Umesoma vitabu gani mwaka 2016?

Umesoma vitabu gani mwaka 2016?

Hahah!, kwa kuniweka kwenye mstari tu, hujambo.
Sasa jamani usukumani na Uafrika si tumeshajua, ndo maana tunajaribu kujua na ya wengine ati.

Heaven Sent nae si kama hao wafaransa sasa na huo u model wake, mbona yeye humpi kibano!

Sasa huo ufaransa nitaweza kunyanyua jembe kulima jaruba?
Huyu mtoto sijui ni utapiamlo au nini, nishachoka nakaangalia tu.
Haha nimecheka leo, kuna mtu kaniambia "Hivi wewe HS unavyokula hivyo, chakula kinaenda wapi maana hunenepi" teh
 
Sasa huo ufaransa nitaweza kunyanyua jembe kulima jaruba?
Huyu mtoto sijui ni utapiamlo au nini, nishachoka nakaangalia tu.
Labda nikupump mama.
Ila ndio mwili mzuri, huoni kui anahangaika na vitabu ili awe kama wewe.

Hahah, jamani eti nini..
Yaani mwanao ana bahati sana kuwa natural model, wengine mpaka tutumie vitabu mweh!
 
Red Giant my bro,
Xmas was in Nonde, I lost my bishdo on 24th, Xmas eve.
Asante kwa topic ya leo.
Vitabu.
Ukitaka kumficha siri mtu mweusi, iweke kitabuni.
Hatusomi ndio maana tu watu duni.
Tunajenga nyumba nzuri sana na hazina maktaba na ghala la kuhifadhia nafaka ( siongelei store mnakoweka makorokoro, spare zisizo na kazi, mafyekeo, matairi mabovu etc) Naongelea ghala la vyakula.
Mwaka huu nimesoma Vitabu vichache kabisa.
1. Nimesoma Biblia
2. Makuwadi wa Soko huria
3. Katiba inayopendekezwa
4. Secret of powers
5. Long walk to the freedom
6. Master of the game
7. Memories of midnight
8. From the distance
9. Learn from the best
Makuwadi wa soko huria nilikisoma mwaka uliopita na nilikipenda mno.R.I.P Chachage s.Chachage
 
Planet of Slums labda kinaweza kuwa ni kitabu kizuri.

Lakini hapa wanajamvi sijaona kitabu kinachotufundisha mtu jinsi ya Kumyanyua "Mwafrika".

Hatuoni vitabu vya "Current Affairs au Science and Technology au matters related to health, our well being na hata zaidi mambo yanayohusu KILIMO na pembejeo"

Vitabu vingi sana katika soko la vitabu ni propaganda, personal opinion/perspective/sensational.

Jinsi vitabu vinavyoandikwa, historia ya mwandishi, maisha yake binafsi ni muhimu sana kumjua. Kuna vitu tunavisoma ambavyo havitusaidi kwenye maisha yetu. Waandishi wengi ni wahuni na wavuta unga/bangi/mvinyo. Tumekutana nao.

Ukiingia Maktaba au dula la vitabu nchi za dunia ya Kwanza kama Marekani, vitabu kama vile kitabu cha Malcolm X au Stive Biko au Thabo Mbeki, lazima kiagizwe kutokana na umaarufu wake. Kuna Muamsho mkubwa sana duniani kwa kizazi cha sasa cha watu weusi, labda Tanzania hatulioni lakini WaAfrika wamekataa kulala na kulalishwa/mfumo onevu.
"Black Lives Matter".

Kuna Wazungu na utamaduni wa Ushoga, wanajaribu sana kuisukuma ajenda hii katika mavazi, maadili na hata sheria zinazotawala duniani kote.

Kuna vita biashara, dola chini ya kivuli cha damu, ajenda kugombanisha vikundi/mataifa na kuuza silaha, kubadilisha Utawala na kufaidika na Rasilimali. Ndio maana tunaona mtu anaandikiwa kitabu kuhusu Uislam na mzungu na kukisifia, tunacheka, maana hujuma na dhulma walizofanyiwa Waafrika na Afrika, ndio Waislam wanafanyiwa leo katika nchi zao. Muamar Gadafi hakushamuliwa na M23 au Malaria. Kila kikundi cha Ugaidi kina asili yake kwa Bwana Mkubwa.

Nani anasoma mfumo wa biashara ya Utumwa walivyoanza kukamatwa na kupekwa kwa nguvu na mpaka leo wanajipeleka wenyewe kwa nguvu za hiyari yao na wengi wamepoteza maisha yao kwenye bahari ya Mediterranean?

Kuna ajenda ya kuwafanya Waafrika kuwa"mazuzu" na kuwatawala kutumia dini zilizoanzishwa 1920 huko Marekani kwa rasmi kwa ajili hiyo.

Ukuu na Ubora wa Wazungu (White Supremacy) unapamba moto, kura zilizompa Bwana Tirampu Ushindi na sasa Ulaya inaweza kuelekea huko.

Nani anayesoma ni maana ya Mfumo wa Kizayuni, nia yake ya kuitawala Israel na Afrika?

Kuna kusoma Ujasusi na Uhalifu kwenye hii Mitandao na pia namna ya kufaidika na mitandao hii kibiashara.
Msisahau WikiLeaks.

Nani anasoma jinsi India na China walivyojikamua na kutoka kwenye Ujinga na Umasikini bila ya kuivamia Congo na kuweka waasi huko?

Nani anasoma adhari na madhara za kutumia jela kuzima Upinzani huko Bangladeshi?

Pan Africanism- Utashangaa sasa Fikra za Mwalimu Nyerere zimepamba moto sehemu nyingi hapa Afrika haswa kwenye taasisi nyingi. Vitabu vya Mwalimu Nyerere vimekuwa adimu sana. Kila Kiongozi wa juu anavisoma vitabu vyake.

Wangapi tunasoma maisha ya Nelson Mandela na kuwa na shauku ya kutengeneza amani duniani?

We have to connect to the real world, what makes the headlines, kuanzia bei ya petrol na mpaka bei ya chakula, thamani na faida ya ardhi yetu.
bila hivyo tutajikuta tumetawaliwa bila bendera na kung'ang'ania vitabu vimeandikwa kwa ajili ya biashara tuu na vingine kwa ajili ya kutupambaza.

692cee2f6034490f1546b8fe2c3a6ad7.jpg
 
Bomba kinoma,
Kuna vingine naweza kukutumia kama utavitaka mkuu!
Hilo la Biblia ni jambo jema sana, mimi kwa siku nilihakikisha nasoma angalau sura moja bila kulala nkajikuta nimesoma karibia sura zote.
Hata mie naomba unitumie mkuu, ni mdau wa kusoma vitabu.Mungu akubariki
 
Nimesoma vitabu vifuatavyo.

1. Success Buttons

2. Covenant Wealthy

3. Born to Win ....

Vyote vimeandikwa na David O. Oyedepo
Ni soft copy?Ni vizuri sana!Naomba kuvipata kama ni soft copy.
 
Malcom, you should have my email for some books.

Mwaka jana ulinipa EDM ambayo nimesikiliza zaidi kwenye playlist yangu
Reload-Sebastian Igrosso

Red Giant pia nashukuru sana

Kweli mkuu ntakucheki kwenye PM.
 
Back
Top Bottom