Expensive life
JF-Expert Member
- May 2, 2020
- 1,703
- 5,477
Ndugu zangu ama kweli bahati haiji mara mbili.
Huu ni ushuhuda nilionao dhidi ya rafiki yangu kipenzi, rafiki yangu huyu baada tu ya kumaliza masomo yake. Mungu si Athumani ni bahati iliyoje alipata kazi haraka sana huko bandarini kwenye moja ya kampuni kubwa sana ya mafuta.
Kaka yake ni moja ya viongozi wakubwa tu huko jeshini, hivyo ilikuwa ni rahisi yeye kupata kazi kutokana na convection aliyonayo kaka yake.
Rafiki yangu maisha yalimnyookea sana huko bandarini, baada ya muda mfupi tu nuru ilionekana alitakata vibaya mno na kitambi kikamtoka kutokana na mafedha.
Marafiki wakaongezeka kwa wingi sana, kazini alikuwa aendi tena kwa daladala, anapiga tu simu tex inakuja kumchukua jioni pia.
Mtaani wakampachika jina la tajiri kibonge, kwa maelezo yake kipindi kile alikuwa anaweza kuingiza si chini ya 300k mpaka 700k kwa siku kama mambo yakiwa mazuri hiyo ni kando ya mshahara.
mambo yakibadilika mwaka 2016 baada ya mwamba John Joseph pombe magufuli kuingia madarakani ( R.I.p)
Mirija yote ya upigaji ilipoea ghafla, akawa anakosa hata 10k kwa siku akawa anategemea mshahara pekee.
Mimi kama rafiki yake kwa kuwa alikuwa akinishirikisha mambo yake mara kwa mara nikuwa nikikumuasa, ndugu yangu nunua hata kiwanja ujenge unachezea sana pesa.
Kama mnavyojua cha mtu ni chake, kutokana na status aliyokuwa nayo mtaani, ilimuwia vigumu sana kuyaishi maisha ya mshahara tu.
Mambo yalizidi kuwa mabaya zaidi 2020 baada ya janga la corona, yeye ni mmoja ya wafanyakazi waliosimashwa kazi kipindi kile kutokana na janga lile.
Bahati alikuwa na akiba nzuri tu bank, hivyo akafungua duka la kuuza nafaka maisha yakaendelea, duka lilitembea lakini halikudumu sana likafa.
Family anayo amepanga kinondoni kodi ya nyumba mzigo, dahhh kutokana na msongo wa mawazo akajiingiza kwenye uvutaji wa bangi kupindukia.
Kutokana na uzoefu aliokuwa nao bandarini alitafuta kazi akapata tena ila sasa siyo nafasi ile aliyokuwa nayo hapo awali upigaji upo ila ile nafasi aliyokuwa nayo hapo awali maokoto yalikuwa yanajileta yenyewe.
Umeshawahi kupata bahati ya kutoboa maisha ukaichezea?
Huu ni ushuhuda nilionao dhidi ya rafiki yangu kipenzi, rafiki yangu huyu baada tu ya kumaliza masomo yake. Mungu si Athumani ni bahati iliyoje alipata kazi haraka sana huko bandarini kwenye moja ya kampuni kubwa sana ya mafuta.
Kaka yake ni moja ya viongozi wakubwa tu huko jeshini, hivyo ilikuwa ni rahisi yeye kupata kazi kutokana na convection aliyonayo kaka yake.
Rafiki yangu maisha yalimnyookea sana huko bandarini, baada ya muda mfupi tu nuru ilionekana alitakata vibaya mno na kitambi kikamtoka kutokana na mafedha.
Marafiki wakaongezeka kwa wingi sana, kazini alikuwa aendi tena kwa daladala, anapiga tu simu tex inakuja kumchukua jioni pia.
Mtaani wakampachika jina la tajiri kibonge, kwa maelezo yake kipindi kile alikuwa anaweza kuingiza si chini ya 300k mpaka 700k kwa siku kama mambo yakiwa mazuri hiyo ni kando ya mshahara.
mambo yakibadilika mwaka 2016 baada ya mwamba John Joseph pombe magufuli kuingia madarakani ( R.I.p)
Mirija yote ya upigaji ilipoea ghafla, akawa anakosa hata 10k kwa siku akawa anategemea mshahara pekee.
Mimi kama rafiki yake kwa kuwa alikuwa akinishirikisha mambo yake mara kwa mara nikuwa nikikumuasa, ndugu yangu nunua hata kiwanja ujenge unachezea sana pesa.
Kama mnavyojua cha mtu ni chake, kutokana na status aliyokuwa nayo mtaani, ilimuwia vigumu sana kuyaishi maisha ya mshahara tu.
Mambo yalizidi kuwa mabaya zaidi 2020 baada ya janga la corona, yeye ni mmoja ya wafanyakazi waliosimashwa kazi kipindi kile kutokana na janga lile.
Bahati alikuwa na akiba nzuri tu bank, hivyo akafungua duka la kuuza nafaka maisha yakaendelea, duka lilitembea lakini halikudumu sana likafa.
Family anayo amepanga kinondoni kodi ya nyumba mzigo, dahhh kutokana na msongo wa mawazo akajiingiza kwenye uvutaji wa bangi kupindukia.
Kutokana na uzoefu aliokuwa nao bandarini alitafuta kazi akapata tena ila sasa siyo nafasi ile aliyokuwa nayo hapo awali upigaji upo ila ile nafasi aliyokuwa nayo hapo awali maokoto yalikuwa yanajileta yenyewe.
Umeshawahi kupata bahati ya kutoboa maisha ukaichezea?