Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 576
- 1,626
Wakuu,
Uzito uliopitiliza, shape na nguvu za kiume na mambo ambayo yanasumbua sana watu na kuna baadhi wako radhi kufanya chochote ili atimize moja la hitaji lake hapo juu.
Dawa hizo nyingi hazitambuliki na mamlaka za dawa na chakula, wanaokuuzia wengi hawajui zimechanganywa na nini, na hata wanaodai kutengeneza dawa hizo wenyewe hawana utaalamu kuhusu tiba.
Baadhi ya michanganyiko hii inakuwa na sumu kutokana na ukweli kwamba wanaotengeneza hawana utaalamu wowote na baadhi hawajali nini kinachanganya hata kama kitamdhuru mtumiaji mradi yeye ameingiza pesa.
Unaweza usipate madhara hayo mara baada tu ya kutumia, lakini sumu ikabaki kwenye mwili wako baada ya miaka hata kumi huko ndio ukaanza kuona madhara yake.
Kwenu wakuu, umewahi kutumia dawa hizo kutoka mtandaoni? Unajua ni kitu gani hasa uliingiza mwilini?
Uzito uliopitiliza, shape na nguvu za kiume na mambo ambayo yanasumbua sana watu na kuna baadhi wako radhi kufanya chochote ili atimize moja la hitaji lake hapo juu.
Dawa hizo nyingi hazitambuliki na mamlaka za dawa na chakula, wanaokuuzia wengi hawajui zimechanganywa na nini, na hata wanaodai kutengeneza dawa hizo wenyewe hawana utaalamu kuhusu tiba.
Baadhi ya michanganyiko hii inakuwa na sumu kutokana na ukweli kwamba wanaotengeneza hawana utaalamu wowote na baadhi hawajali nini kinachanganya hata kama kitamdhuru mtumiaji mradi yeye ameingiza pesa.
Unaweza usipate madhara hayo mara baada tu ya kutumia, lakini sumu ikabaki kwenye mwili wako baada ya miaka hata kumi huko ndio ukaanza kuona madhara yake.
Kwenu wakuu, umewahi kutumia dawa hizo kutoka mtandaoni? Unajua ni kitu gani hasa uliingiza mwilini?