Umeoa Msukuma?

Umeoa Msukuma?

Mhh naomba kuuliza hivi Teddy Kalonga na Miriam Gerald ni wenyeji wa wapi vile????

Sijawahi kuona tatizo lolote kwenye tabia ya Teddy Kalonga! Labda kuwa maarufu ni sehemu ya tabia mbaya hapo sawa!

I dought Miriam Gerald's credentials as a Sukuma. Sio kila mtu anayeishi Mwanza ni Msukumua. Yawezekana wazazi wake wanaishi na kufanya kazi Mwanza lakini sio Wasukuma!
 
wasukuma wana heshima sana kwa mwanaume, pesa sio isuue saana kwao,wanajua kupenda kweli kweli ila pia wanatabia ya kurundikana kwa ndugu.

Kama ukarimu umekuwa sifa mbaya basi mimi najivunia hiyo sifa mbaya.
 
Jamani mimi mbona Mwanza na Shinyanga huwa nakwenda mara kwa mara ila siwaoni?

Unaenda Mwanza na Shinyanga mjini ama??,Jaribu uende vijijini(wilayani) kama Meatu,Maswa,Kahama(maeneo ya vijijini),Malya,Tinde,Bukombe,Msalala,Buzilayombo,Bushilombo,Mwamashimba.Geita,Magu,Kwimba...Pia maeneo ya Nzega,Igunga n.k...Huko ndo utawaona hasa wamama wa kisukuma mkuu
 
Ni kweli wana adabu sana lakini zaidi ya yote wanajua mambo ya fargha,nafikiri wanafunzwa jinsi ya kuishi na waume zao.sihadithiwi ninae.

Jamani punguzeni unazi kidogo najua kuacha haiwezekani.
Halfu Pakajimmy nilikuwa nimesahau kidogo na hii ni muhimu sana ukalijua.Jamani wasukuma wanakula msosi mwingi nakwambia unatakiwa uwe na bajeti kubwa sana ya msosi.Mwanamke wa kisukuma mmoja ni sawa na wanawake wananne wa makabila mengi kwa upande wa ulaji wa chakula.Ndio maana utakuta wanawake wa kisukuma wana miili mikubwa sana ukilinganisha na wanawake wengine.
 
Huyo wako katokea Bukoba na sasa anajifanya Msukuma. Au usikute katokea Ukerewe. Unajua Walerewe wengi sana wanatamanigi kuwa Wasukuma. Dizaini umepata kanyaboya wewe
Julius unataka ugomvi na raia wa huko mahali(BK), NA ni wengi sana pia hapa ndani kuliko nyie wasukuma!
 
wasukuma wana heshima sana kwa mwanaume, pesa sio isuue saana kwao,wanajua kupenda kweli kweli ila pia wanatabia ya kurundikana kwa ndugu.

Kiongozi,kwani kurundikana ndugu ni kosa??,hii ni ishara ya umoja,upendo na mshikamano(Sifa nyingine hii)...Hatuna mambo ya uchoyo na kujitenga sisi bana

Pia wamama wa kisukuma ni wachapa kazi hasa
 
Jamani punguzeni unazi kidogo najua kuacha haiwezekani.
Halfu Pakajimmy nilikuwa nimesahau kidogo na hii ni muhimu sana ukalijua.Jamani wasukuma wanakula msosi mwingi nakwambia unatakiwa uwe na bajeti kubwa sana ya msosi.Mwanamke wa kisukuma mmoja ni sawa na wanawake wananne wa makabila mengi kwa upande wa ulaji wa chakula.Ndio maana utakuta wanawake wa kisukuma wana miili mikubwa sana ukilinganisha na wanawake wengine.

Kabonde, nadhani amani inaendelea!

Lakini nadhani kula sana siyo shida kubwa saana ukilinganisha na matatizo ya wanawake wa makabila haya mengineyo!

Wasukuma tupeni jibu la hii tetesi ya Kabonde!
 
Unaenda Mwanza na Shinyanga mjini ama??,Jaribu uende vijijini(wilayani) kama Meatu,Maswa,Kahama(maeneo ya vijijini),Malya,Tinde,Bukombe,Msalala,Buzilayombo,Bushilombo,Mwamashimba.Geita,Magu,Kwimba...Pia maeneo ya Nzega,Igunga n.k...Huko ndo utawaona hasa wamama wa kisukuma mkuu

Muda sasa! Labda nifanye ''out-sourcing'' kwenye suala hili! 🙂 Maana huko utakwendaje kama huna mwenyeji?
 
Kiongozi,kwani kurundikana ndugu ni kosa??,hii ni ishara ya umoja,upendo na mshikamano(Sifa nyingine hii)...Hatuna mambo ya uchoyo na kujitenga sisi bana

Pia wamama wa kisukuma ni wachapa kazi hasa

Usawa wenyewe bado haujakaa vizuri chumba kimoja bajeti ya chakula tuaijua wenyewe,ndugu wanaanza kufurika hivi tutaweza kumudu maisha kweli.Halafu mtu kakaa kwako mwezi mzima hakuna anachosaidia akiataka kuondoka anaomba nauli fikiria unaishi Lindi itakuwaje ?
 
Kabonde, nadhani amani inaendelea!

Lakini nadhani kula sana siyo shida kubwa saana ukilinganisha na matatizo ya wanawake wa makabila haya mengineyo!

Wasukuma tupeni jibu la hii tetesi ya Kabonde!

Kula sana kwani ni tatizo? Those people are giants na wanafanya kazi sana, ndio maana wanakula. Huwezi kulinganisha Msukuma na Mzaramo! Mzaramo ni mvivu wa kufanya kazi na ndio maana hata kula yake ni ya shida, kwa hiyo anakula kidogo pia kwa kuwa ndicho alichoweza kuzalisha, haimaanishi akiletewa chakula kingi hatakula.

Msukuma kwake chakula sio tatizo.
 
Hao kama wana damu ya Kisukuma basi lazima itakuwa imechanganyika na ya makabila mengine. Sio Wasukuma pure

Teddy Kalonga ni msukuma Pure, Baba na Mama wote ni Wasukuma pure, nadhani ni watu wa Ntuzu zone (Bariadi, Maswa na Magu)
 
Teddy Kalonga ni msukuma Pure, Baba na Mama wote ni Wasukuma pure, nadhani ni watu wa Ntuzu zone (Bariadi, Maswa na Magu)
Tedy ana ubaya gani kwani?ni binti mrembo,hard working,ana upendo.
 
Kabonde, nadhani amani inaendelea!

Lakini nadhani kula sana siyo shida kubwa saana ukilinganisha na matatizo ya wanawake wa makabila haya mengineyo!

Wasukuma tupeni jibu la hii tetesi ya Kabonde!

Ni shida sana tena kubwa kuliko unavyofikiri,usisahau watakuja ndugus,majirani zake wa uko usukumani,rafiki zake wa zamani sasa niambie gunia moja la unga baada ya wiki lazima uende sokoni labda kama unalima ndio utawaweza lakini kama ni unga wa kupima dukani nakwambia utaongea mwenyewe barabarani.Unajua wasukuma wanavyopenda kula ugali mkubwa,
 
Usawa wenyewe bado haujakaa vizuri chumba kimoja bajeti ya chakula tuaijua wenyewe,ndugu wanaanza kufurika hivi tutaweza kumudu maisha kweli.Halafu mtu kakaa kwako mwezi mzima hakuna anachosaidia akiataka kuondoka anaomba nauli fikiria unaishi Lindi itakuwaje ?

Hilo ni tatizo dogo sana ambalo mnaweza kulizungumza wewe na mkeo na kukubaliana jinsi ya kukabiliana nalo!
 

Usawa wenyewe bado haujakaa vizuri chumba kimoja bajeti ya chakula tuaijua wenyewe,ndugu wanaanza kufurika hivi tutaweza kumudu maisha kweli.Halafu mtu kakaa kwako mwezi mzima hakuna anachosaidia akiataka kuondoka anaomba nauli fikiria unaishi Lindi itakuwaje ?

Huo ndio utamaduni wetu wasukuma mkuu,hayo ya ndugu kufurika unayasema wewe,lakini kwetu sisi pouwa tu,ni kama utamaduni tu sasa(sema kwa watu wa mjini wataona ni kero),nenda sehemu yoyote yenye wasukuma(maeneo ya vijijini ya wilaya za mikoa ya Mwanza,Shinyanga na kidogo Tabora,pia maeneo ya bonde la Usangu na Songwe-Chunya) utaona ni jinsi gani wasukuma wanavyoishi kwa umoja,upendo na mshikamano...Hakuna uchoyo wala kuwaza fulani atakula nini maana vyakula vipo(tunalima sana mahindi,mtama,uwele,viazi vitamu-manumbu)mang'ombe yapo(tunapata maziwa-mtindi wa kuchekecha na samli,nyama...pesa),pia tunalima Pamba na Alizeti tunapata hela za kutosha kiasi kwamba tunakuwa hatuna hata muda wa kuwaza kwamba aaargh hawa watu mbona wamekuwa wengi hapa nyumbani kwangu...Ukweli najivunia sana kuwa Msukuma aisee
 
Unaenda Mwanza na Shinyanga mjini ama??,Jaribu uende vijijini(wilayani) kama Meatu,Maswa,Kahama(maeneo ya vijijini),Malya,Tinde,Bukombe,Msalala,Buzilayombo,Bushilombo,Mwamashimba.Geita,Magu,Kwimba...Pia maeneo ya Nzega,Igunga n.k...Huko ndo utawaona hasa wamama wa kisukuma mkuu

Shinyanga na Mwanza mjini wamejaa watu wa mikoa mingine. Kule ndani ndani kama Kanadi na Nhelegani ndio kwenyewe kule
 
Ni shida sana tena kubwa kuliko unavyofikiri,usisahau watakuja ndugus,majirani zake wa uko usukumani,rafiki zake wa zamani sasa niambie gunia moja la unga baada ya wiki lazima uende sokoni labda kama unalima ndio utawaweza lakini kama ni unga wa kupima dukani nakwambia utaongea mwenyewe barabarani.Unajua wasukuma wanavyopenda kula ugali mkubwa,
Kabonde kwanza nadhani wewe ni MTANI WA KABILA HILI, unless if you prove me wrong!!
 
This is too general, sio wote, najua wapo ila sio mademu wote wa kisukuma. Nishabahatika kumuona mmoja ambaye yeye alikuwa anamdunda sana mumewe, by then nilikuwa kijana mdogo alikuwa anaogopwa mtaa mzima.

Katika kila pool ya watu katika jamii, always kuna baadhi ya wachache ambao huwa hawa-conform. Katika hili, kama sample ni kubwa unachoangalia ni conformity ya majority.
 
Huo ndio utamaduni wetu wasukuma mkuu,hayo ya ndugu kufurika unayasema wewe,lakini kwetu sisi pouwa tu,ni kama utamaduni tu sasa(sema kwa watu wa mjini wataona ni kero),nenda sehemu yoyote yenye wasukuma(maeneo ya vijijini ya wilaya za mikoa ya Mwanza,Shinyanga na kidogo Tabora,pia maeneo ya bonde la Usangu na Songwe-Chunya) utaona ni jinsi gani wasukuma wanavyoishi kwa umoja,upendo na mshikamano...Hakuna uchoyo wala kuwaza fulani atakula nini maana vyakula vipo(tunalima sana mahindi,mtama,uwele,viazi vitamu-manumbu)mang'ombe yapo(tunapata maziwa-mtindi wa kuchekecha na samli,nyama...pesa),pia tunalima Pamba na Alizeti tunapata hela za kutosha kiasi kwamba tunakuwa hatuna hata muda wa kuwaza kwamba aaargh hawa watu mbona wamekuwa wengi hapa nyumbani kwangu...Ukweli najivunia sana kuwa Msukuma aisee

Hapo umepiga Ikulu ''Mwanangwa''.

Usukumani ukiuliza njia kama umepotea huko vijijini wanakushauri ukae chini uwaeleze kwa kirefu unapotoka na unakokwenda.

Wakiona ni mbali sana kwa muda huo, wanakushauri ulale hapo kwao ili uendelee na safari yako kesho yake. Basi hapo utakula, utaoga na utalala. Hata kama utalala kwenye ngozi lakini ule ukarimu tu unatosha kukuonyesha kwamba umefika kwenye jamii ya watu wastaraabu.
 
Katika kila pool ya watu katika jamii, always kuna baadhi ya wachache ambao huwa hawa-conform. Katika hili, kama sample ni kubwa unachoangalia ni conformity ya majority.

Una akili sana! 🙂 Nimekugongea SENKSI!!
 
Back
Top Bottom