Asante kwa vitabu naomba unisadie nawezaje kuvipata mim napenda kusoma sana vitabu tatizo ni jinsi gan ya kuvipata hivyo vitabu. Nisadie maduka mazur ninunue
1:Vitabu vingi vinapatikana katika maduka ya vitabu, Kwa dsm unaweza kwenda posta kuna bookshops pale mitaa sijaikalili utapata baadhi.
2:Vitabu vingine huwa vinamwagwa tu mabarabarani mchanganyiko maeneo ya ubungo na Posta pale karibu na Tume ya maadili kama sikosei unaweza kuwaona wale jamaa ukiwatajia jina wanaweza kukutafutia.
3:Vitabu vingine hasa vya kikristo unaweza kuvipata pale Mikocheni karibu na kwa Warioba kuna duka la vitabu nimelisahau jina lakini kuna kibao barabarani.
4: Vitabu vingine vinapatikana Ukishuka Victoria kama unaelekea Hospitali ya Kairuki mkono wa kulia. Kuna taasisi pale ila ninakumbuka kwa wanafunzi wa UDSM ukiwa na kadi/kitambulisho au Kuna Dr mmoja anaitwa Mrindoko anaweza kukupa ramani au ukaenda kujieleza mwenyewe. Pale huwa linakuja kontena la vitabu mchanganyiko unaweza kujipatia vitabu of your interest niliwahi kwenda zamani sijui kama bado inaendelea wanauza bei rahisi maana wanapewa kama misaada.
5:Vitabu vingine unaweza kuvisoma Online kupitia Google books
6:Vingi mimi huwa navigoogle .pdf nikisha kijua jina na mwandishi. Nitakisaka hadi napata copy na kukiweka kwenye notepad maanalum kwa kazi hiyo.
7:Vingine unavitafuta Amazon unakiagiza kwa kufuata utaratibu unapata. Au kama unarafikki nje ya nchi au SA unamwomba anapokuja akuletee copy ya kitabu unachokitafuta.
8:Unaweza pia kununua softcopy online au kujisajiri katika online libraries huko duniani ukawa na uwezo wa kupata access ya kitabu chochote.
9:VIngine unavipatata kwa wadau kama humu. Unaweza kuandika mwenye softcopy ya kitabu flani, na kati ta watu zaidi ya lakin nne huwezi kukosa. Njia nyingine ni kujiunga kwenye Reading clubs hata hapa bongo zipo huko utakutana na kila aina ya watu wenye vitabu vya kila aina.
10:Vitabu vingine unavipata kwenye mikutano ya kidini,Kijamii, siasa,au workshops, Mfano mimi The joy of encouregement nilienda kwenye mkutano flani wa kidini/protestants siku moja kwa lengo la kutafuta kitabu cha kununua na nikakinunua na kuondoka zangu.
Kuna options nyingi ya kupata vitabu hata bure ikiwezekana. Kuna vingine niliwahi kuwaandikia Email shirika moja huko us zamani za kuomba vitabu nikatumiwa box zima posta baada ya muda kidogo.
Hayo ndio maoni yangu wengine wanaweza kusaidia zaidi mkuu