba app(unaweza visoma bure humo). Hivi hapa chini.

10. Nchi ya wasioona(The country of the blind).

Humu jamaa alienda nchi ambayo watu wote ni vipofu, alichotarajia kitatokea kikawa kinyume chake.
View attachment 2050304

11. Shamba la wanyama(The animal farm)
Dhihaka juu ya maisha ya kijamaa.
View attachment 2050305

12. Tajiri wa Babeli(The richest man in Babylon)
Kitabu kizuri juu ya uchumi binafsi. Kuna uzi humu nilikiweka.
View attachment 2050306

13. Sanaa ya vita(The art of war).
Kitabu cha kale cha kichina juu ya mbinu za vita.
View attachment 2050307

14. Kiongozi(The prince)
Mbinu za uongozi na siasa. Kipo jukwaa la great thinkers

15. Lulu(The pearl)
Hadithi juu ya mtu aliyepata lulu bora kabisa na yaliyomtokea. Kuna uzi kipo


16. Hadithi ya Sungura aliyeitwa Peter(The tale of Peter rabbit).
Hadithi ya mafunzo kwa watoto juu ya utii.

17. Vazi jipya la mfalme. Jisomee mwenyewe hii hadithi fupi. Kuna uzi humu ipo

18. Kufikirika

Nafikiri kinazungumza juu ya elimu.

19. Kusadikika.----nchi iliyo kwa anga😀

20. Adili na nduguze. Adili alikuwa fala☹️☹️.

21. Maisha yangu na baada ya miaka 50
. Simulizi la maisha ya Shaaban Robert. Kitabu safi sana.

22. Wasifu wa Siti binti Saad. Shaaban Robert anasimulia maisha ya mwanamuziki maarufu kutoka Zanzibar.
Na vitabu hivi vya adventures.
23. Mashimo ya mfalme Sulemani
24. Hadithi ya Allan Quartamainn
25. Kisiwa chenye hazina
Robinson Kruso na kisiwa chake.


26. Nyayo za binadamu wa kale. Historia fupi ya mwanadamu.

27. Hekaya za Abunuwasi na hadithi zingine
28. Alladin na taa ya ajabu
29. Safari saba za Sinbad
30. Alibaba na wezi arobaini.


Kwa sasa nasoma Black Genesis cha Robert Bauval.

Hiki kitabu kinaelezea mwanzo wa Egyptians civilization kabla ya mafarao. Kinaeleza kuwa chanzo cha ustaarabu wa Misri ni waafrika walioishi katika jangwa la sahara(kipindi lina maji). Anatoa ushahidi wake, hasa wa kinajimu. Kitabu kizuri.
View attachment 2050350

Umesoma vitabu gani mwaka huu?

Kiranga Alisina Paula Paul My Next Thirty Years MALCOM LUMUMBA wadau wengi nimewasahau.

View attachment 20593

View attachment 20294

View attachment 2050293

View attachment 2050294
Hivyo vitabu vya Kiswahili unavipata wapi on line?
 
Mwaka huu nimeamua kusoma vitabu vya Simulizi binafsi za watu (Autobiography na biography) zaidi na vingine tofauti vichache. Vitabu nilivyosoma ni;

1. Muhammad Ali his life and times- by Thomas Hauser
Screenshot_20211223-071222_1.jpg


2. My life- by Bill Clinton
Screenshot_20211223-071250_1.jpg


3. Jackal - Carlos the jackal
Screenshot_20211223-071000_1.jpg


4. The Man of Honor (Joseph Bonano) - by Sergio Lalli
Screenshot_20211223-071211_1.jpg


5. Autobiography of Martin Luther King Jr- by Clayborne Carson
Screenshot_20211223-071237_1.jpg


6. Mob Star The Story of John Gotti- by Gene Mustain
Screenshot_20211223-071139_1.jpg



7. It's all about Muhammad (Prophet Muhammad)- by F. W. Burleigh
Screenshot_20211223-071030_1.jpg


8. King David- by Steven L. Mackenzie
Screenshot_20211223-071017_1.jpg


9. Michael Jackson- by J. Randy Teraborreli
Screenshot_20211223-071155_1.jpg


10. Emperor's of Rome- by David Potter
Screenshot_20211223-071047_1.jpg


11. The World dangerous secret societies- by James Jackson
Screenshot_20211223-070912_1.jpg


12. The Tipping point- by Malcolm Gladwell





View attachment 2054130
Screenshot_20211223-073328_1.jpg
 
Hivyo vitabu vya Kiswahili unavipata wapi on line?
Sehemu mbalimbali. Kuna vichache kama viwili vitatu nilivipata Kindle. Vingine nilinunua Mkuki na nyota( vya Shaaban na Kezilahabi). Vingine niliagizia Abebooks, vile vya zamani kwaajili ya app. Cha Bulicheka nilikipata duka la vitabu Peramiho.

Kuna hawa wachapishaji watawa wa Peramiho na Ndanda, wana vitabu adimu sana.

*Kumbe ulisema online, Kindle vipo vichache maana waliacha kuweka vitabu vya kiswahili. Pia kuna app kama UWARIDI, Sim Gazeti na hiyo maktaba, unaweza okoteza.
 
Sehemu mbalimbali. Kuna vichache kama viwili vitatu nilivipata Kindle. Vingine nilinunua Mkuki na nyota( vya Shaaban na Kezilahabi). Vingine niliagizia Abebooks, vile vya zamani kwaajili ya app. Cha Bulicheka nilikipata duka la vitabu Peramiho.

Kuna hawa wachapishaji watawa wa Peramiho na Ndanda, wana vitabu adimu sana.
Hivyo vya on line unaweza kunisaidia? Please
 
Hivyo vya on line unaweza kunisaidia? Please
Kwenye hii maktaba app(by pictuss), karibu vitabu vyote vya kiswahili nilivyoorodhesha hapo vipo. Kasoro hivyo vitatu vya Kezilahabi. Ukipakua hiyo app unasoma bure, na unasoma hata ukiwa offline.
 
Mwaka huu nimeamua kusoma vitabu vya Simulizi binafsi za watu (Autobiography na biography) zaidi na vingine tofauti vichache. Vitabu nilivyosoma ni;

1. Muhammad Ali his life and times- by Thomas Hauser
View attachment 2054108
2. My life- by Bill Clinton
3. Jackal - Carlos the jackal
4. The Man of Honor (Joseph Bonano) - by Sergio Lalli
5. Autobiography of Martin Luther King Jr- by Clayborne Carson
6. Mob Star The Story of John Gotti- by Gene Mustain
7. It's all about Muhammad (Prophet Muhammad)- by F. W. Burleigh
8. King David- by Steven L. Mackenzie
9. Michael Jackson- by J. Randy Teraborreli
10. Emperor's of Rome- by David Potter
11. The World dangerous secret societies- by James Jackson
12. The Tipping point- by Malcolm Gladwell
Sijui ni Tawasifu! Tawasifu gani kali zaidi hapo?
 
Nimesoma vitabu zaidi ya 50; vyengine hivyo ambavyo umeviweka, ila When breath becomes air hiki ni kitabu kizuri mno. Mbinu niliotumia ni kusoma vitabu zaidi ya vitatu kwa wakati mmoja. Nikimaliza chapter ya kitabu hiki badae naenda chengine.
Mkuu tumemiss nyuzi zako, vichwa vyetu vimemiss madini yako ya upande wa kiroho.
tilmikha
 
Sijui ni Tawasifu! Tawasifu gani kali zaidi hapo?
Karibia vyote! Lakin nimependa zaidi
1. Muhammad Ali- Nimeweza mjua zaidi ya kumuona anapigana ngumi, alikuwa philosopher and orator, a proud of black race. Pia kujua yaliyokuwa yanaendelea kambini wakati anajiandaa na mapambano yake makubwa.
2. Michael Jackson- Nimekuja kumjua jamaa vizuri, a selfish person, who liked to blame others for his problems ( Kama ambavyo anamlaumu baba yake kuwa alikuwa anampiga na kumtania kuwa ana pua kubwa, kuwa ndio sababu kubwa ya yeye kuchonga pua.. uongo mtupu!, Au watu wanavyolaumu wazungu kuwa ndio waliomdanganya abadili rangi .. uongo mtupu! Ni yeye mwenyewe, sema siku zote amekuwa mjanja kuwaaminisha watu). Inaelezea maisha toka utotoni mpaka kufa. Utamjua vizuri
3. Martin Luther King Jr- Mchango wake kwa negroes ni mkubwa sana
4. King David- Utaona vitu vingi kwenye biblia vimeandikwa uongo ili kukamilisha propaganda flan iliyokusudiwa na watu walioandika biblia.. lakin pia jinsi biblia yenyewe inavyojicontradict
5. Muhammad- Historia yake na maswali utajiuliza kuhusu hizi dini na imani ( mfano hapo watu wanapoenda kuhiji Hilo jiwe la kaaba, ni mahali wapagani walikuwa wanahiji miaka maelfu kabla hata hajazaliwa Muhammad, ilikuwaje mahali walikuwa wanahiji wapagani pawe sehemu takatifu?) Unazipata zile za ndaani kabisa!!
 
Back
Top Bottom